Parliament of Tanzania

Contributions By: Hon. Edwin Mgante Sannda

All Contributions

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa jina naitwa Edwin Sannda, wengi huwa wakisikia hili jina wanashtuka kidogo; lakini msishtuke, Sannda hii ni nzuri tu, siyo kama ile ya kuzikia. Ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Mjini. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, nachukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuwepo hapa, lakini pia nikishukuru chama changu kwa kupitisha jina hatimaye likaenda kupigiwa kura. Nawashukuru wadau wangu wote, familia, ndugu jamaa na marafiki na hatimaye wapiga kura wa Jimbo la Kondoa Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, moja kwa moja napenda kuchangia kwenye hotuba ya Rais. Kwanza kabisa naipongeza; imekaa vizuri, imegusa nyanja zote, lakini pia nawapongeza kwa wale waliotupa Mpango wa miaka mitano wa Maendeleo, wameakisi moja kwa moja hotuba ya Rais, wamegusa kila nyanja, nawapongeza sana. Pia yule aliyewasilisha ule mpango ni pacha wangu, kwa hiyo naye nampongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nichangie pale kwa maana ya vitu vikubwa vinne. Mpango mzuri, lakini huwa tatizo letu linakwenda kwenye utekelezaji (execution). Nawaomba hasa wale Wizara ya Fedha na Mipango na Serikali nzima kwa ujumla, suala la utekelezaji ndiyo liwe msingi mkubwa wa kuangalia (execution). (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, yameongelewa mengi sana kuhusiana na government efficiency na effectiveness (ufanisi wa Serikali), lakini kila tunapoongelea ufanisi wa Serikali, tunazungumzia kupunguza gharama na kubana matumizi. Napenda pale kwenye suala la efficiency ya Serikali tuongezee suala la delivery time, kukamilisha miradi, kufikisha huduma na yenyewe mwisho wa siku inaingia kwenye gharama. Tukiweza kufanikisha eneo hili napo tutakuwa tumefanya vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mbali na delivery pia suala la ubora. Tunatengeneza vitu, tunakamilisha miradi chini ya viwango, hatimaye tunahitaji kufanya marekebisho muda siyo mrefu, ambayo pia ni gharama tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwenye government efficiency, labda tungeangalia sehemu tatu, gharama inavyozungumziwa ya kwanza, delivery time, pamoja na quality ya huduma zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu cha tatu ningependa kuzungumzia suala la ubunifu kidogo. Kila mmoja aliyesimama kati yetu hapa anavutia kwake, tatizo liko hili, huduma zinahitajika hizi lakini mwisho wa siku ni lazima tujue ni namna gani tutatoka nje ya box tuwe wabunifu kuongeza kipato chetu. Tukiwa na kipato kikubwa kabisa kama nchi, ina maana hizi huduma zote zitafika, siyo tunagombea zile rasilimali chache. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nafikiri, tujaribu kuangalia kama inawezekana, maana na sisi wenyewe ndio tunaotunga sheria, tukawekeza kwenye baadhi ya sekta. Hawa wawekezaji wakubwa wanaokuja au sekta ambazo tutaziona ni nzuri kabisa zitatuletea tija, mbali na kodi tunayopata, vyanzo vya kawaida vya mapato ya Serikali, lakini tuwe na hisa tuwekeze ili tuwe tunapata magawio yaongeze katika Pato zima la Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri Wizara ya Fedha pamoja na nyingine, hebu tuangalie eneo hili, kama litahitaji sheria ya kubadilishwa au kutungwa, siyo kwamba tunaenda kufanya biashara per se lakini angalau tuwe na uwekezaji na sisi tuongeze vyanzo vya mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho ninalotaka kuongea ni suala la…
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza kabisa naanza na itifaki ya pongezi kwa Rais wetu, Waziri Mkuu kwa mpango mzuri na timu yake nzima ya Mawaziri na Manaibu Waziri.
Kwa ujumla mpango huu ni mzuri sana, nami nimeupitia, nimeuangalia kwa kina, kwa upana wake na kwa ujumla wake ni mpango mzuri kweli kweli; wanastahili pongezi sana. However, kuna marekebisho kadhaa yanahitajika katika maeneo mbalimbali ili mwisho tuweze kuunga mkono hoja kikamilifu. Marekebisho hayo ndiyo yataukamilisha mpango huu uwe bora zaidi ya ulivyo sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nichangie maeneo mawili tu kwa leo; la kwanza ni lile la uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Tukienda ukurasa wa 15, wanasema Serikali itaendelea kutoa mafunzo ya ujasiriamali na kuwadhamini wajasiriamali wenye miradi inayokidhi vigezo kwenye taasisi za fedha ili wapate mikopo yenye masharti nafuu.
Haya mafunzo pamoja na mpango ule ambao upo ukurasa wa 16 wa shilingi milioni 50 kila kijiji, nafikiri mpango ni mzuri, utekelezaji wake ndiyo huwa tatizo.
Sasa ili tuweze kusaidia, nasi Wabunge kwanza tushirikishwe katika mpango wa utekelezaji mapema, tuwe nao. Tutakachofanya, kikubwa zaidi tunaenda kuandaa watu wetu, kwa sababu mpaka sasa hivi, wana matumaini makubwa kweli kweli, wanasubiri, wana kiu na kadri wanavyosubiri, tunatoa fursa ya maneno ambayo huenda siyo sahihi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge tukiupata mapema kama Wawakilishi wa wale wananchi, tukaenda kule, tukauangalia, tukaanza kuujaribu, tukaanza kuustadi kwa kina, tutaweza kubaini upungufu na kuufanyia marekebisho. Kwa hiyo, kabla ya utekelezaji, tutakuwa tumeweka kila kitu kimekaa sawasawa na hatimaye muda wa utekelezaji unapofika, bajeti inakuwa imekaa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine napenda kushauri na hili lipo kwenye Wizara ya Fedha nafikiri kuna umuhimu sana katika maeneo ya kuboresha, ni kutengeneza mechanism ya monitoring na control, watu watakuwa wameshapata zile fursa, fedha zimetolewa lakini unawezaje kuhakikisha na kutengeneza mfumo wa kwamba tunawakagua hawa watu kadri wanavyokwenda? Vinginevyo hizi fedha zitatoka, mikopo itatolewa, lakini lile lengo tunalotaka lifikiwe mwisho, watu wafanikiwe, wapunguze umaskini, wainue uchumi, tutakuwa tumekwama kama hatutatengeneza mfumo na muundo imara wa monitoring na control.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale wanapokosea, kweli watu wetu sio wote wana ujuzi wa ujasiriamali, wanafundishwa leo, halafu unamkabidhi hela mtu ambaye huenda hajashika kiwango hicho cha hela kwa muda mrefu au labda toka azaliwe, halafu ukategemea atafanikisha kadri tunavyotegemea, inaweza ikawa mtihani mkubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naishauri Serikali, tutengeneze mechanism nzuri sana ya kuweza kuwachunguza na kuwasimamia hawa mpaka mwisho tuone matokeo yake. Hapo kweli tutakuwa tumefanikisha zoezi na azma yetu ya kuwawezesha wananchi wetu kiuchumi ili tuweze kupunguza umaskini. Hili ndilo eneo ambalo tukiwawezesha hawa wananchi wa kawaida tunaosema ni maskini, ile macro-economy itakuwa supported vizuri sana na wananchi wa kawaida kwa sababu kila mmoja sasa atakuwa kidogo ana nguvu yake na anaweza kuendesha maisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo moja la uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, naomba niachie hapo, nafikiri Waziri wetu wa Fedha na Mipango amelipata na Naibu wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia suala zima la elimu. Mpango wa elimu ni mzuri, maeneo yote yameelezewa. Hili lipo kwenye ukurasa wa 49, naomba nisome kidogo mwone jinsi ambavyo inatakiwa iwe. Anasema:
“Hatua zinazochukuliwa zinalenga kuhakikisha kwamba elimu ya Tanzania ni ya viwango vya ubora wa hali ya juu ili kuwawezesha vijana wetu kukabiliana na changamoto za maisha ya kujiajiri wenyewe na kumudu ushindani katika soko la ajira la ndani kikanda na Kimataifa.” Mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii kauli ni nzuri sana na imewasilishwa vizuri kweli kweli, lakini lazima tuangalie kwa ujumla wake, ule mfumo, muundo na taratibu za utoaji wetu wa elimu kuanzia awali zinamjenga mtu kwa namna gani. Tunataka practically ziweze kutoa matunda au matokeo ya wanafunzi ambao ni competent, kwenye soko la ajira tukienda huko, tunaona namna tunavyo-perform.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukilinganishwa tu na wenzetu wengine wa nchi za jirani na hapa tumezungumzia kikanda na tumezungumzia Kimataifa, competence yetu kwa kweli inahitaji kuboreshwa sana. Hili ndilo eneo ambalo kwenye hotuba hii ya Waziri Mkuu, kuna umuhimu sana wa kuliboresha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ubora tuuteremshe chini practically, tuhakikishe mifumo, muundo na utaratibu wetu wa kutoa elimu kuanzia chini, unamjenga kijana awe na uwezo, ajiamini, ajitambue kwenye suala zima la nidhamu ya mafanikio.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nizungumze jambo moja ambalo kwa kweli linanisikitisha na Naibu Waziri wa Elimu nafikiri yupo hapa. Watu wanaopata Division IV wanachukuliwa kwenda kuwa Walimu.
Sasa kipindi chote hiki ambacho tulikuwa na Walimu waliopata Division IV ndio wanakwenda kufundisha watu, halafu tunataka kujenga matunda ya watu ambao wana kiwango bora cha elimu, hapa kidogo pana mtihani, lazima tubadilishe hili, haiwezekani!
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatumia neno failure, kwamba Division IV ni failure ingawa kwa sasa kiwango cha Division IV inaonekana ni ufaulu. Sitaki kuamini kama ni ufaulu na ipo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza pia tubadilishe, ufaulu uishie Division III. Unapozungumzia Division one, two, three, ndiyo ufaulu. Sasa tunapiga mahesabu mpaka Division IV mtu anaaminika kwamba amefaulu halafu ndio hao wanaenda kufundisha, halafu tunategemea watoe product ambazo ni nzuri! Siyo rahisi! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka tujenge uwezo, tujenge wanafunzi wanaotoka wanajiamini huko nje; akienda anajieleza, anajiamini. Akiambiwa afanye kazi, ana competence ya kutosha.
Kwa hiyo, napenda nitumie fursa hii kuwasilisha marekebisho kwenye hii hotuba kwamba, suala zima la elimu, dhana ni nzuri sana, lakini ni lazima tuboreshe mfumo na muundo, utujengee na kutoa competence katika elimu yetu kuanzia elementary mpaka Chuo Kikuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, kubwa nataka niwasilishe hili la Division III kuendelea kuwa ufaulu, nashauri libadilishwe. Sasa tukishafanya maboresho hayo yote, kimsingi nitakuwa sina shida ya kuunga mkono hoja hii. Ahsante sana.

