Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Edwin Mgante Sannda

Primary Questions
MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatekeleza Sera ya Elimu Bure kwa kidato cha tano na sita ambalo ndilo kundi pekee lililobaki kugharamiwa na Serikali?
MHE. FELISTER A. BURA (K.n.y. MHE. EDWIN M. SANNDA) aliuliza:-
Mtandao wa miundombinu ya usambazaji wa maji toka chanzo kikuu cha maji ya chemchem katika Jimbo la Kondoa Mjini ni ya zamani na chakavu. Katika ziara yake mwaka jana, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliahidi kutupatia fedha za ukarabati wa miundombinu hiyo:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?
MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-
Wananchi wa Vijiji vya Hurumbi, Dumi na Chandimo Kata ya Serya, Ausia, Mulua na Guluma (Suruke) pamoja na Hachwi, Kutumo na Chora (Kolo) katika Jimbo la Kondoa Mjini, kijiografia wana changamoto kubwa ya huduma muhimu za afya ambapo wanalazimika kufuata huduma hizo katika zahanati za jirani au hospitali ya mjini:-
Je, ni lini Serikali itatupatia Mobile Clinic kutatua changamoto hii?
MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-
Pamoja na kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo watokao Wilaya ya Kondoa, Chemba, Kiteto, Babati na wakati mwingine hata Hanang’, lakini Hospitali ya Mji wa Kondoa haina gari la wagonjwa (Ambulance) na uhitaji wa huduma za dharura na rufaa umeongezeka sana baada ya kukamilika kwa barabra kuu itokayo Dodoma – Babati:-
Je, ni lini Serikali itaipatia gari la wagonjwa hospitali hiyo?
MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-

Halmashauri ya Mji wa Kondoa imepata eneo la iliyokuwa kambi ya ujenzi wa barabara ya Mela – Bonga pale Kolo kwa ajili ya uanzishwaji wa Chuo cha VETA:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza azma hiyo?
MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-

Uwepo wa madini ya chokaa umedhihirika katika Kijiji cha Ausia, Kata ya Suruke, Jimbo la Kondoa Mjini, kwa muda mrefu sasa, katika jitihada za kujaribu kunufaika wananchi wamekuwa wakichimba madini haya kienyeji:-

Je, ni lini Serikali itapeleka Wataalam kufanya utafiti kubaini kiwango cha uwepo na ubora wa madini hayo ya chokaa ili wananchi wa maeneo hayo waanze kunufaika sasa na rasilimali hiyo muhimu?
MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-

Kwa muda mrefu tumepigania kuboreshwa kwa maslahi ya Madiwani ikiwepo posho za vikao na Serikali imekuwa ikisisitiza kuongeza mapato ili halmashauri ziweze kuwalipa Madiwani vizuri kadri ya uwezo, wito ambao umeitikiwa vizuri, mwezi Februari, 2019 tumepokea barua toka TAMISEMI ikielekeza Madiwani walipwe posho za vikao shilingi 40,000 na si vinginevyo.

Je, kwa nini Serikali isiache halmashauri kulipa posho kadri ya uwezo kama ambavyo msisitizo umekuwa toka awali?
MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-

Halmashauri ya Mji wa Kondoa imewasilisha andiko la Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Kijiji cha Mongoroma, Kata ya Serya takribani miaka mitatu sasa, eneo la ekari 3,000 limetengwa kwa ajili ya mradi huo utakaonufaisha takribani wananchi 12,000.

Je, ni lini Serikali italeta fedha hizo ili mradi huo uanze?
MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-

Maboma mengi ya maabara kwenye Shule za Sekondari za Kata nchini hayajakamilika na hata pale yanapokamilika hakuna vifaa vya maabara na tunahitaji sana wanasayansi kuelekea uchumi wa viwanda:-

(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha maabara hizo na lini zitakamilika?

(b) Je, ni lini vifaa vitapelekwa katika maabara zilizokamilika?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's