Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Juma Selemani Nkamia

Primary Questions
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Je, Serikali itakamilisha lini ukarabati wa Mradi wa Maji wa Ntomoko ili kuwaondolea wananchi adha ya ukosefu wa maji kwenye vijiji vya Sambwa, Kirikima, Churuku, Jangalo, Jinjo, Hamai, Songolo na Madaha?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kununua mashine mpya za CT-Scan kwa ajili ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Wakulima wengi wa Wilaya ya Chemba wamefukuzwa katika mashamba yao Wilayani Kiteto licha ya kufuata taratibu na kudaiwa kuwa eneo hilo ni hifadhi.
Je, Serikali ipo tayari kufuta uamuzi uliotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara wa kuwazuia wakulima hawa ili kuondoa mgogoro huu wa muda mrefu?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Bei ya dawa za binadamu imekuwa ikipanda kila wakati na Serikali imekaa kimya wakati wananchi wake wanaumia:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha chombo maalum cha kudhibiti bei ya dawa za binadamu hapa nchini?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni alipotembelea Wilaya ya Chemba aliahidi kuongeza fedha za ujenzi wa Jengo la Halmashauri mpya ya Wilaya:- Je, katika mwaka huu wa fedha, Serikali imetenga kiasi gani kuendeleza ujenzi huo?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Chemba?
MHE. MOSHI S. KAKOSO (K.n.y. MHE. JUMA S. NKAMIA) aliuliza:-
Wilaya ya Chemba haina hospitali jambo linalowalazimu wananchi wake zaidi ya laki tatu kwenda kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa.
Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha Wilaya hiyo inapata hospitali?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Wilaya ya Chemba haina Kituo cha Polisi; je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Polisi na nyumba za askari?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Je, ni lini barabara ya lami kutoka Handeni – Chemba - Kwamtoro hadi Puma Singida itaanza kujengwa?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Shule za Sekondari za Farkwa na Msakwalo zilizoko Wilayani Chemba zimepandishwa hadhi kuwa za A – level na idadi ya wanafunzi imeongezeka katika shule hizo:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji ya uhakika shule hizo ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutafuta maji badala ya masomo?
MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Chemba?
MHE. JUMA S. NKAMIA ali uliza:-

Je, Serikali imekusanya kiasi gani cha kodi kutoka kwa makocha na wachezaji wa kigeni wanaofanya kazi nchini katika mwaka wa fedha 2017/2018?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

Member of the Parliament

View All MP's