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza niende moja kwa moja kwenye ushauri, leo nitakuwa nafanya zoezi la ushauri tu kwa Wizara na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo kama linanishangaza kidogo, ninaposikiliza Wabunge wenzangu wote na ninapofuatilia hali halisi ya migogoro inayotokana na mwingiliano mkubwa kati ya maeneo ya hifadhi pamoja na maeneo ya makazi nashangaa sijaona kama jambo hili limewekewa uzito sana kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri na nilitegemea kwa kuwa hili ni tatizo kubwa sana lazima ungelizungumzia kwa kina sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, karibu kila pori la akiba, kila eneo la hifadhi ni vurumai tu. Tumesikia madhara makubwa ya migogoro, tumesikia vifo, tumesikia wanyama wanadhurika ndiyo maana tunazungumzia habari ya kufanya mipango mizuri ya ardhi kwa ajili ya kuweza kutenga maeneo ya ufugaji, maeneo ya hifadhi na maeneo ya kilimo. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri sijaona uzito unaostahili kwenye hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niende mbele kidogo kwamba, tatizo hili limekuwa la muda mrefu sana, kila kwenye pori kelele ni hizo, miaka nenda, miaka rudi ni kero kubwa kweli. Hatuna budi tufike mahali sasa tuweze kupata ufumbuzi wa kudumu kabisa wa migogoro hii baina ya maeneo ya hifadhi, mapori ya akiba, vijiji, maeneo ya wafugjaji na maeneo ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri kitu kimoja, tufanye mpango mahsusi wa kuwekeza kwenye elimu kwa mambo makubwa matatu. Elimu kwa maana ya mafunzo, hamasa na programu shirikishi. Kwanza kwa ajili ya kuimarisha mipaka, wakati wa kuimarishwa lazima tushirikishe wale wananchi vilevile. Tunapofanya wenyewe mwisho wa siku wananchi wanakuja kuona kwamba “aah, hawa walibadilisha mipaka” malalamiko mengi yamekuja maeneo ambayo wanasema mipaka ilikwishapimwa, zoezi la kuja kuimarisha na kuweka zile beacon limechukua muda mrefu. Serikali ilivyokuja kwa maana ya Wizara ilivyokuja walikwenda wenyewe, hawakushirikisha wale wananchi pale kiasi kwamba wananchi wanaona “aaah! hawa watu wametuvizia wakati hatupo wamekuja wameweka mipaka usiku” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi kuna tatizo au shida gani ya ku-involve wananchi wakati wa kwenda kuimarisha mipaka. Kwa nini tusitumie muda mwingi angalau kuwaunganisha na kuweza kufanya nao kazi pamoja ili kuepuka lawama hizi na migogoro huko mbele. Nisisitize sana wakati wa mazoezi ya kuimarisha mipaka, kwanza tusichukue muda mrefu, lakini wakati wa zoezi hili tushirikishe sana wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine katika mapato tunayoyapata kwenye hifadhi zetu. Tuwekeze kidogo kwenye elimu ya uhifadhi kwa wananchi. Wananchi nao waweze kuelewa kwa nini na wao wawe sehemu ya kulinda yale mazingira ambayo tumeamua kuyahifadhi, nao wanufaike kwa namna moja au nyingine. Tukiwekeza kwenye elimu hiyo, vurumai itapungua, watu watazuia mifugo, wataacha shughuli za kibinadamu kwenda kwenye maeneo yaliyohifadhiwa itakuwa ni win win situation. Tumeweka kidogo na wao wanakaa kule wanajua kabisa kuna umuhimu, leo nimepata labda kisima cha maji pia, wakati mwingine wamekuja watu wametupa mafunzo hapa kama wanakijiji, keshokutwa tumepata madawati, tumejengewa madarasa. Tujitoe kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mtu hapa mmoja alisema ukitaka kula ni lazima uliwe, lazima utoe hela ili uweze kupata manufaa. Naomba nisisitize sana kwenye elimu ya uhifadhi kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuwekeze kwenye elimu ya utii wa sheria bila shuruti kwa wananchi na kwa wale Askari wetu maana tumekuwa na kesi nyingi sana. Mara ya mwisho niliongea hapa kuhusiana na Wizara hii, kesi kubwa sana ya mauaji. Sasa tufanye utaratibu ambapo yule Askari anaji-feel responsible kumkamata mtu, amhoji vizuri, afuate taratibu mpaka yule mtu amtie kwenye mkono wa sheria, siyo anajichukulia sheria mkononi. Wananchi nao pia waweze kuelewa kwamba ninapokutana na labda wanyama wameingia huku kwetu sio naua tu au sio nafanyaje. Tutii sheria bila shuruti, bila kuingia kule, bila ya kwenda kwenye hifadhi kufanya shughuli za kibinadamu, itatusaidia sana kupunguza hii migogoro. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la migogoro limekuwa ni kero kubwa ambayo bila ya kuiwekezea hivi hatutaweza kuimaliza kwa muda mfupi. Mheshimiwa Waziri, pia tufanye uwekezaji kwenye kutoa elimu ya ku co-exist. Wale watu wanaoshughulika na uhifadhi na wananchi waweze kuona umuhimu wa ku co-exist wao pamoja. Kila mmoja ni muhimu kwa mwenzio, siyo mmoja amuone, imefika wakati wanyama wanaonekana ni muhimu kuliko wanadamu, hatuwezi kwenda namna hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitoa ule mfano wa kijana aliyeuawa kwa ajili ya sukari guru, haiwezekani hata kama ameua mnyama gani, hebu tuone namna gani tunaweza tukaona kila mmoja kwa nafasi yake tunaweza tuka co-exist. Siku moja moja mwisho wa siku wakafikia wakaoana kati ya wahifadhi na wananchi kawaida wakawa wanakaa wanashirikiana kwa kila namna. Katika ufumbuzi ninaouona mkubwa wa hii migogoro, tuwekeze kwenye kutoa elimu katika nyanja aina hizo tatu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namba mbili nataka nizungumzie kwenye suala la utangazaji. Utangazaji wa vivutio vyetu, kwa kweli hatujawekeza vya kutosha. Wamezungumza Wabunge waliotangulia, huko tunaona wenzetu takwimu za watalii zinazidi lakini siyo bure, watu wame-invest kama kuna sera, kama kuna utaratibu wa kushirikiana na sekta binafsi kushirikiana na hizi wakala na taasisi mbalimbali tuweze kuongeza uwekezaji kwenye kutangaza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie Mheshimiwa Waziri, ile michoro ya mapangoni ambayo iko kwenye historia sisi toka tuko wadogo tunaisoma, tunayo michoro zaidi ya
450. Wangapi wanaijua hapa, wala haiko mbali, iko hapa Kondoa tu kwetu. Wangapi wanaijua ile michoro, hatujai- promote, tumeiacha na ofisi ziko pale lakini hata rasilimali watu sijui kama inazingatiwa, kama watumishi wapo, yaani pako dull kwelikweli ni kana kwamba vivutio hivi havipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji kuwekeza, tunahitaji kujitoa ili tuweze kuvutia watalii wengi na tutaongeza kipato kupitia njia ya namna hii. Ni lazima tu- invest ili wale watalii tunaotaka waje, watakuja kwa wingi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri napenda sana nizungumzie kuhusiana na uwekezaji hususan kwenye maeneo ambayo yapo, tunayajua kihistoria lakini tumeyaacha kama malikale zimelala, tumeandika kidogo sana kwenye hotuba yetu hapa. Inaonekana hata dhamira ya dhati ya ku-promote vivutio hivi ni kama haipo. Sasa huku kwenye kutenga fedha ndiyo kabisa, kuko kutupu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri kwa safari yetu tunayotaka kuboresha utalii, nafikiri kwa utaratibu huu tutakuwa tumekwama sana. Namwomba pale anapokuja kwenye majumuisho nategemea na naomba nisikie anatueleza nini kuhusiana na investment kwenye promotion ya vivutio vya utalii, malikale na mengineyo. Pia atueleze vizuri mipango na programu zilizopo na uwekezaji ambao upo au anapanga kuuweka kwenye utatuzi wa migogoro hasa kwa njia hizi shirikishi. Kadri nilivyokuwa nimeelezea kwa maana ya kutoa elimu ya uhifadhi, kwa maana ya kutoa elimu ya kutii Sheria bila shuruti na kutokujichukulia sheria mkononi na pia kwa maana ya elimu ya co-existence, pamoja na programu shirikishi za kuwa- engage wananchi ili nao wajione kwamba ni sehemu ya uhifadhi na wasije kuwa wao ndiyo tatizo au changamoto zinazosababisha hii migogoro, badala yake wao wawe chanzo cha ufumbuzi na suluhisho katika kupata majibu ya migogoro hii ambayo imekuwa kero kubwa na inaleta madhara, inapoteza nguvukazi, watu wanakufa kila leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kondoa kuna mapori mawili, yote ni vurumai, karibu mara zote tunasikia huko watu wamekufa watano, mara amekufa mtu mmoja. Kila unapokuta pori la akiba au maeneo ya hifadhi ni vifo. Mheshimiwa Waziri tutavimaliza lini hivi, kweli kila siku tunazungumzia jambo moja tu la migogoro baina ya maeneo ya hifadhi? Tumeshindwa kabisa kupata ufumbuzi wa kudumu wa mambo haya? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya kweli ipo katika hili? Mheshimiwa Waziri na...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naunga mkono hoja.

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimwa Mwenyekiti, awali ya yote nichukue fursa hii adhimu kabisa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia uzima na afya leo tumekutana hivi wote katika dhima nzuri kabisa ya kujadili Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa 2018/2019. Pia nitoe pongezi kwa Serikali ya Awamu ya Tano ikiwa chini ya Mheshimiwa Dokta John Pombe Magufuli pamoja na timu yake nzima kwa kazi nzuri ambayo wanaendelea kufanya na sisi tukiendelea kuisimamia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, halikadhalika, nitoe pongezi kwa wenzetu walioaminiwa, walioaminiwa wapya lakini na wale ambao wameendelea kuaminiwa na Rais kwa uteuzi wa kushika nafasi za Mawaziri, Naibu wa Mawaziri lakini pia nawapongeza na wale ambao walibaki, tutaendelea kusimamia Serikali huku kwenye ukumbi huu wa Bunge.

Mheshimiwa Spika, nitoe pongezi kwa Wizara ya Mipango na Fedha kwa Mapendekezo haya mazuri chini ya Mheshimiwa Dokta Mpango kama jina lako lilivyo lakini pamoja na pacha wangu Mheshimiwa Dokta Ashatu na Katibu Mkuu na timu nzima ya Wizara ya Fedha na Mipango. (Makofi)

Mheshimwa Mwenyekiti, kimsingi hotuba yenu ya Mapendekezo ya Mpango imekaa vizuri tatizo kubwa ambalo tumekuwa nalo ni kwenye utekelezaji. Kama ambavyo wameainisha kwenye hotuba yao wamechukua maoni kutoka kwenye jamii, taasisi za Kiserikali, Kamati ya Bunge ya Bajeti ambayo hiyo unaipata kwenye hotuba yake ukurasa wa nne paragraph ya saba lakini pia wameileta kwenye Bunge ili waweze kuchukua maoni.

Mheshimiwa Spika, tunawaomba sana kwamba uchukuaji wa maoni haya uwe wa ukweli. Tumeanza juzi tunakwenda kumaliza Jumatatu siku tano nzima Waheshimiwa Wabunge hawa kila mmoja kwa nafasi yake anatoa pale alipoona panafaa. Tukitoka kapa kwa maana ya uchukuaji wa haya maoni, kwa kweli tutakuwa tunapoteza maana nzima ya sisi kukaa na kujadili Mapendekezo haya ili yaje kuboresha mpango na bajeti siku za mbele. Tunawasihi sana wachukue maoni yetu haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nataka niseme kwamba pamoja na uzuri wa Mapendekezo na tunatarajia Mpango utakuwa mzuri baada ya kuchukua input zetu, ni lazima tuweke mikakati madhubuti na inayotekelezeka ya kuhakikisha utekelezaji wa Mpango huu unakwenda. Tutachukua maoni lakini utekelezaji unakwendaje? Tuna mikakati gani inayotekelezeka ya kuhakikisha Mpango huu wa Maendeleo na Bajeti ya 2018/2019 utakuwa dhahiri, utakuwa realized kwa Taifa na utakuwa realized kwenye uhalisia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije kwenye maoni na ushauri wangu katika kuboresha Mapendekezo haya ambayo mmeyaleta mbele ya Bunge hili. Nia ni nzuri na nia ni kwamba tunakwenda kujenga, kuimarisha na kuendelea kukuza uchumi imara, uchumi endelevu, uchumi ambao tunataka tufike mahali tunasema sustainable growing economy na sisi tumepanga mpaka 2025 tuwe katika kiwango cha uchumi wa kati, ni lazima tuone tunakwendaje vizuri ili tufike huko kwenye hazima yetu.

Mheshimiwa Spika,Dhana ambayo tunakwenda nayo ni ya uchumi wa viwanda. Uchumi wa viwanda maana yake tunahitaji kufanya mapinduzi ya viwanda. Tumeyasikia mapinduzi ya viwanda yamefanyika kwenye Mataifa mengine mbalimbali na hatimaye kweli wamefikia uchumi wa viwanda.

Mheshimwa Mwenyekiti, nia na madhumuni hapa ni kwenda kuongeza uzalishaji. Tumesikia wenzetu wamechangia kwamba mahali ambapo tunategemea sisi kukusanya au kupata mapato ya nchi ni kwenye vyanzo labda vilevile, tunahangaika na tax base ambayo kila siku inakuwa ni ileile, unakamua ng’ombe ambaye tayari labda hajaweza kuzalisha zaidi. Sisi dhamira yetu lazima twende kuzalisha zaidi tupate surplus ambayo mwisho wa siku tunaweza kuweka akiba na nyingine ikatusaidia kuongeza kipato kwa kuuza huduma na bidhaa ndani na nje ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesema na kwenye maandiko haya yote yako vizuri kabisa kwamba tunataka kuweka viwanda ambavyo vitalishwa na rasilimali zinazozalishwa Tanzania. Ni sahihi kabisa, tungeweza kuzungumzia kila eneo na products zao wanazozalisha. Mfano kule kwetu Kondoa tunaweza kuweka kiwanda cha edible oils, kuna karanga, ufuta, alizeti kwa wingi kabisa na hii inaweza ikawa Kondoa lakini vilevile ikakamata Ukanda mzima wa Kati. Dodoma yote inazalisha alizeti vizuri kabisa, Singida majirani zetu wanazalisha alizeti, karanga, ufuta, tunapiga kiwanda kimoja cha kiwango kikubwa ambacho ni double refinery.

Inaweza kulisha na kuongeza tija katika ukanda wote wa edible oils. Lengo kama ambavyo mmeliainisha ikiwa ni kuongeza thamani ya bidhaa zinazozalishwa kwenye maeneo yetu na kukuza mnyororo wa thamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwakumbushe na kuzidi kushauri Wizara katika kuboresha haya Mapendekezo. Mapinduzi ya viwanda yatafanikiwa pale tutakapofanikisha mapinduzi ya kilimo. Tunazungumzia malighafi zilizoko pale lakini bila ya mapinduzi ya kilimo haya mapinduzi ya viwanda yatakuwa ni hadithi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeendelea kuweka jihada katika kuhakikisha tunapata mbegu bora, kuhakikisha tunaweza kupeleka pembejeo kwa wakati, mikakati mingi sana ipo, lakini jambo moja kubwa ambalo nataka kuliwekea uzito leo hapa ni suala la kilimo cha umwagiliaji. Hiki kilimo cha mvua hata upeleke mbegu za namna gani, uwe na pembejeo za namna gani bila ku-engage kwenye large scale farming ambayo itakuwa inategemea irrigation tutakwama tu kupata mapinduzi ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nisisitize sana eneo kubwa ambalo lazima tuliwekee mipango ni hili la irrigation ambalo tumekuwa tukilizungumzia mara nyingi. Wizara ya Maji na Umwagiaji ukiangalia bajeti yake kwenye upande wa irrigation ni ndogo sana. Hapa tunahitaji tuwekeze heavily kwenye infrastructure za irrigation, iwe kupitia mabwawa, kupita kwenye utaratibu wa matone (drip irrigation) au na mifumo mingine ya mito, mifereji na kadhalika lakini bila irrigation large scale farming itashindikana.

