| E-mail this to a friend | Printable version |
|
||||||
| Session No | Question Number | To the Ministry of | Sector | Date Asked | ||
|---|---|---|---|---|---|---|
| 8 | 130 | INFORMATION, CULTURE AND SPORTS | Information | 4 July 2012 | ||
| Mheshimiwa Mwenyekiti namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake ya ufanisi, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa pamoja na kuwepo kwa sheria hizi zinazohusu usalama wa chakula, Consumer Protection na usalama kwenye madawa, bado tunaendelea kushuhudia matangazo mengi yanayopotosha Umma na hivyo kuwaondolea haki ya kupata taarifa sahihi watumiaji wa huduma hizi? Je, Serikali haioni sasa kwamba ni vizuri ikaanzisha mfumo ambao utakuwa ni self regulating kwa kuanzisha chombo ambacho kitakuwa ni advertising standard council ambacho katika nchi 71 Ulimwenguni kimeweza kuleta mafanikio makubwa kuondokana na tatizo hili? |
||||||
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 130 SESSION # 8 | ||||||
|
||||||
| NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nilitaka niseme kwamba Serikali inapokea ushauri wake na tutaendelea kuufanyia kazi. Lakini nataka nisistize tu kwamba wamiliki wa vyombo vya habari na magazeti wazingatie sera, sheria na kanuni za uandishi wa habari. Hili ni pamoja pia na kuhakikisha kwamba vyombo hivi vinakuwa na waandishi wenye taaluma na uweledi wa tasnia ya utangazaji. Lakini pia kuhakikisha kwamba wanazingatia maadili na miiko ya utangazaji na uandishi wa Habari. |
||||||