Parliament of Tanzania

KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YAAGIZA HALMASHAURI KULIPA FEDHA WANAZODAIWA KWA WAKATI

Agizo hilo limetolewa Mkoani Iringa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Aloyce Kwezi wakati kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa Kupanga, Kupima ardhi wa Igumbilo ambao umetekelezwa na Manipsaa ya Iringa kwa kutumia fedha hizo za mkopo walizopewa na Wizara ya Ardhi.

‘‘Kimsingi kazi ya upangaji miji ni jukumu la kila Halmashauri na siyo Wizara hivyo ni lazima mtambue kwamba Wizara iliwasaidia katika kutekeleza majukumu yenu ya msingi kuwakopesha fedha na ndiyo maana mkopo huo haukuwa na riba ili mkapange, mpime na mmlikishe wananchi ardhi kwenye Halmashauri zenu’’ alisema Kwezi.

Kwa upande wake Mhe. Angelina Mabula Naibu Waziri Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, aliishukuru Kamati hiyo ya Bunge na kusema nia ya Serikali kupitia Wizara ni kuona kila kipande cha ardhi nchini kinapimwa na hivyo Wizara iliamua kuziwezesha Halmashauri zenye dhamana ya upangaji miji katika maeneo yao kwa kuzikopesha kiasi cha fedha ili zitumike katika utekelezaji wa kazi hizo za upangaji,upimaji na umilikishaji ardhi na kisha kuzirejesha.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's