Mheshimiwa Spika, tunapozungumzia large scale farming ndiyo italeta mapinduzi ya kilimo, tunazungumzia wakulima wakubwa lakini pamoja na hawa wadogo, wakitumia kilimo cha umwagiliaji tija yake ni kubwa, una uhakika wa yield. Tusipofanya hivyo tutakuwa tunakabiliwa na changamoto ya tabia nchi kila mara na hatimaye uhakika na usalama wa chakula na uzalishaji usiwepo, hata hivyo viwanda ambavyo tunataka malighafi tunazolima wenyewe ziende kulisha kwenye viwanda ikashindikana.

Mheshimiwa Spika, nawaomba sana Mheshimiwa Dokta Mpango na pacha wangu Dkt. Ashatu, na nawasihi sana ushauri huu wa kui-nvest heavily kwenye scheme na infrastructure ya irrigation ni jambo ambalo tukiweka hapo mkazo litatuondoa na tutafikia kwenye mapinduzi ya viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine kwenye kufanikiwa mapinduzi ya viwanda nimezungumzia mapinduzi ya kilimo lakini vilevile tujiwekeze na tujikite kwenye kuzalisha wataalam wa ufundi. Amezungumza ndugu yangu hapa Mheshimiwa Maige, siku za nyuma nimewahi kuzungumza tulivyokuwa tunajadili Mpango 2016/2017 na 2017/2018 kwenye Bunge hilihili kuhusiana na polytechnics, kuzalisha wataalam kwa ajili ya kwenda kuviendesha na kuviendeleza viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunazungumzia uchumi wa viwanda, wako wapi hao wataalam ambao wanakwenda kuwa wabunifu na kuvikuza viwanda hivyo kama kila mmoja anataka afanye kazi ya white colour. Vyuo vilivyokuwepo awali, Chuo cha Ardhi amezungumzia mzee hapa Dar Technical vile ambavyo products zilizokuwa zikitoka kule zinatoka kwenda kufanya kazi ya ufundi. Managers ni wengine, watakuwepo mainjinia watapata degree na kadhalika lakini wanaokwenda kuendesha viwanda vile tunawazalishia wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwekeze kwenye polytechnics, vyuo vikuu vya ufundi, vya ufundi wa kati ma- artisan hawa, technicians wa FTC lakini pia na vyuo vikuu vya ufundi ambavyo wenzetu maarufu wanaviita polytechnics ili viweze kwenda kuzalisha wataalam watakavyovikuza na kuviendeleza viwanda hivyo. Haya ambayo nimeyaongea ya polytechnics lakini ya irrigation nadhani tukiyazingatia yatatusaidia sana kwenda kuleta tija kwenye Mpango huu ambao tutakuja kuujadili mwakani. Jambo lingine na la mwisho, huko mwanzo nimezungumzia kuongeza uzalishaji mwisho wa siku ina-ripple effect kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine na la mwisho nataka kuzungumzia kuhusu na dhana nzima ya uwezeshaji wananchi kiuchumi. Sitagusa milioni 50 za kwenye Ilani kwa sababu nadhani huko siko tunakotaka kwenda, lakini basi tujikite kwenye kuwezesha infrastructure muhimu, kutengeneza mazingira mazuri ya micro-financing ambapo wale wananchi wa kawaida wataweza kupata angalau nguvu kidogo ya uchumi liquidity ikaongezeka kupitia sijui SACCOS, kuimarisha mifumo ya VICOBA, micro-finances nyingine, kujenga na kuimarisha mazingira haya ili angalau mwananchi wa kawaida aweze kunufaika na mikopo au upatikanaji wa mitaji yenye masharti na gharama nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mazingira ya kawaida, yule mfanyabiashara pale Kondoa kijijini au mjini au mkulima ni ngumu sana ku-access financing kupitia financial institutions tulizonazo. Ni lazima tutengeneze miundombinu mizuri kabisa, tujenge mazingira ya kuwafikia hawa watu wa chini wakope kidogo kidogo ili waweze kujiinua kiuchumi wao wenyewe mmoja mmoja na hatimaye jamii nzima ya maeneo halisia na hatimaye Taifa kwa ujumla. Tutakuwa tumepiga uchumi jumla na tumepiga micro- economy, mwisho wa siku Taifa linakwenda mbele na kwa kazi kubwa zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, kwanza kabisa pamoja na kazi kubwa, kazi nzuri inayofanywa na Waziri pamoja na timu yake yote, lakini napenda kusema kwamba, naona bajeti hii haija-reflect ile safari tunayotaka kwenda, haija-reflect mapinduzi ya elimu ambayo tunataka kwenda.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumezungumzia tunakwenda kwenye uchumi wa kati, uchumi wa kati tukasema tunahitaji mapinduzi ya viwanda, lakini kunahitajika mapinduzi mengi tu, mojawapo ni mapinduzi ya elimu, tuweze kweli kweli kupata transformational change. Sasa kama safari ni hatua, tuone kabisa hatua inayokwenda, kama nakwenda tuseme Kondoa, basi naona nimetokea Dodoma naona nimefika Aneti, nione nimefika Chemba, mwisho wa siku nifike Kelema na hatimaye nifike Kondoa. lakini kwa bajeti hii na malengo yetu ya muda mrefu ambayo tunataka kuyafikia, kwa kweli Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yako, nafikiri kuna kazi kubwa sana ya kufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri inabidi tuamue sasa kuwekeza kwenye elimu kwa kiwango kikubwa kweli kweli. Huu uwekezaji tulioufanya sasa hivi katika bajeti, naona hautatufikisha pale tunapotaka kwenda, hiyo nilipenda nianze kuzungumzia kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niende kwenye hoja mahususi katika bajeti nzima ya elimu. Kwanza napenda kuongelea wanafunzi. Suala la mfumo, muundo na kanuni za ufundishaji na kwa maana ya kutoa mitaala naona haimjengi mwanafunzi wa Kitanzania katika kwenda kuingia umahiri katika soko la ushindani kwa maana ya competence. Sisi hatuko wenyewe, dunia siku hizi ni kijiji na inatakiwa wanafunzi wetu wanapotoka huko nje waweze kushindana katika soko duniani, waweze kujiamini, wajenge uelewa badala ya kujenga kukariri na kufaulu mitihani, wajenge uwezo wa kujieleza, matokeo yake wanapofika huko mbele wana uwezo mkubwa wa kupambana na ku-survive, wanasema survival for the fittest. Sasa kama elimu yetu haitujengi kwenda kuwa fit duniani itatukwamisha sana, tutakuta tu tunaendelea ku-import knowledge kutoka kwa wenzetu, lakini wa kwetu sisi hawatoki kwenda nje nao wakafanye vitu vyao huko. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri ni wakati muafaka kabisa Wizara ikae na kujiuliza, hivi tatizo liko wapi? Tujiulize sana na tufanye tafiti za kutosha sana, tunao Wataalam, tujiulize tatizo liko wapi? Kwa nini output, kwa nini products za wanafunzi wetu siyo mahiri? Kwa nini hatuko competent sana on average? Wapo watu wazuri, wanatokea wazuri, lakini on average elimu yetu hairidhishi. Kwa hiyo katika hili, ningesisitiza sana uwekezaji investment ifanywe kubwa sana kwenye RND kuweza kuhakikisha tunainua ubora wa elimu yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, nataka nizungumzie kwa upande wa Walimu. Hapa hasa ndiyo kwenye kasheshe. Ifike mahali sasa ile dhana iliyopo kwamba Ualimu ni kazi ambayo ni dhaifu, mtu huwezi kujivunia, hatuwezi kuikimbilia, tubadilike kabisa. Ifike mahali Ualimu uheshimike, mtu unapoamua kwenda kusomea Ualimu una-proud kwamba mimi ni Mwalimu. Mwalimu awe na uhakika wa ajira, lakini awe na uhakika wanasema maslahi mazuri, very well paid, waweze kuwa motivated vizuri sana, waweze kuwa na incentives kubwa, lakini mazingira pia ya kazi lazima yawe tofauti sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaowachukua hawa kuwa Walimu, siyo ile ya sasa hivi labda tunakwenda mpaka division tofauti tofauti, Walimu wanatakiwa kuwa top scores, top performance ndiyo wawe Walimu na mwisho wa siku na kama maslahi yako mazuri na wanalipwa vizuri, kila mtu atakuwa ana pride kusema akawe Mwalimu na watu wengi watakimbilia kwenda kufundisha. Ualimu uwe ni kazi ya bright students. Tukifanya hivyo kweli tutakuwa tumefanya transformational change, mwisho wa siku Walimu wetu kama ni wazuri, obviously products zao zitakuwa ni nzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine, napenda kuchangia kwenye suala zima la polytechnic, Vyuo vya Ufundi. Hapo zamani tulikuwa na Vyuo vya Ufundi Dar Tech, chuo ambacho nilisoma mimi, Chuo cha Ardhi kilikuwa kinatoa Wataalam, Mafundi, lakini sasa hivi vile vyuo vyote tumevigeuza vinapanda hadhi vinakuwa Vyuo Vikuu. Sasa kama kila mtu atavaa tai, kila mtu anataka kuwa meneja, kila mtu anataka kuwa na degree, nani atakwenda site kusimamia kazi? Nani ataingia maabara kuhakikisha kazi za kitaalam zinafanywa vizuri?
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka kuwa na Vyuo Vikuu vingi, ni sawa tuwe na Vyuo Vikuu vingi, lakini polytechnic ni muhimu sana kuhakikisha kazi za kitaalam zinafanywa. Rai yangu kwa Serikali, hebu tuache hili suala la degree na tai, lakini tuwe na FTC‟s za kutosha. Arusha tech ziimarishwe, ziwe bora zaidi, ziwe equipped, ziwe resourced ili watu wetu wanaotoka kule wakienda kazini, wawe na uwezo hasa wa kusimamia details za kitaalam. Turudishe polytechniques zetu. Kwa hiyo, pamoja na jitihada kubwa ya kuongeza idadi ya Vyuo Vikuu na kutoa degree, hebu na suala la polytechnique tuliangalie sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, la tano na la mwisho, napenda kuongelea kuhusiana na wataalam, watu wanao-qualify, wamekwishasoma degree zao au kama ni FTC, wametoka wameingia kwenye soko la ajira, tutengeneze utaratibu mmoja wa kuwekeza kwa hawa watu ili wakapate exposure programs, wajifunze, waige utaalam, waige experience. Nchi za wenzetu ambazo kwa baadhi ya taaluma zinafanya vizuri. Nitatolea mfano suala la Madaktari, hata Walimu au Wahandisi, lakini nitatolea mfano suala la Madaktari; watu wawe wanatoka tunawapa Mikataba specific wameshamaliza shule, lakini anapelekwa mtu zaidi ya miaka mitano mpaka hata kumi, si tunawekeza kwa ajili ya generation zijazo? Tunawekeza kwa ajili ya kupata transformation ya elimu yetu kwa ujumla wake, watu waje hapa wana uwezo mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi tu tumeshuhudia Tanzania zimefanyika operations za kwanza kubwa za moyo. Watu wanafunua moyo ule ndani wanazibua mirija iliyoziba, lakini waliokuja kufanya ile operation wanatoka India. Kawaida kuna ushirikiano na Australia, Saudi Arabia na Marekani, basi tuwapeleke Madaktari wetu nao wakasome, tuweke mikataba mahususi, watu wakasome, tukishamaliza kuwekeza kwenye elimu hapa, wakimaliza wanakwenda nje, wakirudi they bring back wealth of experience ambayo itatusaidia sana kubadilisha mfumo mzima wa uwezo na knowledge hapa nchini. Kwa hiyo, nasisitiza sana, katika jambo kubwa tunalotakiwa kulifanya kama Serikali ni kuwekeza kwenye elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumerudia na tunaendelea kuimba kwamba tunakwenda kwenye uchumi wa kati, lakini huu uchumi wa kati bila mapinduzi na transformation ya sekta nyingine hizi kama elimu, pia ni mtihani mkubwa tunaweza tusifike. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Elimu kama pioneer katika Serikali kwenye suala zima la elimu, hebu tuangalie maeneo yote haya, kuanzia mitaala, kuufanya Ualimu uwe ni kazi ya kujivunia, shule zetu za polytechnique pamoja na hawa wataalam tuweze…

