Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Godbless Jonathan Lema

Primary Questions
MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MHE. GODBLESS J. LEMA) aliuliza:-
Hivi karibuni Mheshimiwa Rais ameamuru Wakuu wa Mikoa kuwakamata na kuwaweka mahabusu vijana watakaokutwa wanacheza pool table na draft mitaani kama ishara ya mizaha katika nguvukazi:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza ajira ili vijana waweze kuajiriwa na kuepuka adhabu hiyo itakayotekelezwa na Wakuu wa Mikoa?
(b) Ni dhahiri kwamba Taifa letu linapita katika adhabu kubwa ya umaskini. Je, Serikali haioni kwamba Taifa linaweza kuingia katika vurugu kati ya vijana wasiokuwa na ajira na Jeshi la Polisi?
MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y MHE. GODBLESS J. LEMA) aliuliza:-
Mahitaji ya tairi za magari katika Mkoa wa Arusha na Tanzania kwa ujumla ni makubwa. Mpango wa Serikali kufufua kiwanda cha tairi cha General Tyre unaonekana kwenda taratibu:-
(a) Je, ni lini Serikali itatambua umuhimu wa kiwanda hicho kuanza uzalishaji mapema;
(b) Wapo baadhi ya waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda hicho bado hawajalipwa mafao tangu kiwanda kifungwe: Je, Serikali ina mpango gani wa kuwahakikisha wafanyakazi hao wanalipwa stahili zao?
MHE. ABDALLAH A. MTOLEA (K.n.y. MHE. GODBLESS J. LEMA) aliuliza:-
Agizo la Mheshimiwa Rais la kufufua viwanda ni muhimu na la msingi kwa maendeleo ya Taifa:-
Je, Serikali haioni mradi wa Kurasini Logistic Centre unakwenda kinyume na fikra za Mheshimiwa Rais kuhusu viwanda?
MHE. JOHN W. HECHE (K.n.y. MHE. GODBLESS J. LEMA)
aliuliza:-
Kukosekana kwa mpango madhubuti wa Mipango Miji pamoja na gharama kubwa za ujenzi zinazosababishwa na kodi kubwa katika vifaa vya ujenzi kumefanya wananchi kujenga kiholela.
• Je, ni kwa nini Serikali isiondoe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vifaa vyote vya iujenzi?
• Shirika la Nyumba la Taifa linajenga nyumba bora za makazi na bashara; je, ni kwa nini Serikali isiondoe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye nyumba za Shirika hilo ili ziwe za bei nafuu?
MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. GODBLESS J. LEMA) aliuliza:-
Barabara ya Mzunguko wa Afrika Mashariki (by pass) inayojengwa katika Jiji la Arusha na viunga vyake inaonekana kusuasua ingawa fedha za ujenzi zimeshapatikana.
Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi walioacha maeneo yao kwa ajili ya mradi huo?
MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. GODBLESS J. LEMA) aliuliza:-
Mishahara ya taasisi za umma hupangwa na Serikali. Utaratibu huo wa Serikali kupanga mishahara ya watumishi wake huathiri pia upangaji na ukadiriaji mishahara katika taasisi binafsi.
Je, Serikali haioni haja ya kuboresha mishahara yake na kuzielekeza taasisi binafsi kulipa mishahara inayoendana na hali ya maisha?
MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y MHE. GODBLESS J. LEMA) aliuliza:-
Mishahara ya Taasisi za Umma hupangwa na Serikali. Utaratibu huo wa Serikali kupanga mishahara ya watumishi wake huathiri pia upangaji na ukadiriaji mishahara katika taasisi binafsi:-
Je, Serikali haioni haja ya kuboresha mishahara yake na kuzielekeza taasisi binafsi kulipa mishahara inayoendana na hali ya maisha?
MHE. GODBLESS J. LEMA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kunufaika na nishati mbadala itokanayo na jua hasa, katika mikoa yenye ukame unaosababishwa na jua kali kwa kutengeneza Solar Village na kuunganisha nishati hiyo kwenye Gridi ya Taifa?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's