Parliament of Tanzania

TANZIA

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Y. Ndugai (Mb), anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge wa Konde (ACT), Mhe. Khatib Said Haji, kilichotokea saa 11:45 alfajiri ya leo tarehe 20 Mei 2021 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

“Nimeshtushwa na nimesikitishwa na kifo cha Mhe. Khatib (Mb). Natoa pole kwa wafiwa wote wakiwemo familia ya marehemu,Waheshimiwa Wabunge, ndugu, jamaa na marafiki. Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki kigumu,” amesema Mhe. Spika

Mazishi ya Marehemu Khatib yatafanyika leo saa 10 alasiri Kisiwani Pemba. Innalillah wainailaih rajiun.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's