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa niweze kuchangia kwenye hotuba ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa pamoja na Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nawapongeza Mawaziri wote wawili kwa hotuba zao nzuri sana, zimesheheni mambo mengi, hata hivyo, pamoja na hotuba nzuri napenda kutoa maboresho kwenye maeneo machache yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la kwanza ni suala zima la utawala bora na uwajibikaji. Taarifa na hotuba inaeleza vizuri baadhi ya watumishi ambao wamekuwa wakifanya makosa na wakivuruga wanawajibishwa kwa kufuata taratibu za kinidhamu na hatimaye pia za kijinai. Wapo ambao pia wamepelekwa Mahakamani, wapo ambao wamefukuzwa kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na taarifa hii inaonesha tuko vizuri sana katika utaratibu huu, lakini kiuhalisia nikitoa mfano wa Halmashauri kama ya kwangu ya Kondoa Mjini wamekuwepo watu wengi sana ambao wamekuwa wakivuruga hasa Maafisa Ardhi, hata Mkurugenzi aliyekuwepo. Kinachotokea badala ya kuwajibishwa kutokana na makosa yaliyofanyika, wanahamishwa. Sasa unapomhamisha huyu mtu unahamisha tatizo siyo? Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Mawaziri, badala ya kufanya suala la kuwa-reshuffle hawa watumishi wanaovurunda, taratibu za kuwawajibisha kinidhamu na hatimaye kijinai zifanyike kwa wote.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa na Maafisa Ardhi wengi sana wamekuwa wakituvuruga, anatoka Kondoa anapelekwa Rombo, anatoka Rombo anapelekwa sijui eneo lingine, wanaenda kuhamisha matatizo tu hayo. Pia wapo ambao kesi zimepelekwa Mahakamani, lakini wanatoka pale wanakwenda Makao Makuu TAMISEMI, wanasema sijui wamekaa benchi au vipi, sasa utaratibu huu haujengi nidhamu ya kuwafanya hawa watumishi wengine wawe waadilifu na wafanye kazi zao kadri ya miongozo na taratibu zinavyowataka.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri huu utaratibu wa kutumbua majipu, huku kwenye Halmashauri zetu uende vizuri kabisa, watu kweli watumbuliwe maeneo yote, siyo mtu anavuruga halafu anahamishwa, hii haitatusaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hilo, ipo hali ya baadhi ya watumishi kutokuwajibika, mfano, sasa hivi Halmashauri yangu ni zao la Halmashauri iliyokuwepo, wale wote ambao walionekana kwamba they are non- performance, wanahamishwa wanapelekwa kwenye Halmashauri mpya, kweli hakuna utaratibu tunaoweza kujiwekea kupima performance ili hawa ambao mwisho wa siku hawa-perform wawajibishwe? Nafikiri hilo ni suala muhimu sana la kuliangalia Waheshimiwa Mawaziri, ili watumishi wetu wanaokuwa Serikalini na kwenye hizi Halmashauri waweze kuwa wawajibikaji wote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala zima la elimu, kwenye elimu naongelea suala la Walimu, nikianza na upungufu wa Walimu. Upungufu wa Walimu ni tatizo kubwa, najua utaratibu unafanywa ili Walimu wengine watoke vyuoni waweze kuingia kwenye mashule kufundisha, lakini wanapotoka upungufu ni mkubwa sana hapa katikati, shule zinateseka, wanafunzi wanaumia, wanashindwa kupata masomo yao kadri inavyostahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, pale kwangu kwenye elimu ya Sekondari tuna upungufu wa Walimu zaidi ya 80. Jibu dogo tu la Kondoa Mjini upungufu zaidi ya Walimu 80, kwenye shule ya msingi kuna upungufu wa Walimu zaidi ya 60. Mpaka waje kutimia na mahitaji najua ni ya nchi nzima, utakuwa mtihani mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nishauri kitu kimoja, wapo wale Walimu ambao in the interim kama mpango wa muda mfupi tu wakati tunasubiri uzalishaji wa wale Walimu wengine wapya. Wapo Walimu ambao walistaafu, haiwezekani tukawapa mikataba ya muda mfupi, wa- fill hii gap in the interim wakati tunasubiri hao wengine wanakuja, itusaidie kidogo kupunguza makali ya upungufu wa Walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda niliweke hilo kama changamoto na mapendekezo ya kuboresha hawa Walimu ambao tunazungumzia wanadai mafao, wanadai malimbikizo ya mishahara, hebu tuwatumie wale wanaweza wakatusaidia kwa muda mfupi.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiwa hapo, katika suala la Walimu, najua hili litamgusa zaidi Waziri wa Elimu Profesa Ndalichako, pia nataka niliweke hapa kwenu, Walimu na nilizungumza kwamba mkazo wangu upo sana kwenye elimu. Walimu watokane na best performance, siyo Walimu watokane na yale madaraja ya mwisho ndiyo wanaenda kuwa Walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kufanya ni kuboresha maslahi yao pia kuwa-remunerate vizuri, kuwa- compensate vizuri na kwa kuwa ajira yao itakuwa inaonekana ina uhakika zaidi na iko vizuri wanafunzi wengi watataka kwenda kufanya hii kazi ya Ualimu. Tutakuwa tumewa-motivate, tumewa-inspire, matokeo yake kazi ya Ualimu itaonekana ni kazi yenye heshima, siyo kazi tu ya wale wanaofeli. Wanalipwa vizuri, wanatengenezewa mazingira mazuri ya kazi, matokeo yake inawa-motivate na kuwa-inspire watoto wetu wote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Profesa Ndalichako katika marekebisho yetu tunayoyafanya, moja ya vitu vya kuhakikisha vinarekebishwa ni kuona kwamba Walimu wanatokana na best performance.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiwa hapo elimu, naomba sana hili najua linaenda zaidi kwa Profesa Ndalichako Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi tena, tubadilishe huu utaratibu wa madaraja, tunasema ufaulu ni asilimia kubwa, tunaamini kwamba mpaka division IV ni ufaulu!
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tusijidanganye, tunajipa picha kwamba watu wetu wanafaulu, kumbe tunakwenda kupeleka katika soko la ajira watu ambao hawako competent. Turudishe ufaulu division one mpaka three, ndiyo iwe maximum ya ufaulu na watu watajitahidi, watu watapambana, na Walimu watapambana kuhakikisha kwamba vijana wetu wanafaulu katika madaraja hayo.
Mheshimiwa Nabu Spika, tunajiridhisha tu kwamba ufaulu mwaka huu asilimia 69 kumbe kuna division four kule ndani, division four ni ufaulu? Haiwezekani tunataka tutoe Taifa la watu ambao wanajiweza. Taifa la watu ambao wako competent, tukitoka hapa tunashindanishwa na watu wa Mataifa mengine, tuweze ku-survive. Naomba sana hilo tulizingatie na kama inawezekana , tuanze kulibadilisha sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu nataka kuliongelea kidogo ni maji. Katika Jimbo langu la Kondoa kuna upungufu mkubwa sana na tatizo kubwa sana la maji Mjini pamoja na Vijijini. Pamoja na upungufu wa maji huu na miradi inayokwenda michache, bado usimamiaji wa miradi ambayo ilikwenda kule mwanzo siyo mzuri kiasi kwamba miradi inakufa, visima vinashindwa kuendeshwa vizuri, wale watu hawapati elimu ya kutosha, Kamati za Maji hazijielewi, matokeo yake hata ile miradi michache iliyokwenda inakufa na tatizo linazidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuomba Waziri wa TAMISEMI suala hili tuliangalie, tuhakikishe maelekezo mazuri yanakwenda kwenye Halmashauri zetu, watu wasimamiwe wapate maelekezo mazuri, Kamati ziundwe, ziwe zinakuwa monitored, matokeo yake miradi iweze ku-survive. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, najua bajeti yenyewe ni ndogo, hiyo miradi michache itakayokwenda kule lazima tuilee na iwe endelevu, bila usimamizi mzuri, tunawaelewa watu wetu vijijini, itakuwa changamoto kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimependa nizungumze hayo matatu tu katika hotuba hizi mbili. Nakushukuru sana na naunga mkono hoja.

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii. Kwanza kabisa nipende kuchukua fursa hii kuzipongeza Kamati zote mbili kwa taarifa na mapendekezo yao na pia nianze kwa kusema naunga maoni na mapendekezo yote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, basi nichukue fursa kuzungumzia machache. Kwa upande wa Kamati ya Maliasili napenda kwanza kushauri kutolewe na zitengwe fedha kwa ajili ya kutoa elimu ili watu wafahamu umuhimu na faida za uhifadhi kati ya mipaka ya mapori ya akiba, mapori tengefu na maeneo ya makazi. Watu wamekuwa hawaelewi umuhimu wa hili jambo; ndiyo maana unakuta watu wanavamia, mifugo mara nyingine inakwenda inaingia ndani ya hifadhi, kunakuwa na vurumai sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kufuatilia hakuna fedha hata kidogo zinazotengwa za kutoa elimu kupitia Wizara na hizi Mamlaka za Uhifadhi; sasa wanawezaje kuendesha hiyo kampeni ya kuelimisha wananchi? Matokeo yake wanakwenda na nguvu tu, wakati mwingi wanatumia nguvu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimejaribu kwenye Jimbo langu Kondoa kufanya zoezi hili na likafanikiwa kwa kiwango kikubwa, watu wameanza kuelewa kutii sheria bila shuruti, kwa maana ya kutokuingia kule ndani, lakini pia taasisi hizi zinazohusika na uhifadhi ni lazima ziwe na fungu la kufanya zoezi hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale kwetu kuna pori la akiba la Swagaswaga na lipo Mkungunero na watu lazima waelewe namna ya ku-co-exist, tusipo co-exist na wananchi wakajua kuna faida gani ya haya mapori, wakaziona na wakanufaika nayo ina maana itakuwa vurumai inaendelea tu. Kwa hiyo, nataka kusisitiza Wizara lazima kutengwe fungu hawa watu waweze kuelimishwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika hiyo hiyo namba mbili, askari wa wanyamapori; kweli wana jukumu la uhifadhi, lakini ndugu zetu hawa kwa kuwa wamekuwa wanahifadhi wanyamapori wamekuwa na wenyewe kama wanyama, wanaua hovyo. Wakati mwingine hata hakuna sababu ya kutumia nguvu kubwa hiyo, lakini wanakutana na mtu labda tena wakati mwingine; mimi nina kesi mwezi wa 12 hapa, alikuwa ameonekana kijana ana pikipiki amebeba kifurushi cha sukari guru, kinavuja vuja hivi wao wakadhani ni nyama ya pori labda ni swala. Walimfuatilia wao wana gari lao land cruiser yule kijana ana pikipiki wamekwenda kumuua kwenye kijiji wala si kwenye hifadhi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kijana mmoja, hana silaha hana lolote, anaendesha pikipiki yake of course na yeye alikimbia maana wale askari wa hifadhi wakionekana watu wanapata hofu; akawa anakimbia na pikipiki yake wale jamaa wamemkimbiza wamefika hatua kijana asiye na silaha anapigwa risasi sita. Sasa hata kama angekuwa ni Thomson Gazelle ameuwawa pale si furushi la sukari guru kweli hukumu yake ilistahili kupigwa risasi zote zile? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara na mamlaka, hizi taasisi hebu tuwafundishe hawa askari wetu wawe na ubinadamu kidogo. Halafu baada ya kumuua wamemchukua wakamkimbizia porini ili waje kudai kwamba mtu huyu ameuwawa ndani ya hifadhi; mtu kauwawa kijijini. Wakachukua na furushi lake la sukari guru na pikipiki wakaingia nayo ndani kwenda kupotosha ushahidi. Kumekuwa na taratibu hiyo mara nyingi sana kwa sababu askari kwa askari taarifa ikiripotiwa wanalindana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuona dalili zile, bahati nzuri nilifika kwenye tukio mapema sana, nimshukuru sana Mheshimiwa Mwigulu nilizungumza naye nikamwambia nina wasiwasi hapa kuna dalili za kupotosha ushahidi, watu wameingiza maiti ndani. Wewe umeua mtu si unamuacha kwenye crime scene? Tena ni askari una ujuzi, unaondoa kwenye crime scene unapeleka porini ili ukamsingizie. Basi akaweka jitihada ule utaratibu ukafuatwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, walikuwa ni askari saba mpaka sasa hivi wamekamatwa askari watatu tu wako ndani including wawili waliopiga risasi; mmoja ali-shoot risasi mbili na mwingine risasi nne. Imeenda kupasua mapafu na moyo mpaka kijana wa watu akapoteza maisha namna hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu tuwafundishe askari wetu; Mheshimiwa Waziri na viongozi wote huko; hawa jamaa wawe na ubinadamu. Kuwa wahifadhi wa wanyampori haina maana nao ni wanyama. Nataka kupendekeza, tukio lile lilitangazwa na likawa kubwa sana kwenye vyombo vya habari, basi hata hawa maaskari watakapohukumiwa nalo lijulikane ili wananchi wapate imani na Serikali yao kwa sababu wanaona watu wanawekwa ndani kwa muda tu halafu wanapotea. Mtu aliyeua namna hii stahili yake ni hukumu ya kunyongwa mpaka kufa, umeua makusudi, si bahati mbaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nisisitize sana Wizara iliangalie hili kwa kina sana na limetokea, Mkungunero; miaka ya nyuma wakati wa tokomeza tuliona haya yamekuwa kwa wingi sana. Kwa hiyo, nisisitize Wizara ilitilie mkazo na kuwafunda wale askari, si wanyama wale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nataka kuzungumzia uimarishwaji wa ile mipaka kati ya mapori tengefu, mapori ya akiba, hifadhi na maeneo ya wananchi. Ndugu zangu siku vile vikosi kazi vinapokwenda kuweka ile mipaka ishirikishe wananchi. Kwa sababu unaweza ukasema usishirikishe wananchi baadaye migogoro inaendelea miaka nenda rudi. Wawe sehemu ya uwekaji wa mipaka ile. Idara za ardhi katika Halmashauri zetu zishiriki, wanakwenda na GPS wanaona mipaka na wanajiridhisha hii ndio iliyoandikwa na ndio tunayoijua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu vinginevyo malalamiko yanaendelea, aaa, mpaka ulikuwa hapa, sasa wameusogeza mbele. Sasa tutaendekeza malalamiko ya namna hii kwa muda gani? Kuna ugumu gani Wizara na hizi mamlaka za hifadhi kuwashirikisha wananchi na idara za Halmashauri zikaenda na vifaa; na document zao wanazo basi utaratibu unakuwa clear. Hilo nalisisitiza sana ili tuweze kupunguza hii migogoro isyokwisha kati ya hifadhi na maeneo ya makazi na kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kidogo kwa ufupi sana kuhusu kilimo; jamani tutazungumza sana kilimo na uchumi wa viwanda. Hiki kilimo kama hatutakiwekea bajeti kubwa kabisa ya kutosha kwenye upande wa umwagiliaji tutakuwa tunapiga story tu.

