Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Primary Questions
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:-
Kwa miaka mingi sasa Tanzania Investment Bank na TADB imekuwepo ila mchango wake katika kupunguza umaskini haufahamiki zaidi hata kwa Waheshimiwa Wabunge. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa Benki za TIB na TADB zinajielekeza kwenye utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM kwa sababu ndiyo mkataba wa mpango kazi wa maendeleo ya nchi yetu?
MHE. INNOCENT S. BILAKWATE (K.n.y MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA) aliuliza:-
Mpango wa NSSF kutoa mkopo kwa bei nafuu kwa Vyama vya Ushirika ili navyo viweze kutoa mikopo kwa bei nafuu kwa wananchi wa Karagwe ulikuwa mzuri lakini umekabiliwa na changamoto na kero kubwa kwa wananchi waliotozwa sh. 280,000/= kama kigezo cha kupata mikopo hiyo, lakini mpaka sasa wananchi hawajapata mikopo hiyo na Serikai haijatoa maelekezo yoyote juu ya hali hiyo:-
Je, ni nini msimamo wa Serikali kuhusiana na jambo hili?
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:-
Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya M. Kikwete aliwaahidi wananchi wa Jimbo la Karagwe kuwa Mradi wa Maji wa Lwakajunju ambao haukujengwa kama ulivyoahidiwa, lakini Mheshimiwa Rais John P. Magufuli naye aliahidi kwamba mradi huo utatekelezwa:-
Je, Serikali imefikia wapi katika utekelezaji wa mradi huo?
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:-
Wilaya ya Karagwe ina walimu ambao bado wanadai malimbikizo ya mishahara, walimu hawa hupandishwa madaraja bila ya kurekebishiwa mishahara yao kitu ambacho kimekuwa ni kero kubwa kwa walimu wa Karagwe na maeneo mengine nchini.
(a) Je, Serikali inawaambia nini walimu hawa na imefikia wapi kutatua kero zao?
(b) Je, Serikali imefikia wapi katika kuhakikisha Teachers Service Commission (TSC) inapata rasilimali watu na fedha ili iweze kutetea maslahi ya walimu nchini?
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:-
Kwa muda mrefu wananchi wa Karagwe wamekuwa wakiahidiwa kujengewa Hospitali ya Wilaya na taratibu zote zimekuwa zikifuatwa kupitia Vikao vya Baraza la Madiwani na RCC lakini maombi haya hutupiliwa mbali na TAMISEMI.
Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa hospitali hii ambayo pia ipo kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais?
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:-
NSSF ilikuwa na mpango wa kutoa mikopo kwa Vyama vya Ushirika ili viweze kukopesha wanachama wake. Kwa upande wa Karagwe wananchi walitozwa michango ya kujiunga na NSSF lakini hawajapata mikopo hiyo.
(a) Je, ni lini NSSF itatoa hiyo mikopo nafuu?
(b) Je, ni kwa nini wananchi wanailalamikia NSSF kwa muda mrefu lakini hakuna majibu yanayotolewa?
MHE. INNOCENT L. BUSHUNGWA aliuliza:-
Wananchi wa Bushagaro wamekuwa wakitengwa na maeneo mengine wakati wa vipindi vya mvua kwa sababu ya ubovu wa barabara ya Nyakahanga-Chamchuzi, na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano wakati wa kampeni za uchaguzi za mwaka 2015 aliahidi ujenzi wa barabara hiyo kwa lami na kuweka kivuko eneo la Chamchuzi:-
(a) Je, ni lini barabara hiyo itatengenezwa na kuwekwa kivuko?
(b) Je, ni lini ahadi ya kujengwa kwa lami kilomita 5 ya kianzio kwa ajili ya kutengeneza eneo korofi la Kajuna Nketo itaanza kama Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano alivyoahidi?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's