Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Primary Questions
Ujenzi wa Barabara ya Kidahwe - Kasulu - Nyakanazi
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Je, ni lini barabara ya Kidahwe – Kasulu – Nyakanazi itakamilika kwa lami?
Pori la Akiba la Kagera Nkanda lililopo Wilaya ya Kasulu lilianzishwa kipindi ambacho Wilaya ya Kasulu ilikuwa na wakazi wachache na kwa sasa idadi ya watu katika Wilaya hiyo imekuwa kubwa na kufanya mahitaji ya ardhi kuwa makubwa, pia hivyo kusababisha mgogoro baina ya wakulima na wafugaji na mamlaka za misitu na wanyaa pori.
Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza migogoro hii na kuwasaidia wananchi?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Mkoa wa Kigoma umekumbwa na wimbi kubwa la wakimbizi wa kutoka Burundi na Congo (DRC), kutokana na wimbi hilo ujambazi umeongezeka sana.
Je, Serikali iko tayari kuongeza ulinzi wa kutosha na vitendea kazi vya kutosha ili mamlaka husika iweze kukabiliana na tatizo hilo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na malalamiko baina ya wakulima na Mamlaka ya Mapori ya Hifadhi ya Misitu, kwa sababu ya kuongezeka kwa watu lakini ardhi haiongezeki, hivyo kufanya ongezeko hili la watu wakose ardhi kwa shughuli zao za kilimo na mambo mengine yahusuyo ardhi:-
Je, ni lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Sheria husika ili kufanya marekebisho katika mipaka ya Hifadhi hizo ili kupata eneo la kilimo kwa wananchi walioongezeka ambao hawana maeneo ya kilimo.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Mkoa wa Kigoma una madini ya chokaa, dhahabu,
platinum na kadhalika:-
Je, Serikali imechukua hatua gani kuendeleza utafutaji na uchimbaji wa madini katika mkoa huo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Wilaya za Kakonko, Buhigwe na Uvinza ni Wilaya mpya ambazo hazina Hospitali za Wilaya.
Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Serikali imekuwa ikitoa ruzuku ya pembejeo kwa njia ya vocha kwa lengo la kuwasaidia wakulima, lakini utaratibu ukiwanufaisha Mawakala wa Mbolea kuliko wakulima ambao ndio walengwa.
Je, Serikali inachukua hatua gani ya kuweza kubadilisha utaratibu huo na kuja na utaratibu mwingine utakaoweza kuwasaidia wakulima?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Zahanati nyingi za Vijiji vya Mkoa wa Kigoma katika wilaya zote zina upungufu mkubwa sana wa watumishi wa afya na baadhi ya zahanati hazina Waganga hivyo huduma zinatolewa na Manesi Wasaidizi tu:-
Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa afya wa kutosha katika maeneo hayo ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya vijijini?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Moja ya jukumu la Serikali ni kuhudumia wafungwa kwa maana ya kukwapatia huduma za msingi kama vile chakula, mavazi na matibabu:-
Je, Serikali inafanya nini ili kuhakikisha huduma hizo za msingi katika Gereza la Kasulu zinapatikana kwani wana hali mbaya sana hasa kimavazi?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Upatikanaji wa maji safi na salama katika Mji wa Kasulu bado ni changamoto kubwa sana, kwani maji yanayotoka kwenye mabomba ni machafu.
Je, ni lini Serikali itatoa pesa kwa ajili ya kununua chujio la maji ili wananchi waweze kupata maji safi na salama?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Mwaka 2017 wakati Mheshimiwa Rais akiwa katika ziara Mkoa wa Kigoma, katika Wilaya ya Kasulu aliwaruhusu wananchi waliokuwa wakilima katika maeneo ya Hifadhi ya Makere (Kagera Nkanda) kwa sharti kwamba wasiongeze maeneo mengine zaidi ya yale waliyokuwa wakilima:-
Je, kwa nini TFS wanapingana na agizo la Mheshimiwa Rais na wanawatesa wananchi kwa kuwapiga na kuwanyan’ganya baiskeli na pikipiki?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Wanawake Mkoani Kigoma wameitikia wito wa kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali kama vile vikundi vya kilimo cha muhogo, kurina na kuchakata asali na VICOBA:-

Je, Halmashauri za Wilaya za Mkoa wa Kigoma zimechangia kiasi gani kwa vikundi hivyo kama sheria inavyotamka?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Maeneo ya mipakani katika Wilaya za Kakonko, Kibondo, Kigoma Vijijini, Buhigwe na Kasulu yanakabiliwa na tatizo la mawasiliano ya simu kutokana na kukosekana kwa minara ya simu:-

Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika maeneo ambayo hayana minara Mkoani Kigoma ili kuondoa tatizo la mawasiliano kwa Wananchi?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Mwezi Novemba, 2018, Waziri wa Maji alifanya ziara Wilayani Kakonko na Kibondo na kukagua miradi ya maji iliyokwisha tumia zaidi ya shilingi bilioni moja lakini haifanyi kazi:-

Je, ni lini miradi hiyo itakamilika?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutafuta soko la uhakika la mazao ya mahindi, maharage na mihogo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Daraja kwenye Mto Malagarasi ili kuunganisha Kata ya Ilagara na Kata ya Sunuka katika Wilaya ya Uvinza?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakipatia Kituo cha Afya cha Muyama Wilayani Buhigwe vifaa vya Ultrasound na X-ray?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni kwa kiasi gani Serikali imewezesha Maafisa Maendeleo ya Jamii ambao wamepewa jukumu kubwa la kuanzisha na kusimamia shughuli za vikundi vya Maendeleo kwenye Halmashauri ili waweze kutimiza majukumu yao ipasavyo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, Serikali imewezesha kwa kiasi gani Maafisa Ushirika kuweza kufanya shughuli zao kwa ufanisi, ikizingatiwa kuwa kumekuwa na msukumo mkubwa sana wa kuanzisha Vyama vya Ushirika?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa vibali ili kuajiri walimu na kuondoa upungufu wa walimu uliopo nchini?
MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?
MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italeta Sheria Bungeni kuruhusu Halmashauri kuzikopesha SACCOS za vijana na wanawake?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Simbo hadi Kalya?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kuzungumza na wenye viwanda vya mbolea ili kuwe na ujazo wa kilo tofauti na 50?

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Muhange Wilayani Kakonko?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, lini Halmashauri ya Mji wa Kasulu itaondokana na matumizi ya maji machafu kutokana na ukosefu wa chujio?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's