Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Supplementary Questions
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Ahsante Mheshimiwa Naibu Spika. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya barabara hii, lakini hazipelekwi. Mara tatu mfululizo imekuwa ikitenga fedha hazipelekwi; mara ya kwanza shilingi bilioni nne; mara ya pili mwaka 2015/2016 zilitengwa shilingi bilioni 10 hazikwenda.
Je Serikali inaweza kulihakikishia Bunge hili na wananchi wa Mkoa wa Kigoma kuwa fedha zitatengwa sasa na kupelekwa Kigoma ili barabara hii iweze kukamilika? (Makofi)
Swali langu la pili, Kidahwe – Kasulu kuna mkandarasi ambaye yupo pale lakini amesimama kwa sababu hajaweza kulipwa fedha zake. Je, ni lini mkandarasi huyo atalipwa ili aweze kuendelea na kazi ya ujenzi wa barabara hiyo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kwa muda mrefu sana kumekuwepo mgogoro wa wananchi na Serikali kwa maana ya Hifadhi za Serikali na wananchi wamekuwa wakilalamika sana kwa sababu watu wameongezeka lakini ardhi haiongezeki:-
Je, ni lini sasa Serikali italeta sheria Bungeni ili ifanyiwe marekebisho kuweza kumaliza mgogoro baina ya wananchi na Serikali?
Swali la pili, kwa kuwa kuna mgogoro mkubwa na wa muda mrefu katika Hifadhi ya Pori la Kagerankanda na Serikali; na wananchi wamekuwa wakipata shida sana kutokana na shida iliyopo kwa sababu kwa muda mrefu hifadhi haijafanyiwa marekebisho ya kupimwa mipaka:-
Je, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri tutafuatana kuja Kasulu kwa ajili ya kumaliza suala la Mipaka katika Wilaya ya Kasulu katika eneo la Kagerankanda?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika nakushukuru. Naitwa Genzabuke.
Mheshimiwa Spika, ukosefu wa viwanda katika Mkoa wa Tabora ni sawa na ukosefu wa viwanda katika Mkoa wa Kigoma. Kwa muda mrefu sana Mkoa wa Kigoma umekuwa kama uko kisiwani kwa maana ya ukosefu wa miundombinu ya barabara za lami na umeme. Hata hivyo, kwa juhudi zinazofanywa na Serikali inayoongozwa na Chama cha Mapinduzi, mkoa ule umeanza kufunguka na siyo muda mrefu utafunguka kabisa. Je, Waziri yuko tayari sasa kuwahamasisha wawekezaji kuja kuweka viwanda katika Mkoa wa Kigoma?
kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa ukosefu wa vifaa tiba katika Wilaya ya Chamwino ni sawasawa kabisa na ukosefu vifaa tiba uliopo katika Wilaya ya Kasulu. Wilaya ya Kasulu haina ultra sound, lakini mpaka sasa hivi ninavyoongea Wilaya ya Kasulu haina vifaa-tiba vya kupimia sukari (test strips), na hili linasababisha wagonjwa kuweza kupoteza maisha kwa sababu wanapopima vipimo kinakosekana kipimo cha sukari wakati mwingine wanaweza kupoteza maisha kwa sababu wanapima…
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo. Sasa ni lini Serikali itahakikisha inapeleka ultra sound Kasulu lakini sambamba na vifaa vya kupimia sukari? Ahsante
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni muda ni muda mrefu sana mgogoro wa Kagera Nkanda umekuwa ukiongelewa humu Bungeni lakini maka sasa hakuna ufumbuzi ambao umeshapatikana. Na kwa kuwa watu wanaongezeka lakini ardhi haiongezeki, ni lini Serikali italeta sheria Bungeni ili ifanyiwe marekebisho kusudi mipaka iweze kusogezwa wananchi wapate maeneo ya kulima?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma unapakana na nchi za Burundi na DRC, na kwa kuwa eneo kubwa la mpaka halina ulinzi, hali inayopelekea wahalifu kupita na kupitisha silaha nzito kuingia Tanzania, wahalifu hao kwa kushirikiana na raia wasiokuwa waaminifu hufanya ujambazi na unyang‟anyi.