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa hii ya kuchangia kwenye hotuba ya bajeti ya TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora. Kwanza kabisa nawapongeza kwa kuwasilisha hotuba nzuri na kuwasilisha mpango wa bajeti mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia siyo vibaya na ni muhimu tukaweza kutoa maboresho pale ambapo panaonekana panahitaji kuboreshwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitaanza na eneo la kujenga uwezo kwa maana ya mafunzo. Nimemsikia kaka yangu Mheshimiwa Simbachawene namna alivyoliweka; tunaelewa mlipotoka, tunaelewa maana yake, lakini nataka niseme, mafunzo ya kujenga uwezo ni jambo muhimu sana. Hata ukiwa umesoma namna gani, una Ph.D, umetoka umewiva, una experience nzuri kabisa kwenye eneo lako la kazi, lakini kujifunza ni dhana endelevu. Utajifunza mpaka siku ya kwenda kaburini.
Sasa tunaposema kwenye baadhi ya maeneo kwamba tumechagua watu au tumeteua watu ambao wamekwishawiva, nafikiri pale kidogo tunahitaji tulitafakari upya. Nashauri, jambo hili la wenzetu Wazungu, wanasema “learning is a continuous process.” Mpaka siku ya mwisho
utaendelea kujifunza tu, hautafika mahali ukasema wewe umekamilisha, unajua kila kitu, haiwezekani. Ni lazima tuendelee kujifunza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, napendekeza kwamba Wizara, kwa maana ya Serikali, bajeti ya kujenga uwezo iendelee kuwepo na izingatiwe sana. Taifa ambalo halijifunzi, hili litakuwa ni Taifa la namna gani? Kweli mtu anasema nimeshamaliza kujua! Haiwezekani. Ndiyo maana wakati mwingine tunakutana na changamoto za makosa madogo madogo ambayo yangeweza kuepukika kupitia capacity building.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nisisitize sana, nimeona kuna bajeti kidogo kwa wale ambao wengine wanawaita maarufu kama wateule kwa maana DED, DC, DAS na Wakuu wa Idara wengine, lakini nataka niseme pia hii capacity building isiishie kwa hawa wateule peke yake,
hata sisi Wabunge, lakini wale Madiwani, Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji ambao toka wameingia, sehemu kubwa mfano kwa Wenyeviti hakuna chochote walichojifunza. Matokeo yake unajikuta wako tu kule hawajui hata wanakwenda vipi pamoja na kwamba waliomba zile nafasi
wakiamini wana uwezo na zile nafasi lakini kwa kweli wanahitaji kufanyiwa mafunzo ya kujenga uwezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nisisitize kwamba katika bajeti, hili ni jambo la msingi sana na kama tunakwenda na falsafa ya kwamba hakuna tena; kulikuwa na ile dhana ya Semina Elekezi. Naishauri tu Serikali yetu, naamini Serikali yetu ni sikivu, jambo hili tutakuwa tunakwenda kidogo kwa kimakosa. Tujaribu kulitazama upya, tutenge bajeti kwa ajili ya shughuli hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo nitapenda nichangie, kumejitokeza kule kwenye Halmashauri zetu ukinzani kati ya maelekezo kutoka Serikali Kuu na vipaumbele kutoka kwa wananchi. Sisi tunaokwenda kwa wananchi tunakutana na changamoto. Tunataka kuzitatua
changamoto kutokana na vipaumbele ambavyo tumefikuta kwa wananchi, lakini mkikaa kwenye vikao vile pale Halmashauri wakati mwingine tayari kuna maelekezo, safari hii kipaumbele ni moja, mbili, tatu, huku kwingine hapana.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua hata hii Serikali tumeiweka kwa ajili ya kuhudumia wale wananchi. Tunapoweka one size fits all kwamba katika ngazi ya Serikali, sawa. Kulikuwa na jambo ambalo limeonekana safari hii tufanye operesheni hii twende namna hiyo, lakini vile vipaumbele ambavyo tunakwenda kuviibua kwa wananchi, tusiviache. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri, hebu labda kuwe na maelekezo kwamba panapotokea mambo ya vipaumbele na maelekezo kabisa ya labda miongozo, maana yake hii miongozo ndiyo Watendaji wengi wanafanya nayo kazi hiyo, ili kusiwe na migongano sana katika hilo. Mwenyekiti, Mbunge na Madiwani wengine wanapambana na vipaumbele vilivyoibuliwa huko na wananchi; lakini Watendaji wa Halmashauri, wanapambana na melekezo. Mwisho wa siku hatutafika. Naomba sana Mheshimiwa Waziri hilo tuliangalie vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu, napenda kuongelea kuhusiana na suala zima la huduma kwa wazee kwa maana ya kule hospitali. Niko sasa kwenye mpango wa afya kwa maana ya hospitali. Sera ipo vizuri na mipango ni mizuri. Nataka niwaambie, utekelezaji wake kule hospitali hebu tengenezeni mkakati au mechanisms za kuhakikisha unatekelezwa kadri mnavyopanga, kwa sababu utekelezaji kule haupo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwaambie kama kwangu kule Hospitali ya Mji wa Kondoa, ukiuliza habari ya Dirisha la Wazee, halipo. Ukiwauliza, sera hii ipo vipi? Wengine hawaelewi. Kwa hiyo, hebu tuhakikishe kuna mikakati mahususi ya kuona hii mipango tunayoiweka katika ngazi ya kitaifa inatekelezwa mpaka kule chini. Tuwe na mechanisms za kusimamia utekelezaji ambao utakuwa makini.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la vitambulisho; hao wazee wa kuanzia miaka 60 wapate vitambulisho ili waweze kuhudumiwa. Siyo tena kila wakati wakija wapite kwa Mtendaji wa Kata waandikiwe barua. Hiyo haijakaa sawa! Ni usumbufu ambao unapunguza ufanisi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiwa hapo hapo kwenye suala la afya, napenda niongelee suala la dawa. Malalamiko juu ya dawa ni mengi kweli kweli. Hapa tunasikia kwamba hela zimepelekwa nyingi kwa ajili ya dawa, lakini kule unakuta hakuna dawa. Tatizo liko wapi hapa? Nataka
nishauri Serikali tufanye utaratibu wa kuweka procurement experts kule kwenye Hospitali zetu ili waweze kujua supply chain ya dawa inakwenda vipi? Inapofika wakati mtu anasema matumizi yake ya dawa ni shilingi milioni 15 kwa wiki, huku analetewa hela tofauti, au ana-order kila baada ya quarter moja wakati dawa zinakatika katikati hapo ina maana hatuna mpango mzuri wa dawa. Tuweke taratibu
ambao kutakuwa na minimum reorder level, ikifika kiasi fulani wana order tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, bila kuwa na experts wa procurement kule kwenye hospitali zetu, tutaendelea kusumbuka na haya malalamiko yatakuwepo na hela zipo, zimepelekwa. Ukiangalia kwenye upande hela, zipo dawa hakuna. Naomba na hilo nalo liangaliwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine kwenye upande huo huo wa afya, kuna baadhi ya hospitali zinakutana na changamoto kubwa sana kama ile hospitali ya Mji, Kondoa. Inahudumia Halmashauri tatu Kondoa Mji, Kondoa Wilaya, Chemba, lakini pia na sasa hivi barabara kubwa ya lami
imepita na dharura zinaongezeka, lakini fungu kubwa la bajeti linakwenda kwa ajili ya Hospitali ya Mji; haitatosha. Hebu tuangalie kama pale tunaweza kuboresha kufikiria mpaka hao wengine watakapojenga hospitali zao za wilaya, lakini kwa sasa hivi wote wanahudumiwa kupitia Hospitali ya Mji, Kondoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, niguse kidogo tu kwenye upande wa TASAF. Napongeza mpango huu, ni mzuri na malengo yake yana tija sana, lakini nataka niwaambie, utelezaji wake unahitaji mkakati wa kuusimamia ili ukidhi malengo. Kwa sasa hivi kuna upungufu mkubwa na kunatokea malalamiko mengi…(Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naunga mkono hoja.

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa, kwanza kabisa niipongeze Waziri, Wizara na timu yake nzima kwa uwasilishaji mzuri. Napenda kusema machache kwa maana ya kuboresha na kurekebisha pale ambapo panahitaji marekebisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nataka niongelee kuhusiana na hospitali yetu ya Kondoa ambayo kabla ya kugawanywa Halmashauri kidogo tulikuwa tunakwenda vizuri, lakini sasa hivi kutokana na utaratibu bajeti yake imebaki kuwa kutokana na idadi ya watu wanaotokana na Halmashauri ya Mji Kondoa ni kidogo sana. Inapigiwa bajeti kwa ajili ya watu 68,000 wakati inahudumia watu 250,000 wa Kondoa Vijijini, inahudumia watu wa Chemba karibu 250,000, kwa hiyo jumla inahudumia watu karibu 600,000 ingawa inatengewa bajeti kwa ajili ya watu 68,000. Kwa hiyo uwezekano wa kutoa huduma kwa ufanisi haupo kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nakuomba sana jambo hili pamoja na kwamba tunaangalia kigezo cha population, hebu tuende mbele zaidi, hospitali hii inahudumia na akina nani wengine?

Mheshimiwa Mwenyekiti, babaraba ya kutoka Dodoma - Kondoa kwenda Babati inaeelekea mwisho kumalizika kwa kiwango cha lami. Sasa hivi tena ndiyo tatizo linaongezeka kutakuwa na wasafiri pale watakaohitaji huduma, wako hata jirani zetu wa Wilaya zingine za pembezoni nao wanapata huduma pale. Ninakuomba suala hili la kuangalia kigezo hiki cha idadi ya watu peke yake kwa hospitali kama ya Kondoa najua na wengine wapo wanakumbana na matatizo kama haya, hebu tuliangalie tuweze kutoa huduma hii vizuri kuliko ilivyo sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiwa hapo hapo niongelee kidogo kuhusiana na upungufu wa Miundombinu na vifaa muhimu. Kwanza kabisa ni ambulance, pongezi kwa kazi ambayo tayari imeshafanywa kwa Halmashauri nyingine kupata ambulance, ninakuomba Shemeji yangu Mheshimiwa Waziri Dada Ummy kwamba itakapofika awamu ya pili basi na mimi niwepo katika Halmashauri ambazo zitafuata awamu ya pili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunachangamoto kubwa sana ya mortuary, mortuary ina uwezo wa kuchukua miili minne tu, kwa hospitali kubwa namna ile miili minne ni kitu kidogo sana. Tunahitaji kufanya utaratibu kuongeza facility hii. Hata maabara nayo ni changamoto. Upande wa madaktari pia tuna upungufu, ninakuomba katika utaratibu wako basi na kwenyewe utufanyie mpango.

Pia niongelee suala la dawa, tunazungumza hapa bajeti ipo vizuri fedha zimepelekwa, lakini Mheshimiwa Waziri hoja isiishie tu kwenye fedha zimepelekwa. Fedha zipo lakini ukitafuta mrejesho kwa wananchi huku dawa hazipatikani. Wananchi siyo kwamba wanaangalia fedha zimeingia au wanataka maelezo, wanataka dawa ziwepo, kuna tatizo pale. Kuna tatizo ambalo nahisi kwenye utaratibu wa manunuzi lakini pia na madaktari wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri vitu viwili, namba moja tupate wataalamu ma-expert wa manunuzi ili supply chain ya madawa iweze kwenda vizuri isije ikafika wakati dawa zinakatika hela ziko kwenye hospitali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili labda tutengeneze muundo wa ki-digital ambapo madaktari watakuwa wanajua stock gani ipo ndani kiasi kwamba hata anapo- prescribe dawa zile anajua dawa zilizopo, siyo daktari anatoa dawa kumbe kwenye stock hakuna. Sasa tutengeneze mfumo ambapo kila zinapotumika, zinapopungua anajua kiasi cha dawa zilizopo na ni dawa za aina gani. Hiyo itatusaidia sana kupunguza hii changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule site watu hawaangalii hela, wanaangalia dawa zipatikane. Ninaomba sana Mheshimiwa Waziri jambo hili na mtuambie tu sasa hivi kuna mechanism gani ya kwenu kuhakikisha kweli dawa zinafika na mnapata mrejesho na mfumo gani unawekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu nataka kuzungumza kidogo kuhusiana na…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Sannda.

