United Republic of Tanzania
Parliament of Tanzania
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Y. Ndugai (Mb), anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge wa Konde (ACT), Mhe. Khatib Said Haji, kilichotokea saa 11:45 alfajiri ya leo tarehe 20 Mei 2021 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
“Nimeshtushwa
na nimesikitishwa na kifo cha Mhe. Khatib (Mb). Natoa pole kwa wafiwa wote
wakiwemo familia ya marehemu,Waheshimiwa Wabunge, ndugu, jamaa na marafiki.
Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki kigumu,” amesema Mhe. Spika
Mazishi ya Marehemu Khatib yatafanyika leo saa 10 alasiri Kisiwani Pemba. Innalillah wainailaih rajiun.