Je, Serikali iko tayari kufanya utafiti wa kukagua mpaka upya na kubaini maeneo yasiyokuwa na ulinzi ili kuweza kuweka ulinzi maeneo yasiokuwa na ulinzi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kwa kuwa mara nyingi vituo vya polisi hukabiliwa na ukosefu wa mafuta, hivyo kuwafanya polisi kushindwa kufanya kazi yao kikamilifu. Je, Serikali iko tayari kuongeza bajeti ya vituo vya polisi, hasa Mkoa wa Kigoma ili polisi waweze kukabiliana na majambazi hao?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa wananchi wa Kasulu wengi wao kwa kutokujua mipaka inaishia wapi; wamekuwa wakilima mpakani mwa pori la Kagera Nkani na kwa sasa mazao yao yako tayari wanahitaji kuvuna.
Je, Serikali iko tayari kumuagiza Mkuu wa Wilaya awaruhusu wananchi waweze kuvuna mazao yao huku utaratibu mwingine ukiwa unaendelea?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma ni kati ya mikoa ambayo iko pembezoni na viko vijiji ambavyo vimepakana na nchi jirani ya Burundi na vijiji hivyo havina mawasiliano. Je, Serikali iko tayari kushawishi makampuni kupeleka minara katika Vijiji vya Kitanga (Kasulu), Kilelema (Buhigwe) na Nyagwijima (Kibondo)?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma ni kati ya mikoa ambayo iko pembezoni na viko vijiji ambavyo vimepakana na nchi jirani ya Burundi na vijiji hivyo havina mawasiliano. Je, Serikali iko tayari kushawishi makampuni kupeleka minara katika Vijiji vya Kitanga (Kasulu), Kilelema (Buhigwe) na Nyagwijima (Kibondo)?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru kwa kunipa nafasi, nina swali moja la nyongeza. Tatizo la ukosefu wa Mahakama katika Wilaya ya Chunya ni sawasawa na tatizo llililopo katika Mahakama ya Herujuu. Jengo lililokuwepo la tangu enzi za ukoloni limebomoka kabisa hivyo huduma ya Mahakama wanakaa chini ya miti. Je, ni lini Serikali itatoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama ya Herujuu?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa, wananchi wanaoingia kwenye hifadhi ya misitu siyo kwamba wanaingia kwa sababu ya ukatili ni kwa sababu ya kukosa maeneo ya kuishi na kulima.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano; wananchi wa Wilaya ya Kasulu wanaoingia kwenye pori ya Hifadhi ya Kagerankanda ni kwa sababu watu wameongezeka, ardhi ni ile ile, maeneo ya kilimo yamekuwa ni kidogo. Je, kwa nini, Serikali isiwaruhusu waendelee kulima wakati Serikali inaandaa utaratibu mwingine wa kupima mipaka. (Makofi)
Swali la pili; kwa kuwa, ongezeko la watu ni kubwa sana, kwa nini, Serikali isitenge baadhi ya maeneo ya misitu ili wananchi waruhusiwe kuishi na kuwapunguzia tatizo hili la kuhangaika kutafuta maeneo ya kulima?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Swali la kwanza, katika Wilaya ya Kasulu katika kijiji cha Makere lakini pia katika Wilaya ya Kakonko wananchi wamekuwa wakipata kipato chao kwa kuchimba chokaa, lakini mara nyingi wamekuwa wakizuiliwa kufanya shughuli hiyo. Je, Wizara ya Madini na Wizara ya Maliasili iko tayari kukaa pamoja na wananchi hao ili kuweza kutatua tatizo hilo na kuwawezesha kuwa wachimbaji rasmi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha inatenga eneo la wachimbaji wadogo ili kuepusha migogoro inayoweza kutokea baadaye?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa wapo wazabuni ambao walitoa huduma hiyo ya kusambaza vyakula na vifaa mbalimbali katika shule zetu zikiwemo na shule za watoto wenye ulemavu, lakini wazabuni hao wengi wao wana miaka zaidi ya mitano hawajaweza kulipwa pesa yao na walio wengi wamekopa benki na wengine nyumba zao zimeuzwa na wengine ziko hatarini kuuzwa. Je, Serikali iko tayari kufanya uhakiki wa madeni hayo ili kuweza kuwalipa wazabuni hao? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa wapo wazabuni wapya ambao walitoa huduma ya kusambaza vyakula shuleni wao wamelipwa lakini wazabuni wa zamani hawajalipwa. Je, Serikali iko tayari kuwalipa wazabuni wa zamani ambao walitoa huduma ya kusambaza vyakula shuleni ambao hawajalipwa lakini wapya wamelipwa? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Matatizo yaliyopo Momba ni sawa kabisa na matatizo yaliyopo katika Mkoa wa Kigoma ikiwa ni katika Wilaya ya Kakonko na Buhigwe. Wilaya hizo ni mpya na zimekuwa zikipata huduma kutoka kwenye Wilaya Mama. Ni lini Wilaya ya Kakonko na Buhigwe zitapatiwa Hospitali ya Wilaya? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mkoa wa Kigoma kwa muda mrefu umekuwa haupati watumishi kwa sababu upo pembezoni lakini pia wakimbizi wameingia kwa wingi katika Mkoa wa Kigoma pamoja na kwamba wana hospitali zao kwenye makambi lakini kutokana na binadamu wasivyoweza kuzuiliwa wanaingia kwa wingi katika miji yetu hali inayosababisha wagonjwa kuwa wengi kwenye hospitali zetu. (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Kakonko kwa sasa wanapata huduma katika Kituo cha Afya cha Kakonko na kituo hicho kimezidiwa kwa sababu msongamano wa watu ni mkubwa. Kituo hicho kinahudumia wananchi kutoka hadi Mkoa jirani wa Kagera kwa maana ya wananchi wa Nyakanazi, Kalenge pia na wakimbizi kwa sababu katika Wilaya ile kuna kambi za wakimbizi, Waziri amesema kwamba mwaka 2017/2018 zimetengwa shilingi milioni 500.
Je, Waziri yupo tayari sasa kutokana na jinsi wananchi wanavyopata shida pamoja na waganga na wauguzi kwa sababu watu wakiwa wengi waganga nao wanachanganyikiwa, yupo tayari kufuatilia hizo shilingi milioni 500 ziweze kwenda mara moja Kakonko kwenda kuwasaidia wananchi? (Makofi)
Swali la pili; kwa wakati huu ambapo Wilaya ya Uvinza haina Hospitali ya Wilaya, wananchi wanapata huduma katika vituo vya afya na zahanati, lakini vituo hivyo vya afya pamoja na zahanati havina watumishi wa kutosha.
Je, katika mgao huu wa wafanyakazi ambao wataajiriwa kwa sasa, Serikali iko tayari kabisa kupeleka watumishi wengi wa kutosha kwenda kusaidia katika Wilaya ya Uvinza ambayo haina Hospitali ya Wilaya? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa kulikuwa na ahadi ya Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kununua meli katika maziwa makuu matatu kwa maana ya Ziwa Tanganyika, Ziwa Victoria na Ziwa Nyasa, na katika bajeti hii ya Mawasiliano na Uchukuzi kuna ununuzi wa meli moja ya Ziwa Victoria, lakini hivi karibuni Waziri wa Katiba na Sheria alisikika akipongeza uundwaji wa meli mpya ya mizigo na abiria katika Ziwa Nyasa. Je, ni lini sasa meli mpya itapelekwa katika Ziwa Tanganyika ili tuachane na meli ya MV Liemba?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Kakonko ni kati ya wilaya mpya na mpaka sasa Wilaya hiyo haina Hospitali ya Wilaya. Eneo hilo la Kakonko limepakana na Mkoa wa Kagera na wananchi wengi wanakuja kutibiwa katika Kituo cha Afya cha Kakonko kwa kuwa hawana hospitali jirani yao. Serikali iliahidi kupeleka shilingi milioni 500, mpaka sasa shilingi milioni 500 hizo hazijapelekwa katika Wilaya ya Kakonko. Nilitaka kujua, je, ni lini Serikali itapeleka milioni 500 ili wananchi wa Kakonko waweze kupata huduma ya matibabu? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa vipo vikundi vya akina mama ambavyo vimeanzishwa na kuunda SACCOS, lakini halmashauri hawatoi pesa hiyo asilimia 10 kuvipatia vikundi hivyo na wakati vikundi hivyo havijaweza kukopeshwa na mabenki au taasisi mbalimbali za kifedha.Je, ni kwa nini sasa Serikali isiagize Halmashauri ili vikundi hivyo navyo vilivyoundwa kama SACCOS viweze kukopeshwa pesa hiyo? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwanza naipongeza Serikali kwa kubadilisha utaratibu wa awali kwa sababu utaratibu wa awali wakulima waikuwa hawanufaiki. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa msimu wa mvua katika maeneo mbalimbali hapa nchini unatofautiana, kwa mfano, katika Mkoa wa Kigoma mvua za kupandia ni za mwezi wa Oktoba. Je, Serikali iko tayari sasa kuhakikisha mbolea inawafikia wakulima mapema zaidi kuliko ilivyo sasa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, wapo mawakala waliofanya kazi kubwa ya kusambaza mbolea kwa wakulima. Na kati ya mawakala hao wapo waliofanya kazi kwa uadilifu mkubwa na uaminifu, lakini wapo ambao hawakuwa waaminifu na Serikali ilituma watu kwenda kuhakiki madeni kwa mawakala hao nchi nzima.