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizari ya Maji na Umwagiliaji

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza kabisa naipongeza Wizara kwa kazi nzuri ambayo imeendelea kufanya chini ya Waziri wetu na timu yake yote. Kabla sijachangia yale ambayo ningependa kusema, ningependa nitoe maoni yangu ya ujumla kuhusiana na bajeti ya Wizara hii ambayo imewasilishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia, sijui niombe ombi la tofauti kidogo? Tumwombe Chief Whip wetu anipatie dakika 15 kwa sababu, ninayo mengi hapa, ikiwezekana hiyo tukatengua Kanuni, itakuwa nzuri zaidi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza maoni yangu ya jumla, pamoja na mawazo ya wengi ambayo yamekuwepo kuhusiana na kuongeza bajeti hii, mimi nimejaribu kuitafakari. Mwaka 2015/2016, tulikuwa na karibu shilingi bilioni 130 halafu mwaka 2016/2017 tukaruka sana mpaka shilingi bilioni 900 mwaka huu 2017/2018 tumekwenda chini kidogo mpaka shilingi bilioni 600. Wengi wamedhani kwamba ni vizuri tungeweza kuongeza bajeti ifikie angalau lengo la mwaka jana. Mimi nafikiri tulipofanya maoteo ya shilingi bilioni 900 labda hatukuwa sahihi sana ndiyo maana hawa wenzetu wakarudi nyuma wakawa realistic zaidi na kurudi kwenye shilingi bilioni 600. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi wenyewe Wabunge, tumekuwa tukisimama hapa kila siku tunasema bajeti za Serikali zije za uhalisia, leo wamerudi nyuma wamekuwa halisia, tunawaambia warudi kule. Nataka niwaambie, katika shilingi bilioni 900 plus, utekelezaji mpaka Machi ni shilingi milioni 181, kweli! Asilimia 19.8 halafu tunataka turudi kule?Tunawaambia Watanzania ukweli au tunataka kuwafurahisha? Kwa maoni yangu ya jumla, hapa ambapo mmepaweka ni sawa. Hatuna sababu ya kurudi kwenda kuibadilisha bajeti kwa sababu tunataka kuwa wahalisia zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niende kwenye maoni yangu. Kwanza kabisa napenda niungane na wenzangu wengi ambao wamechangia kwamba tupate lile ongezeko la shilingi 50 kwenye Mfuko wa Maji ili tufikie shilingi 100, nina uhakika Mfuko wetu wa Maji utatusaidia sana. Kwa hiyo, nami naungana na wenzangu katika hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niongezee tena zaidi, pamoja na kwamba tunafikiria tuongeze shilingi 50 kwenye mafuta lakini hata kwenye masuala ya vinywaji tunaweza kufanya hivyo. Kuna mmoja wetu hapa alizungumza hili, tukizungumzia vinywaji na bidhaa nyingine ambazo tunatumia kama sigara na kadhalika tukaongeza pale kasenti, tutapata hela ya kwenda kwenye maji, maji mijini na vijijini yatapatikana. Katika kilio kikubwa kuliko vilio vyote, nafikiri hii Wizara ndiyo kilio kikubwa kwetu Wabunge wote. Kwa hiyo, napenda sana niungane na Waheshimiwa Wabunge wengine kuhusu Mfuko wa Maji tuutunishe zaidi uweze kusaidia kwenye suala hili la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye suala zima la umwagiliaji. Nimeangalia ile Tume ya Umwagiliaji ina shilingi bilioni 20 sijui kati ya hiyo shilingi bilioni 600. Tumesema tunataka Tanzania inayoelekea kwenye uchumi wa kati. Uchumi wa kati kwa mpango wetu utakwenda kufanikishwa na uchumi wa viwanda lakini uchumi wa viwanda unataka mapinduzi ya kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi mapinduzi ya kilimo tutayaleta kwa kutegemea mvua au kwa hii shilingi bilioni 20 iliyotengwa, kweli? Mapinduzi ya kilimo yatafanikiwa pale tu tutakapoamua kuwekeza zaidi kwenye kilimo cha umwagiliaji. Viwanda vyetu vitawezeshwa na malighafi za ndani. Malighafi za ndani zinalimwa hapa na ili zilimwe sawasawa ni lazima kilimo kiwe kilimo chenye tija, endelevu, cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti ya umwagiliaji kwa kweli hairidhishi. Hata ile Tume ya Umwagiliaji bajeti iliyotengewa Mheshimiwa Waziri pale hatupo sawa sana. Pale nitapenda sana kutofautiana na ninyi. Niombe anaporudi atuambie, maana shilingi bilioni 20 kwa shilingi bilioni 600 unazungumzia chini ya 10% ya bajeti yote inaenda kwenye infrastructure na mambo mengine yote kuhusiana na umwagiliaji, kweli hapa ndiyo tutapata mapinduzi ya kilimo? Haiwezekani! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumze kidogo pia kuhusiana na suala zima la Jimboni kwangu. Suala la umwagiliaji tuliwahi kuwasilisha maombi muda mrefu kidogo ya Bwawa moja la Umwagiliaji la Mongoroma ambalo lina ekari 3,000. Ekari 3,000 kama tungeweza kuwekeza, hela iliyohitajika ni kama shilingi bilioni mbili, hela iliyohitajika ingeweza kuwekwa pale ni watu takribani 12,000 wangenufaika. Hebu niambie nimultiplication effect ya kiasi gani, ripple effect ya kiasi gani wananchi wangepata kiuchumi kutokana na kilimo cha umwagiliaji chenye uhakika kwa staili hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri na timu yake, naomba hii miradi ya umwagiliaji tuiangalie sana. Mabwawa kama Mongoroma yangeweza kutusaidia kweli. Nimeona kwenye ripoti ziko sehemu nyingi amezungumzia lakini hebu na kule kwetu mkutazame. Mongoroma andiko letu lina zaidi ya miaka mitatu na tija yake ni kubwa, hata uchumi baadaye ungeongezeka sana kule Kondoa, Warangi wangeanza kufurahi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye masuala hayahaya ya mabwawa, Bwawa la Munguri pale Kondoa ambalo kwa kiwango kikubwa lingeweza kusaidia kupunguza upungufu wa maji Kondoa Mjini na maeneo ya pembezoni lina muda mrefu tumelisemea, limeandikiwa, limefuatiliwa lakini inaonekana kama Serikali imekuwa na kigugumizi kuanza kufanya mchakato wa kushughulikia bwawa lile liweze kupata maji ili wananchi wa Kondoa wanufaike. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, basi nashukuru kwa hayo. Nilitamani kumalizia kidogo, lakini naunga mkono hoja, naomba mzingatie hayo niliyoyaeleza.

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Kwanza kabisa napenda kuipongeza Wizara chini ya majemedari wetu wawili hawa wana mama kwa kuwasilisha hotuba nzuri kabisa ya bajeti hii ya Wizara ya Elimu. Lakini na mimi nitumie fursa hii fupi nichangie machache, kimsingi nataka nizungumze kwenye upande wa ufundi, leo nitajikita kwenye ufundi tu sitaongelea kitu kingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona mipango mizuri, utekelezaji ambao umefanywa huko nyuma lakini nataka nizungumzie ufundi kwa maana ya ufundi wa elimu na mafunzo kwa maana ya ufundi stadi na ufundi sanifu. Hapa tunazungumzia vyuo kama vile DIT, Mbeya Technical, Arusha Technical tunazungumzia pia VETA pamoja na FDC vile Vyuo vya Maendeleo. Huko nyuma tulikuwa navyo kwa maana halisi ya ufundi, lakini baadae tumekuja kutoka kila mmoja anataka awe meneja apate degree, avae tai kama Mheshimiwa Sannda wakati tunahitaji mafundi wakae site tuweze kupata weledi na umahiri katika utekelezaji wetu wa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tunajikuta tunaishia kwenye kazi zenye ubora wa viwango vya chini kwa sababu ya upungufu na ukosefu wa mafundi kule site, kila mmoja manager lakini technicians na artisans tatizo limekuwa ni kubwa sana. Ningependa sasa nimeona mipango na maelezo mengi ya huko nyuma na mipango kwa ajili ya 2017/2018, lakini ningependa Mheshimiwa Waziri unaporudi baadaye wakati wa kuhitimisha utueleze kidogo kuhusu sera na dhamira ya dhati ya kuhakikisha utekelezaji wa mipango hii na mikakati unakwenda kutekelezwa kwa maana ya kutenga bajeti nzuri ya utekelezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya dhati itakuwepo tu pale ambapo tutawekeza kwenye vyuo hivi vya ufundi, turudishe polytechnics. Sasa tuna Vyuo vingi Vikuu vinatoa degree mbalimbali katika fani mbalimbali, lakini pia hatuwezi kutoka moja kwa moja kila mmoja akawa meneja, tunataka tujenge kundi kubwa la mafundi ambao watakwenda kuwa weledi katika utekelezaji pia watajijengea stadi za maisha za kuweza kujiajiri badala ya kila mmoja kusubiri kwenda kuajiriwa ofisini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sijaona dhamira hii ya dhati kabisa katika uwekezaji kwenye hili. Tunahitaji tutenge bajeti yake lazima iakisi kwamba hapa tunataka kwenda kutekeleza hii mipango. Tutaongea mambo mazuri kweli kitabu chako kimeeleza vitu vizuri sana, lakini kwenye bajeti haipo hivyo katika nyanja hii. Kwa hiyo, ninakuomba Mheshimiwa Waziri, Wizara kwa ujumla na timu yako yote, suala la fani na mafunzo ya ufundi sanifu na ufundi stadi siyo kitu tena cha kukisubiri au kukifikiria labda tutakifanya baadae. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zama hizi tunataka kwenda kwenye uchumi wa viwanda; uchumi wa viwanda bila hawa watu tutakuwa tuna-import skills nje sana. Tunahitaji watu wetu a ndani ili waweze kwenda na kuiwezesha azma hii ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kujikita kwenye uchumi wa viwanda. Jambo langu kubwa ninaloweza kusisitiza tutenge bajeti na tuwe na dhamira ya dhati kabisa ya kuweka bajeti ya kutosha kwa ajili ya elimu na mafunzo ya ufundi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyuo kama Chuo cha Ardhi kilikuwa chuo mahiri kabisa, watu wanavyokwenda kujifunza kule wanakwenda kujifunza muda mwingi ni mafunzo ya vitendo. Nadharia inakuwepo, lakini sehemu kubwa ya ufundishaji wao na mafunzo yao ni sehemu ya vitendo, kiasi kwamba wanapotoka pale shuleni ni watu ambao wameiva, wamepikwa wakapikika vizuri kabisa wanaweza kuwa tayari, wanasema wengine you hit the ground running ili uendelee na kupambana na maisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninapende tu kusisitiza kurudisha na kuweka focus kwenye vyuo kama Chuo cha Ardhi, Mbeya Technical, Arusha Technical na vingine vya namna hiyo. Pia huku nyuma tulikuwa na shule za ufundi, ukitoka form four unaenda kuanza shule za ufundi kama ilivyokuwa Ifunda. Kwa hiyo, unaanza kupikwa kutoka hapo, ukija kwenda kwenye technical colleges huko ni mtu ambaye tayari mzuri kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zamani tulikuwa tunataniana tunasema wale ma-engineer waliokuwa wanakwenda site wanaajiriwa na makandarasi, waliotoka Chuo Kikuu wamesoma Uhandisi kabisa na wale waliotoka DIT ukiwaweka pamoja huyu wa Chuo Kikuu yeye ni mwepesi, mweupe kabisa. Tunataka watu watakaoenda kufanya kwa vitendo badala ya wengi kuwa na ndiyo tutakapoendeleza vizuri uchumi wetu wa viwanda na kujenga viwanda vingi na vikawa na wataalam wengi wa kuviwezesha vikastahimili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo langu kubwa kwa siku ya leo katika Wizara yako Mheshimiwa Waziri nilipenda sana niongelee suala la ufundi na sitazungumzia kitu kingine chochote. VETA pamoja na FDC najua ndiyo mmevichukua sasa hivi Vyuo vya Maendeleo basi tuwekeze zaidi huko, tuhakikishe kwamba na kwenyewe tunakuhuisha ili tupunguze hii kelele ya kila mmoja akimaliza siku hizi vijana wana hitaji msaada sana wa kutafutiwa ajira basi kila mmoja anakutumia CV yake ukiona ni degree, waite kwenye usaili utaona kasheshe yake, uivaji haujakaa vizuri, lakini tungekuwa na watu ambao ni wataalam anaweza akatoka ameshajifunza stadi za ufundi na stadi za maisha anaingia mwenyewe anajasiria viwanda. Anaanzisha kazi kelele na tatizo kubwa tulilonalo la ajira litakuwa limepatiwa ufumbuzi mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, basi mimi nafikiri ya kwangu ni hayo na nitakuwa nimetunza muda kweli. Ninakushukuru sana na naunga mkono hoja. Ahsante.

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Mimi naomba nimalizie fursa ya kuchangia kwa dakika kumi halafu tutaendelea na huo mfumo wa dakika tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nataka nichukue fursa hii kuipongeza Serikali, nimpongeze pacha wangu hapo Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Ashatu, nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Mpango, lakini pia nimpongeze Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na timu yake nzima ya Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya, hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia labda huenda dakika tano zikawa hazikutosha basi mimi nasema naanza na kuunga mkono hoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuongelea mambo makubwa matatu ama manne, kwanza ni suala lile la shilingi milioni 50 kila kijiji. Unajua ile ni ahadi yetu kwenye Ilani na tumefika kule tumejitangaza vizuri na kila mtu anasubiria. Kwenye bajeti hii hakuna lililoongelewa. Mwaka jana tuliambiwa na pesa kiasi cha shilingi milioni 59 zitatengwa, mwaka huu kimya kabisa. Hebu tusaidieni tunaenda kujibu nini na ni ahadi ambayo tumeitoa, hii nafikiri haijakaa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, itabidi niende haraka ni zile shilingi milioni 40 ambazo kwenye hotuba tumezungumzia kwa maana ya suala zima la road license. Mimi nataka nishauri badala ya kusema road license ambayo itapeleka mzigo mkubwa sana kwa wananchi wengi ambao hawatumii hayo magari, ile shilingi 40 ifanywe tuiweke kwenye mfuko wa maji, wengi wamezungumza hiyo. Isiwe shilingi 40 turudishe iwe shilingi 50 badala ya shilingi 40 iingie kwenye Mfuko wa Maji, kama tutatenga kidogo katika hicho kisehemu ika-cover kwenye suala la road license sawa lakini maji hata ukiweka, najua mafuta yanaongeza gharama kwenye kila kitu lakini kama yanaongeza gharama halafu unaenda kuwapatia wananchi wa kawaida maji umefanya jambo jema kabisa na jambo kubwa. (Makofi)

Nafikiri hiyo itakuwa imeondoa sintofahamu ambayo Wabunge wengi wameongelea hapa. Nawaomba sana tulitafakari hilo na tulielekeze huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, nimeona kwenye hotuba yako viashiria vya uchumi jumla; takwimu zote zinaonesha uchumi upo vizuri na tunakwenda vizuri kadri ya taarifa yako sawa, lakini hali halisi kwa wananchi huku ni kitu tofauti kabisa hasa wananchi wale wenye hali ya chini, wa kati na hata wale wa juu, hali halisi ya mzunguko ile tumezungumzia mzunguko wa fedha kuwepo ni ngumu kweli. Nakuomba Mheshimiwa Waziri hebu tufafanulie, huenda sisi labda upande huu wa masuala ya fedha hatuko vizuri sana lakini tuelezee hivi hii hali unaielezaje. Viashiria vyote viko vizuri sana na tunaelekea vizuri, lakini uhalisia hauko sawa, hauko vizuri ni kilio kila mahali, mfanyabiashara wa kati na chini kila mmoja analia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la nne nimeona tunafanya kuboresha kwenye kuondoa kodi za bidhaa kwenye bidhaa ambazo tunataka walau tu-promote, kwa mfano kazi zetu kama lile la upande wa vyandarua na hasa vyandarua vilivyowekwa viuatilifu vya malaria. Tuna dhamira ya kwenda kuondosha malaria moja kwa moja, vyandarua vinavyotengenezwa ndani vina Kodi ya Ongezeko la Thamani wakati vinavyotoka nje huenda havina, hivi una mfanya vipi huyu mtu aweze ku-compete na wale wa nje? Ili tuweze kuwapa incentive hawa wetu wa ndani wanaoweza kuzalisha hivi waweze kwenda kutusaidia kuondoa malaria basi vyandarua vile vyenye viuatilifu vya kuua wadudu wa malaria basi vifanyiwe utaratibu na vyenyewe viondolewe Kodi ya Ongezeko la Thamani ili waweze kuvizalisha kwa wingi viwanda vyao vikue na viweze kuwa endelevu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nafikiri kwa ufupi ningependa kugusia hayo matano, nakushukuru sana na ninaunga mkono hoja.

