| E-mail this to a friend | Printable version |
|
||||||
| Session No | Question Number | To the Ministry of | Sector | Date Asked | ||
|---|---|---|---|---|---|---|
| 8 | 107 | FINANCE AND ECONOMIC AFFAIRS | Finance/Treasury | 29 June 2012 | ||
| Mheshimiwa Spika nashukuru. Kwa kuwa Serikali imechukua zaidi ya miaka mitatu kuweza kujua kama washtakiwa wana kesi ya kujibu ama la, na kwa kuwa utaratibu huu ukiachwa ukiendelea maana yake kesi ya msingi inaweza ikachukua zaidi ya miaka mitatu mpaka minne, na kwa kuwa suala la DECI linahusu maslahi ya Watanzania wengi maskini. Je, Serikali haioni kwamba baada ya kujulikana kama kuna kesi ya kujibu ama la, kuweka muda maalum ambao kesi ya DECI inatakiwa iishe? La pili, mwaka 2009 aliyekuwa Waziri wa Fedha Mheshimiwa Mkulo alikiri kwamba kuna vigogo wa Serikalini wanaohusika na DECI, lakini vile vile kuna fedha za umma ambazo ziliingizwa kwenye DECI kwa malengo ya kuvuna ili kile kiasi cha Serikalini kirudishwe Serikalini. Lakini kwa taarifa ambazo tunazo, kesi iliyopo inayohusika na DECI ni ya wale wachungaji watano. Nilitaka Serikali iniambie kufuatia tamko lile la Mheshimiwa Mkullo, ni vigogo wangapi wa Serikali wameshachukuliwa hatua ambao walihusika na suala hili la DECI kwa mantiki ya kuweka fedha za Umma. |
||||||
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 107 SESSION # 8 | ||||||
|
||||||
| NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala zima la kuwa washutumiwa wana kesi ama hawana hiyo itabidi Mahakama yenyewe iamue na ndipo hatua zinaotakiwa kuendelea za kisheria zitaendelea kufanyika. Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kuiwekea Mahakama kikomo cha kesi hii isikilizwe kwa muda upi naamini hiyo ni juu ya Mahakama yenyewe, sisi kama Serikali hatuwezi kuingilia muhimili huo na kuwashurutisha wafanye hiyo kazi kwa shinikizo letu sisi. Mheshimiwa Spika, kuhusiana na vigogo wangapi waliochukuliwa hatua, naomba nikiri kuwa sina taarifa kuwa kuna vigogo waliohusika. Lakini naamini kutokana na kesi kuwa ipo Mahakamani hata wao watachukuliwa hatua zinazopaswa kufuatana na sheria zinavyosema. |
||||||