Je, ni lini Serikali itawalipa mawakala waliofanya kazi kwa uadilifu, ili waweze kulipa madeni waliyokopa katika benki mbalimbali, wakiwemo mawakala wanawake ambao wanateseka sana kudai pesa zao? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali moja, Mkoa wa Kigoma Wilaya Tano zinapakana na nchi jirani ya Burundi na kati ya Wilaya hizo zina vijiji ambavyo vimepakana kabisa na nchi ya Burundi na wakati mwingine zinapata mawasiliano kutoka Burundi. Je, ni lini Serikali itakaa na makampuni ili kuweza kupeleka minara katika vijiji vya Kalalangabo, Mtanga na Kiziga? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu kuna upungufu mkubwa wa Madaktari na Wauguzi, Muuguzi mmoja anahudumia wodi moja akiwa peke yake hali inayosababisha azidiwe na shughuli. Wagonjwa wanawalalamikia Wauguzi kwamba hawawahudumii lakini ni kutokana na kuzidiwa na kazi nyingi. Je, ni lini Serikali itapeleka Waganga na Wauguzi ili kumaliza tatizo liliko katika Wilaya ya Kasulu? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, katika Mkoa wa Kigoma kuna kambi tatu za wakimbizi. Wilaya ya Kasulu kuna Kambi ya Nyarugusu, Wilaya ya Kakonko kuna Kambi ya Mtendeli na Wilaya ya Kibondo kuna Kambi ya Nduta. Wagonjwa wanapozidiwa katika kambi mbili ya Mtendeli na Nduta katika Wilaya ya Kibondo na Kakonko, wale wa Nduta hupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kibondo na wale wa Mtendeli hupelekwa katika Kituo cha Afya cha Kakonko. Je, ni lini Serikali, kwanza, itapeleka pesa za kumalizia Hospitali ya Wilaya katika Wilaya ya Kakonko na kupeleka Wauguzi na Madaktari? Pili, katika Wilaya ya Kakonko ni lini nao watapelekewa Waganga na Wauguzi wa kutosha ili kumaliza matatizo yaliyopo katika hospitali hiyo? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na swali moja la nyongeza. Mji wa Kibondo unakaabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa maji, na mji huo uko kilimani. Pampu zinazosukuma maji kusambaza ndani ya mji wa Kibondo zimechakaa, ni lini Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya mradi wa maji Wilayani Kibondo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika Mkoa wa Kigoma ipo NGO ambayo imezunguka kwa muda wa wiki mbili katika Wilaya zote saba ikiwatoza wanawake shilingi 10,000 na kuwapigisha picha kwa kuwaahidi kwamba Serikali itatoa mikopo kupitia Mfuko wa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu. Ninataka Serikali inieleze, je, mpango huo wa kutoa pesa kupitia Mfuko wa Mama Samia upo? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Wilaya ya Kakonko takribani kata sita zimepakana na nchi ya Burundi na Kata ya Lugenge na Kasuga nazo pia zimepakana na maeneo hayo ambayo hayana mawasiliano kwa njia ya simu. Mawasiliano ni hafifu na ni shida kabisa, nataka kujua, ni lini Serikali itapeleka minara katika maeneo hayo kiusalama kwa sababu maeneo hayo yamekaribiana na nchi ya Burundi? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa zaidi ya wafungwa katika Gereza la Kasulu ni wakimbizi hali inayochangia gereza hilo kubeba mzigo mkubwa. Je, Serikali iko tayari kukaa na Shirika la UNHCR ili iweze kuchangia pesa katika Gereza la Kasulu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kwa kuwa miongoni mwa huduma nyingine za wafungwa ni pamoja na usafiri; na kwa kuwa gereza la Kasulu ninakabiliwa na ukosefu mkubwa wa gari la kubebea mizigo, lori la kusombea vitu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuni za kupikia chakula; je, ni lini Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya kununua gari kwa ajili ya gereza la Kasulu? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, sijaridhika sana, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na athari kubwa sana zilizoletwa na ujio wa wakimbizi Mkoani Kigoma, ongezeko la watu, miundombinu isiyotosheleza, ni lini hasa mpango kabambe utaletwa? Naomba commitment ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, ujio wa wakimbizi ndani ya Mkoa wa Kigoma, Makambi ya Wakimbizi ya Kibondo, Kasulu na Kakonko yamesababisha uharibifu mkubwa wa mazingira; je, Serikali inalijua hilo? Ni mikakati gani ya Serikali katika kusaidia Mkoa wa Kigoma kutokana na athari hizo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa muda mrefu sana katika Wilaya ya Kasulu, eneo la Kagera Nkanda wananchi walikuwa wakizuiliwa kulima. Mwaka jana tarehe 21 Mheshimiwa Rais alipokuja Wilaya ya Kasulu wananchi walimpokea kwa nderemo na vigelegele akawaruhusu kwenda kulima katika pori la Kagera Nkanda, lakini hivi sasa ninavyoongea tarehe 21 mwezi huu, wananchi wameambiwa waondoe mazao katika eneo hilo la Kagera Nkanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kauli ya Serikali, ni kwa nini wananchi waliruhusiwa na Mheshimiwa Rais kulima katika eneo hilo na leo wanaondolewa kwa kutaka kupigwa ndani ya wiki moja? Naomba kauli ya Serikali. (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kabla ya kuuliza swali naomba uniruhusu niwape pole wananchi wa Jimbo la Buyungu kwa kupoteza Mbunge wao. Naomba wawe watulivu katika kipindi hiki kigumu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mji wa Kakonko bado lipo tatizo kubwa la upatikanaji wa maji. Katika mji huo maji hutoka mara tatu kwa wiki katika visima viwili; kimoja ni kisima cha Mbizi ambacho kinatumia pampu na cha pili ni kisima cha Kanyovi kinachotumia solar. Nashukuru Serikali katika bajeti hii kwa kutupangia pesa. Je, ni lini sasa mradi huo utaanza katika Mji wa Kakonko? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; katika Kata ya Mwilamvya ndipo yalipo machinjio ya ng’ombe, mbuzi na kondoo. Eneo hilo hupata maji mara mbili kwa wiki au mara tatu, lakini hivi sasa ninavyoongea eneo hilo halina maji na ni muda wa mwezi mzima maji hayapatikani katika eneo hilo.
Je, Serikali iko tayari kutoa pesa kwa mpango wa dharura ili eneo hilo la machinjio liweze kupatiwa maji? (Makofi)
Swali langu la pili, katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu DC ipo miradi ya maji ambayo haijakamilika, imefikia asilimia 85 mpaka 95 lakini imekwama kwa ajili ya ukosefu wa pesa; je, ni lini sasa Serikali itamalizia miradi hiyo kwa kupeleka pesa ili miradi hiyo iweze kukamilika na wanawake waweze kuondolewa adha ya upatikanaji wa maji? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu maswali mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, kabla ya kuuliza swali langu, naomba nichukue nafasi hii kupongeza Halmashauri ya Kusulu TC kwa kuweza kufanya vizuri kwa kutoa pesa hizo kila baada ya miezi mitatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza, kwa kuwa wanawake wengi, vijana pamoja na walemavu wameweza kuhamasika kufungua vikundi lakini zipo Halmashauri ambazo zinasuasua na nyingine kutokupeleka pesa hizo kama sheria inavyotaka. Je, Wizara iko tayari sasa kutoa agizo ili Halmashauri hizo ziweze kutoa pesa kwa wakati?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, zipo Halmashauri ambazo bado ni changa mfano Halmashauri ya Kakonko pamoja na Buhigwe, makusanyo yao sio mazuri sana, ni kidogo. Je, Serikali inatoa kauli gani kwa kuzisaidia Halmashauri hizo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tarehe 10 Agosti, 2018, Waziri wa Nishati alizindua mradi wa REA III katika Mkoa wa Kigoma katika Kijiji cha Lusesa, Kata ya Lusesa na akaahidi kwamba baada ya mwezi mmoja umeme utawaka katika kata hiyo na viunga vyake vinavyozunguka kata hiyo, lakini mpaka leo umeme haujawaka. Nataka nijue ni lini Serikali itaagiza wanaohusika na umeme waweze kuwasha umeme katika kata hiyo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya hizo nilizozitaja, vipo vijiji ambavyo ukipiga simu mawasiliano unayoyapata ni ya nchi jirani ya Burundi siyo Tanzania. Kwa mfano, katika Wilaya ya Kakonko ipo Kata ya Mgunzu, kipo Kijiji cha Kigra na Chulazo ambavyo mawasiliano yake ni ya shida. Hata katika wilaya nilizozitaja viko vijiji ambavyo havikuweza kutajwa kwenye jibu la Waziri ambavyo mawasiliano yake bado ya wasiwasi. Je, Serikali iko tayari kuendelea kuhamasisha makampuni kujenga minara katika maeneo hayo ili wananchi waweze kupata mawasiliano ya uhakikika?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Serikali imeamua zao la mchikichi lilimwe Kigoma na liweze kuwa zao la biashara na Waziri Mkuu kwa kuweka msisitizo ameenda Kigoma mara tatu kufuatilia zao hili la mchikichi; na kwa kuwa wananchi wameamua kuitikia mwito huo wa kulima zao hilo…

MWENYEKITI: Swali.