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. EDWIN M. SANNDA: Sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa nichukue fursa hii kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri zaidi inayofanywa. Pia nimpongeze Mheshimiwa Profesa Mbarawa, ndugu yangu Mheshimiwa Kwandikwa na mwenzangu Mheshimiwa Nditiye. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nina mambo matatu madogo. La kwanza katika kuunga mkono jitihada za kuhamia makao makuu na kuchochea maendeleo ya maeneo ya makao makuu tumeona hapa kwenye CDD, mji wa makao makuu tunajenga ring roads lakini pia tunahitaji kujenga ring roads kwenye wilaya za pembezoni mfano unazungumzia Katesh - Kondoa, Babati - Kiteto ili na haya maeneo mengine ya pembezoni yaweze kuchochewa maendeleo kwa kupitia miundombinu ya barabara kama za lami. Ring roads zitengenezwe sio tu kwa makao makuu lakini nje ya mji wa makao makuu kwa kiwango cha lami. Hii itatusaidia sana katika kuchochea maendeleo ya maeneo yale ya pembezoni. Hilo ni moja ambalo ningeshauri lifanyiwe mchakato na lenyewe liweze kufanyiwa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni suala la TARURA. Hawa watu wa TARURA na wenyewe ni wataalam kama ambavyo TANROADS walivyo lakini barabara zinazotengenezwa na TARURA zinaonekana kama ziko chini sana ya viwango. Unatengeneza barabara hakuna mitaro wala matoleo matokeo yake mahitaji ya matengenezo yanakuwa ya mara kwa mara.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningeshauri tutengeneze vigezo vya viwango kwamba kila barabara inayotengenezwa iwe na viwango kama ambavyo kwenye TANROADS wanatengeneza ili barabara hizi ziweze kudumu na kukaa muda mrefu whether ni ya light grading au iwe heavy grading lakini vigezo vya mitaro kwa maana ya mifereji na matoleo viweze kuwepo maji yapite barabara zidumu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine hapohapo kwenye TARURA, nadhani ni muhimu kidogo kuongeza bajeti. Ule mgawanyo wa 30 kwa 70 sasa tuufikirie hata kama sio 50 walau 40. Najua kiwango cha barabara zinazotengenezwa na TARURA haziwezi kuhitaji gharama kubwa kama hizi barabara kuu za lami, lakini mtandao wake ni mkubwa sana. Tunahitaji tuwaongezee bajeti na wao waweze kufanya kazi ambayo itakidhi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hapo hapo kwenye TARURA, wazingatie vipindi vya kutengeneza barabara. Tunapoteza hela kwa kutengeneza barabara wakati wa mvua, muda mfupi tu baadae inabidi turudie. Kwa hiyo, labda kile kipindi cha mvua ni kuangalia upungufu uko wapi halafu baada ya mvua ndiyo barabara zinatengenezwa, hasa zile za udongo na za viwango vya changarawe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu, nataka kuongelea kuhusu alama za barabarani kwenye hii barabara yetu ambayo Mheshimiwa Rais anakwenda kuifungua rasmi kesho kutwa tarehe 27 Aprili. Barabara imejengwa vizuri, tunawapongeza sana lakini kuna maeneo mawili ya hatari sana, pale kwenye Daraja la Ausia na kwenye Milima ya Kolo, ni maeneo hatari kwelikweli yanahitaji kuwekwa alama za aina yake, alama kubwa kama kule kwenye madaraja mengine kama Wami ili kupunguza ajali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo yale yamekuwa wakisababisha ajali nyingi sana na kupoteza maisha ya Watanzania wenzetu. Kwa hiyo, tunasisitiza na kusihi, tumeshaongea kwenye Bodi ya Barabara ya Mkoa lakini si vibaya kuliweka tena hapa, ili mradi suala hili lipewe uzito unaostahili na hatimaye alama hizo kubwa kabisa ziwekwe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine na dogo la mwisho, nataka kuzungumzia habari ya mawasiliano kwenye Jimbo la Kondoa Mjini. Mawasiliano yapo karibu maeneo yote lakini yapo maeneo yenye changamoto mawasiliano hayapatikani vizuri hasa katika Kata za Kondoa Mjini, Seria pamoja na Kingale usikivu unakuwa siyo mzuri na drop calls mara nyingi zinatokea. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri na timu yake hebu naomba watuangalizie kule Kondoa nini tatizo hasa ili tuweze kulipatia ufumbuzi tatizo la mawasiliano yasiyosikika vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, kwa kuwa najua sasa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Awali ya yote nichukue fursa kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Daktari John Pombe Joseph Magufuli, lakini pia na timu yake yote ambayo anakwenda nayo. Naona tunakwenda vizuri sana kwenye mwelekeo tunaoutarajia. Pia nimpongeze dada yangu Profesa Ndalichako kwa kazi nzuri ambayo mnakwenda nayo na hotuba nzuri ambayo mmewasilisha hapa, wewe pamoja na Naibu wako Ole Nasha na timu nzima ya Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hotuba nzuri lakini yapo mambo ambayo nadhani kuna kila sababu ya kuyajazia nyama au kuyaboresha hivi. Nitakuwa na mambo machache nikianza na suala zima la walimu.

Mimi nadhani katika kuinua ubora wa elimu katika kuhangaika sana na suala zima la ufaulu wapo wadau kadhaa muhimu sana, wanafunzi, wazazi pia na walimu. Kwenye upande wa walimu, upatikanaji wao na uendelezaji wao nadhani tuangalie vizuri kidogo. Ningependekeza badala ya kuchukua walimu ambao wanakuwa wamefaulu labda daraja la pili au la tatu, ili mtu uwe mwalimu utoke kama top class student ili ukaweze kuwasaidia hawa ambao unajaribu kwenda kuwaelimisha. Kuchukua hawa ambao huku nyuma huku wamefaulu labda wastani na nini inaweza isiwe sawa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua huenda kuna changamoto ambayo tutakumbana nayo hapo mbele lakini napenda sana kusisitiza sana walimu watokane na wanafunzi wanaofaulu juu kabisa kwenye darasa lao. Kama ambavyo kwenye vyuo vikuu wapo wale top student ambao ndio wanaenda kuwa tutorial assistants matokeo yake baadae wanakuwa lecturers huko mbele. Kwa nini nasema hivi tunataka kuboresha elimu tunataka kupata kizazi ambacho kina upeo mkubwa ni lazima upate wenzao wanaowafundisha wawe na upeo mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ikifikia hapo; najua kuna changamoto mojawapo ya labda kuboresha maslahi ya walimu ambayo ni lazima tuanze mahali. Suala la kuboresha mazingira ya kazi za walimu lazima tuanze mahali. Ifike wakati mtu akisema mimi nakwenda kusomea ualimu anajivuna. Kazi na taaluma ya ualimu iwe ni wito wa kujivunia kama ambavyo tunaona wenzetu wanasheria akikaa anaweka kifua mbele anasema mimi I am a learned brother au architect au madaktari, twende namna hiyo. Huko nyuma kazi ya ualimu ilikuwa na heshima sasa hivi mtu anakwenda ili mradi akafanye kazi. Nasisitiza sana wanaokwenda kusomea ualimu tuwe tunawatoa kutoka wale waliofaulu vizuri kabisa, top class student.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo hapo ukishawapata hawa walimu umuhimu wa kuwajengea uwezo endelevu unatakiwa. Si ilimradi nimefaulu nimekuwa mwalimu basi naendelea, na muda unapita education yangu huku kichwani inakuwa wakati mwingine obsolete au una-rust, unaota kama kutu hivi. Kuwe na utaratibu wa kuhakikisha hawa watu kuna mfumo na mpango endelevu wa kuwaendeleza, continuous learning, continuous training hapa na pale katika suala zima la kuwapatia capacity building, hilo ni jambo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nataka niongelee suala zima la shule zisizo za Serikali. Hizi shule zimeonekana zikifanya vizuri sana miaka yote, tangu huko nyuma. Sasa mimi swali langu najiuliza hapa katika kutafakari, kama hawa wenzetu wanafanya vizuri ina maana wana kitu tunaita best practice, kwa nini tusiwatumie wao, tushirikiane nao ili na sisi tuweze kuboresha huu upande wa kwetu? Yaani ni lazima kuna button nzuri wanazozi-press, the right button zinazowapelekea wafaulu. Suala zima la nidhamu, suala zima la kuwa-strict kwenye uendeshaji wao, mahusiano kati ya mwalimu, mwanafunzi na mzazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini inavyoonekana sasa hivi shule za binafsi, zisizo za Serikali ni kama maadui hivi kwa shule za Serikali, jambo ambalo si sawa. Tuwatumie tuwaweke karibu, tuanzishe utaratibu wa kuwashirikisha kwenye kutengeneza sheria zetu kwenye kutengeneza kanuni, miundo, mifumo, haya matamko yanayotoka haya, maelekezo yanayotoka, miongozo inayotoka basi isiwe kana kwamba inakwenda kuwakandamiza, iwe kana kwamba ina-support their existence kwa sababu ndio wanatunyanyua. Ni lazima tushirikiane nao ikiwezekana na kama itaonekana inafaa kiwepo chombo huru ambacho kitaunganisha pande zote ambazo zitakuwa zinatengeneza mwelekeo mzuri wa elimu yetu. Nasisitiza sana hilo la pili kwamba shule zisizo za Serikali ziwe part and parcel ya kuandaa mikakati yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ninataka kuongelea suala la vyuo vya ufundi. Najua tumewekeza sana kwenye upande wa elimu ile tertiary, lakini upande wa elimu ya ufundi nako kidogo inabidi tuongeze uwekezaji. Tuweke mkazo kwenye vyuo hivi kwa sababu kwanza inaendana na dhana kubwa tunayokwenda nayo sasa hivi ya uchumi wa viwanda.

