Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Primary Questions
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-
Mradi wa umwagiliaji Lupilo umesimama na haujulikani ni lini utaendelea kujengwa:-
Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa mradi huo?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-
Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa ulianzishwa kwa ajili ya kuratibu na kusimamia matibabu kwa watumishi wa Serikali, taasisi na mashirika ya umma nchini:-
(a) Je, hadi sasa ni Taasisi na Mashirika ya umma mangapi yamejiunga na mfuko huo?
(b) Je, ni Taasisi na mashirika ya umma mangapi hayajajiunga na mfuko huo?
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA (K.n.y. MHE. GOODLUCK A. MLINGA) aliuliza:-
Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano aliahidi kuwapatia wananchi wa Kata za Lupiro, Iragua, Milola na Minepa eneo la ardhi oevu ya Bonde la Mto Kilombero kwa ajili ya makazi na kilimo pindi tu atakapoingia madarakani. Je, utekelezaji wa ahadi hiyo imefikia wapi?
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ (K.n.y. MHE. GOODLUCK MLINGA) aliuliza:-
Kumekuwa na ongezeko kubwa la wanyama waharibifu kama vile viboko na tembo kwenye maeneo ya mashamba katika Kata za Ruaha, Chilombola, Ilonga, Ketaketa, Mbuga ya Lukande na Lupilo.
Je, Serikali ina mpango gani kuzuia uharibifu huo wa mazao?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-
Sehemu kubwa ya Jimbo la Ulanga imezungukwa na Hifadhi ya Selous Game Reserve hivyo kufanya wananchi wa Kata za Mbuga, Ilonga, Kataketa na Lukunde kukosa maeneo ya kilimo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo maeneo ya kilimo?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-
Wilaya ya Ulanga ina ongezeko la mifugo; ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe lakini hakuna huduma za mifugo kama vile majosho:-
Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa majosho?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-
Barabara ya kutoka Ifakara mpaka Mahenge Mjini ni muhimu sana kwa usafirishaji wa mazao kama mpunga, mahindi, ufuta, ndizi na maharage. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-

Wilaya ya Ulanga ina Shule za Msingi zaidi ya 50 na Sekondari zaidi ya 17 lakini haina Chuo chochote ambacho Wanafunzi wanaomaliza masomo kwenye shule hizo wanaweza kujiunga:-

Je, Serikali inasema nini juu ya hali hiyo?
Kumekuwa na tatizo kubwa katika jamii yetu la ubakaji wa watoto wadogo chini ya miaka mitano na vikongwe:-

Je, Serikali imeshawahi kufanya utafiti ili kujua chanzo cha tatizo hilo?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-

Nchi yetu imebarikiwa kuwa na Hifadhi nyingi zenye wanyama wengi wa kuvutia lakini mapato yatokanayo na utalii ni kidogo: Je, Serikali ina mikakati gani ya kuongeza mapato ya utalii?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-

Majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Ulanga ni machache, madogo na machakavu hasa yale ya kulaza wagonjwa:-

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo hayo na ujenzi wa majengo mapya?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

Member of the Parliament

View All MP's