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali iko tayari sasa kuhakikisha wananchi wanapata mbegu na kuanza kulima zao hilo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa muda wa miradi hiyo kutokukamilika umekuwa mrefu sana, je, Serikali iko tayari kupeleka pesa ya kutosha ili miradi hiyo iweze kukamilika?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa Makao Makuu ya Wilaya za Kibondo na Kakonko upatikanaji wa maji umekuwa ni wa kusuasua, na wilaya hizo zina watu wengi kutokana na ongezeko la watu wengi wakiwemo wakimbizi, na zipo taasisi nyingi ambazo ziko pale zikiwemo hospitali, shule pamoja na ofisi za mashirika ya wakimbizi. Ni lini sasa Serikali itapeleka pesa katika Wilaya za Kakonko na Kibondo kumaliza tatizo la maji katika miji hiyo mikuu ya wilaya hizo? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, barabara ya kutoka Uvinza kuelekea kwenye Daraja la Kikwete - Malagarasi, barabara hii iliahidiwa kujengwa kwa pesa za kutoka Abu Dhabi. Nataka Serikali iniambie ni lini sasa kipande hiki cha kilometa 48 kitakamilika?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nina swali moja la nyongeza; katika halmashauri zetu zipo SACCOS za vijana na wanawake ambazo zimeundwa na wanawake na vijana, lakini SACCOS hizo hazikopeshwi kupitia Mifuko ya Halmashauri. Sasa, ni lini Serikali italeta sheria Bungeni ili SACCOS hizo za vijana na wanawake ziweze kukopesheka kupitia Mfuko wa Halmashauri?
MHE. JOSOPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Pamoja majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakulima wetu wakiwemo wanawake na vijana wanatumia nguvu nyingi, wanatumia muda mwingi, lakini pia wanatumia pembejeo ambazo wanakuwa wamezikopa kwenye vikundi mbalimbali. Wanakopa pesa, wananunua mbolea na dawa; na wanapokuwa wamelima na wamevuna wanakosa soko hatimaye wanashindwa kulipa madeni pale walipo kopa pesa.