Pili, kuna kundi ambalo huwa halifanikiwi kwenda kwenye elimu ile rasmi ya form five na six na hatimaye chuo kingine basi wapite huku kwenda kutengeneza ajira, kuwa- capture wale vijana ambao wanakuwa hawakupata fursa wasije wakazagaa mtaani…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa hii ya kuchangia Wizara ya Maji, Wizara muhimu kabisa. Kwanza niwapongeze Wizara, Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na wengine wote kwenye Wizara hii kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya na ukiona kama kilio ni kikubwa hapa si kwamba kazi hawafanyi, kazi wanafanya lakini bado uhitaji ni mkubwa kweli kweli, tunawashukuru sana na tunawapongeza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri ambazo anaendelea nazo na usimamizi mkubwa wa hata Wizara hii iliyo chini yake na Wizara nyingine zote, mambo mazuri yanaendelea na nchi naona kabisa kwamba sasa mwelekeo tunaokwenda ni mwelekeo umenyooka, mwanga unaonekana kule mbele kwamba Tanzania mpya sasa inaonekana. Tunampongeza sana Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye Wizara yetu hii ya Maji na mahitaji na changamoto ambazo tunazipata pale Jimbo letu la Kondoa Mjini. Toka nimeanza 2015 au tuzungumzie 2016 mwanzoni mpaka leo tunavyozungumza tulikwishaidhinishiwa fedha kiasi cha bilioni 3.7 na mpaka sasa ambazo zimekwishaingia, zimelipwa kabisa ni bilioni 2.5, hizo tayari kabisa zilishapokelewa, bado kuna kiasi kidogo cha kuwalipa makandarasi. Hapa tumechimba visima 10 ambavyo kati ya hivyo vingine vilikwenda Kata za Mjini ambazo ziko kama tatu, kata ambazo ziko pembezoni ni kama nane hivi na kwenyewe tumesambaza kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katikati Mji kwenye kata tatu, mwanzo tulikuwa tunategema maji ya chemchem ya asili, kulikuwa na tatizo kubwa sana, tukaamini na fedha hizi zote ambazo zimeingia kule kwetu basi tatizo la maji litapungua kweli kweli kwa sababu pale katika kwenye hizi kata tatu tumechimba visima vitano ambavyo vimeenda kuongezea upatikanaji wa maji ambavyo vinaenda ku- compliment ile chemchem. Hata hivyo, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri, leo tunavyozungumza bado kilio ni kikubwa kweli kweli cha tatizo la maji pamoja na kwamba tuna visima vipya vitano na vimesambazwa pale Kwapakacha, Kilimani, Tura, Tumbelo na maji yamesambazwa Wisikwantisi lakini bado huu mzigo wote tulitegemea sasa ule mzigo uliokuwa ukienda chemchem ungepunguza uhitaji basi hii mitaa mingine ibaki ina maji ya kutosha lakini sivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni nini? Inaonekana liko tatizo la wazi kabisa katika utekelezaji wa hii miradi kwamba labda zile design zinazofanywa za usambazaji, idadi ya matenki, urefu wa mabomba , idadi ya vizimba, huenda kuna tatizo wakati wa design, wasanifu wetu wanapofanya kazi inabidi Wizara isimamie kwa karibu sana kuona design hizi ni efficient na zitakuwa effective, sasa hebu fikiria bilioni 2.7 imeingia na bado kilio cha maji kipo kikubwa Mitaa ya Mnarani, Miningani, Ubembeni, Maji ya Shamba ambapo ndio mjini katikati, kilio ni kikubwa kweli kweli. Hapa nimwombe Mheshimiwa Waziri hebu tufanye utaratibu, turudi tufanye kazi na timu labda Mainjinia wa Mkoa lakini na kule halmashauri kwetu tuone tatizo liko wapi? Kwa nini tulishatoa hela nyingi halafu tatizo la maji bado ni kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuongezea, tulikuwa tumeomba pia fedha kiasi cha shilingi bilioni nne kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya maji pale mjini katikati, ilifanywa design nzuri tu sijui sasa kama Wizara na yenyewe imeihakiki ile design, tumepeleka andiko pale Wizarani, mpaka dakika hii niki-compliment yale niliyokuwa nikiongea mwanzo, inawezekana hata haya maji ambayo tayari tumeshakuwa tukiyasambaza kupitia hivi visima vipya na ile chemchem, chanzo cha maji cha chemchem inawezekana yasiweze kukidhi au kusambaa vizuri kama fedha hizi za ukarabati wa miundombinu zisipopatikana. Tunaomba, tutakuwa tumefanya kazi kubwa sana huku nyuma kama tumekula ng’ombe mzima tumebakiza mkia, hela imeshalipwa lakini wananchi hawanywi maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nisisitize kwenye hili kwamba kuna umuhimu mkubwa kupata zile fedha za ukarabati wa miundombinu ya maji. Miundombinu hii ilijengwa mwaka 1972, wakati Mji wetu wa Kondoa una population ambayo ilikuwa labda haizidi watu 20,000, leo hii tuna population ya watu 50,000, haiwezekani ikawa inatosha, lakini pili imeshakuwa chakavu… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Edwin Sannda.

MHE. EDWIN M. SANNDA: … kwa kiwango hiki hela ile tuipate.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii. Nianze kwa kupongeza sana Wizara hii kwa wasilisho wao, nikupongeze Waziri (shemeji yangu), nikupongeze Naibu Waziri (kaka yangu) lakini pia na Makatibu wote Wakuu na watendaji wa Wizara kwa kazi nzuri ambayo tunathibitisha kwamba mnaendelea kuifanya. Pia naunga mkono hoja hii iliyopo mbele yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hospitali ya Mji wa Kondoa imeendelea kukua na kuongeza uhitaji wa huduma kwa maeneo mbalimbali. Hospitali ya Kondoa Mjini inahudumia zaidi ya halmashauri tano, tunazungumzia Vijijini, Chemba, Kiteto mpaka Babati na Katesh wengine wengi wanategemea huduma ya Kondoa Mjini. Mara baada ya barabara yetu kumalizika, uhitaji umekuwa mkubwa kwelikweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wale watu ambao tulikadiria wataudumiwa na hospitali ile takribani 60,000 sasa imekwenda zaidi ya wagonjwa, siku hizi wanawaita wateja, zaidi ya 400,000 au 500,000, sasa tumekuwa na upungufu mkubwa sana kwanza ni suala la ambulance. Nimekuwa nikipigia kelele sana kuhusiana na kupata ambulance. Tumejitahidi tukakarabati iliyokuwa mbovu lakini tunaomba sana tupate ambulance. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya barabara ile ya kutoka Dodoma kwenda Kondoa kumalizika ajali zimeongezeka, uhitaji wa wagonjwa kupatiwa rufaa kwenda Dodoma umekuwa mkubwa lakini hatuna ambulance. Mwaka jana hata Mbunge mwenzetu mmoja alipata ajali pale tulilazimika kuungaunga, unaomba Chemba, Kondoa Vijijini na ile mbovu ya kwetu kuwaleta majeruhi hapa Dodoma. Tunakuomba sana Mheshimiwa Waziri na timu yako angalia Hospitali ya Mji wa Kondoa ipate ambulance. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa uongezekaji wa mahitaji ya huduma hivyo hivyo hatuna X-ray. X-ray yetu imekuwa ni ya muda mrefu ni ya toka 2000, inaharibika mara kwa mara, ni ya zamani kweli kweli, inakaa hata miezi mitatu mpaka sita, sasa inatokea ajali watu inabidi kupata X-ray tu waje mpaka Dodoma. Nakuomba sana Mheshimiwa Waziri tuangalie kwenye hili suala la X-ray kwenye Hospitali ya Mji Kondoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaendelea kuipongeza Serikali yetu kwa ajili ya kutengeneza miundombinu ya barabara. Sasa barabara imekuwa nzuri lakini pia na ajali na watu wanaopoteza maisha wanaongezeka, mochwari yetu ni ndogo na ya zamani sana, kichumba kile ni kidogo hata maeneo ya kuoshea, fridge ni mbovu na imezeeka. Nakuomba sana Mheshimiwa Waziri tuangalie kwenye Hospitali yetu ya Mji Kondoa tuweze kupatiwa mochwari itakayokidhi mahitaji na haja ya huduma za afya pale Kondoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mtanzamo huo huo tena bajeti yetu kwenye basket fund inatuangalia sisi watu wa Kondoa peke yake ilhali tunahudumia watu zaidi ya 400,000 au 500,000. Sasa hivi bajeti yetu kwa mwaka tupo kwenye milioni 32 wakati tukiangalia mahitaji inakwenda kwenye milioni 100 mpaka milioni 120. Hebu na hapo pia mtufikirie tuweze kuwahudumia wagonjwa ambao wanaitegemea Hospitali hii ya Mji Kondoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri yetu wa Mji wa Kondoa imegawanyika katika kanda kama tatu. Kanda ya kwanza ya Kusini, Kanda ya Kati ndiyo Hospitali ya Mji ipo pale na Kanda ya Kaskazini. Tunazo zahanati na tunashukuru Serikali tumepata kituo cha afya kimoja kwenye hii Kanda ya Kusini kwenye Kata moja Kingale. Watu sasa kutoka Ukanda wa Kusini wanakwenda kupunguza uhitaji wa kwenda mjini kwa ajili ya kufuata huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunachoomba tupatiwe walau kituo kingine cha afya kwenye hii Kanda ya Kaskazini katika Kata ya Kolo na jambo ambalo nimeliongea sana kwenye Bunge letu hili Tukufu ili kuwaondolea adha ya kusafiri umbali mrefu wananchi hawa wa kutoka Ukanda huu wa Kaskazini kutafuta huduma za afya kwenye Hospitali ya Kondoa Mji. Tukipata Kituo cha Afya, Kata ya Kolo, matokeo yake tutakuwa tumewasaidia watu wote wa Ukanda huu wa Kaskazini pamoja na Kata za Bolisa na majirani wa Sowera na kadhalika. Tunaomba sana Mheshimiwa Waziri tuweze kupatiwa kituo hiki cha afya ili tusogeze huduma karibu kadiri ya mpango na sera zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru kwanza kabisa nichukue fursa hii kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Jemedari makini kabisa Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kazi nzuri sana ambayo imeendelea kuifanya na ama kwa hakika watanzania tunaona mwanga mbele kule kwamba tunaona tunaenda kuipata tanzania mpya. Na tanzania mpya kweli inawezekana chini ya Dkt. Magufuli.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri na Manaibu wake wote wawili ndugu yangu Mheshimiwa Kwandikwa na na mwenzangu Mheshimiwa Engineer Nditiye nimpongeze katibu Mkuu wa Wizara hii architecture mwenzangu Mwakalinga lakini pamoja na watendaji wote pamoja na wakuu wa taasisi zote zilizopo chini ya Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na pongezi zote hizo kwa kazi inayoendelea naomba nichangie mambo machache kama ifuatavyo:-

Kwanza kabisa nitapenda kuongelea barabara yetu ya kutoka Dodoma kwenda Babati ambayo inapita pale kwangu Kondoa Mjini ni barabara nzuri na ya viwango ambavyo havina shaka wakati mwingine unaweza kuendesha mpaka unaweka ile cruise control sina hakika katika nchi ya Tanzania ama na sehemu nyingine barabara nzuri kama ile unaipata wapi nawapongeza sana kwa viwango vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo karibu kidogo naunafika kondoa mjini lipo daraja moja linaitwa Msangalale. Daraja lile limekaa sehemu ambayo kama inamtego kidogo kuna mlima halafu kuna kona kunamteremko wa hatari sana kumekuwa kukisabisha ajali nyingi, watu wamekufa, watu wengi sana wamepoteza maisha pale na wengine wamepata vilema. Sasa niliwahi kuzungumza siku moja kwenye RCC na ninamshukuru sana Engineer wa Mkoa wa Dodoma Eng.Leonard Chimagu alili-react haraka na wakafanya utaratibu wakweka alama za hatari lakini pia wakweka tuta la kupunguza speed.

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya eneo lilipowekwa lile tuta na eneo ilipowekwa ile alama ni karibu sana na lile daraja matokeo yake bado ajali zimeendelea nakuja mtu huko na spidi yake kwa sababu barabara ipo tamu, anakuja na speed yake anaona alama hii hapa ghafla tuta, na tuta lenyewe bahati mbaya pia halina ubora wa sahihi ukiligonga lile watu wanarukia mtoni. Mara kadhaa malori yamedondoka na mara kadhaa gari ndogo zimedonga na zimesabisha kupoteza maisha kwa wapita njia pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Sasa basi ushauri wangu ni nini, alama zisogeze nyuma na ninaomba sana Wizara ilizingatie na kulifuatilia hili, alama isogezwe nyumba na lile bampu lilekebishwe vile viwango vyake vilivyoweka lisiwe la kustukiza wakati mwingine linaharibu hata gari. Halafu kabla ya bampu huwa kunakuwa wanaita kama rasta hivi zisogee nyuma kidogo takribani viwango ninyi mnavijua na ninaamini suala hili kadri nilivyolieleza mtaweza kulirekebisha kwa upande kama unatoka Dodoma na kwa upande kama unatoka Kondoa sehemu zote mbili alama za hatari ziwekwe mbali ile kona imekaa vibaya sana hilo ni moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili kwa upande wa barabara nataka niongelee barabara inaoyounganisha Kondoa kwenda mpaka Kateshi mmtenga bilioni 50 kwa ajili ya barabara ya Munguri lakini hapa Kondoa Mjini lipo daraja la mto mkondoa si daraja kuna daraja dogo ambalo sio la barabara ya TANROADS maximum ni tani 10 malori makubwa hayawezi kupita ili barabara ile ya TANROADS maroli makubwa yapite yanapita korongoni. Sasa napo pale lazima kuweka daraja kwa sababu kunganisha usafiri kati ya kondoa mpaka Kateshi lile daraja la Mto Mkondoa la lenyewe lazima lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana hilo mlingalie vinginevyo magari yatakuwa yanapita halafu yanakwamia pale kwenye Mto Mkondoa. Ukitaka kupitia hili daraja hili la tani 10 malori makubwa hayawezi kupita halafu inaingia mjini kuna kona dongo sana malori makubwa hajawezi kupita naomba sana hilo liangaliwe hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili Jimbo la Kondoa lipo mjini kabisa lakini bado tunazo kata kama sita hivi suala la masiliano ni changomoto kubwa tunazungumzia Kata ya Kingare. Mheshimiwa Naibu Waziri Engineer Nditiye niliwahi kukugusia hii na orodha nilikupa Kata kingare maeneo ya Kampori na mengineyo tunazungumzia Kata ya Suruke, tunazungumziea Kata ya Seria maeneo ya Hurumbi na Dumu na Chandimo tunazungumzia Kata ya Koro maeneo ya Chora na Hachwi, tunazungumzia Kata ya Borisa, tunazungumzia na Kata ya Kondoa Mjini yenyewe hebu fikiria mjini kwenye kuna maeneo ya Tumbero na Chang’ombe hakuna mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili nakuomba sana Mheshimiwa Naibu Waziri hebu lifanyie kazi pale mjini tujisikie nasi tunaweza kupata huduma muhimu vinginevyo sisi tupo Makao Makuu, kweli tupo Makao Makuu halafu tunakosa mawasiliano jamani. Jiji la Dodoma Makao Makuu ya nchi hebu naomba tusaidie sana kwenye hili nilitamani sana niseme zaidi lakini naona kama dakika zangu umenipa mbili sijui…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's