Je, Serikali ina mpango gani na inachukua hatua gani kuwa inauza mazao nje ya nchi? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa usanifu ulikamilika na kuwa usanifu unaofanyika ni uhuishaji wa usanifu wa awali. Je, Serikali haioni haja kutenga fedha mwaka ujao wa fedha ili kujenga daraja hilo 2021/2022 ili kunusuru maisha ya wanawake na watoto wanaopoteza maisha kwasababu ya kutokuwa na kivuko hicho?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Kwa kuwa, kivuko kinaanca kazi saa 01:00 asubuhi na kuishia saa 01:00 jioni. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza saa ili kivuko hicho kifikie saa 06:00 usiku kuweza kuwanusuru wananchi wanaopoteza maisha kutokana na saa hizo kuwa fupi?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kipande cha barabara ya kutoka Uvinza hadi Malagarasi, kilometa 48, Serikali iliahidi kukijenga kwa msaada wa pesa za Falme za Kiarabu. Tangu mwaka juzi, 2019 Serikali imekuwa ikisema kwamba kipande hicho kitajengwa kwa pesa hizo za msaada wa Falme za Kiarabu:-

Je, ni lini sasa Serikali itajenga kipande hicho cha kutoka Uvinza hadi Malagarasi? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza. Kutokana na majibu yaliyotolewa na Serikali, inaonyesha ni dhahiri ni Halmashauri mbili tu kati ya Halmashauri 184 nchi nzima ambazo zimepatiwa pikipiki. Hali hii inaonyesha jinsi ambavyo upo uhitaji mkubwa katika Halmashauri nyingine. Je, Serikali ina mkakati gani wa makusudi kuhakikisha kitengo hicho kinawezeshwa kibajeti katika Halmashauri zote? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nina swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi. Kipande cha barabara ya kutoka Uvinza mpaka Malagarasi kilometa 51 kiliahidiwa kujengwa tangu kwenye utawala wa Rais wa Awamu ya Nne Dkt Kikwete. Kipande hicho mpaka leo hakijaweza kujengwa lakini Chagu mpaka Kazilambwa nayo haijakamilika. Ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa kipande hicho cha kilometa 51?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kazi kubwa katika kusimamia vyama vya ushirika ipo kwenye wilaya zetu. Je, vifaa hivi vilivyozungumziwa vinaelekezwa kwenye Wilaya au Mikoa? (Makofi)

Pili, Taarifa ya Shirika la Ukaguzi (COASCO) ya mwaka 2019/2020 inaonesha ni vyama 6,021 vilifanyiwa ukaguzi, kati ya vyama hivyo ni vyama 289 nivyo vilivyopatiwa hati safi, sawa na asilimia 4.8.

Je, Serikali haioni kwamba ipo haja ya kuwawezesha maafisa ushirika ili waweze kufanya kazi hiyo kwa ufanisi zaidi? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mafupi. Nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kibondo ni kati ya Wilaya kongwe nchini, Wilaya hiyo haina Chuo cha VETA. Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Kibondo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kata ya Rungwe Mpya iliyoko Jimbo la Kasulu Vijijini ina idadi kubwa ya watu wengi sana: Je, ni lini Serikali itakubali kuigawa kata hiyo?
MHE. JASEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Pamoja na majibu yake nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Kagera/Nkanda iko kilomita 70 kutoka Makao Makuu ya Wilaya. Kutoka Kagera/Nkanda mpaka Mgonde mara nyingi hutokea uhalifu wa utekaji wa magari, ikitokea dharura usiku wanawake wanashindwa kufikishwa katika hospitali ya Wilaya kutokana na kuogopa kutekwa magari usiku.

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kata ya Kagera/Nkanda?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nina swali moja; je, ni lini Serikali itaweka minara ya mawasiliano kati ya Manyoni na Tabora?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Uvinza?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Kigoma ni lango kuu la uchumi wa nchi yetu kwa sababu umepakana na nchi za jirani za DRC Congo na Burundi. Mara nyingi serikaliimekuwa ikiahidi kuja kujenga uwanja wa ndege Kigoma na kuweka taa kwa maaa ya ndege ziweze kuruka usiku.

Sasa nataka Waziri aniambie ni lini Serikali itakuja kuweka taa na kuongeza uwanja wa ndege wa Mkoa wa Kigoma kwa sababu Kigoma imepakana na nchi jirani za Congo na Burundi?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Jimbo la Kigoma Kusini vipo vijiji vilivyopakana kabisa na Ziwa Tanganyika lakini vijiji hivyo havijapatiwa maji. Ni mpango upi wa Serikali kuvipatia vijiji hivyo vinavyopakana na Ziwa Tanganyika?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante mwanzoni nilisema Spika, nafanya marekebisho. Kwa kuwa kuna upungufu mkubwa wa walimu wa hisabati, na wanafunzi wamekuwa wakishindwa kufanya vizuri kutokana na ukosefu wa walimu wa hisabati. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha shule zote nchini zinapatiwa walimu wa hisabati kama ilivyowahi kufanya kwenye somo la sayansi?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kipande cha barabara ya kutoka Uvinza – Kasulu kupitia Basanza hakina lami, na mara nyingi matukio ya unyang’anyi na ujambazi hutokea katika barabara hiyo ya Uvinza – Kasulu.

Je, ni lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika Mji wa Kasulu maji yanayotoka kwenye mamomba ni machafu na yana tope, tulileta ombi hili ndani ya Bunge lako na Waziri akaahidi kumaliza tatizo hilo. Je, ni lini sasa tatizo hilo la maji katika Mji wa Kasulu litapatiwa majibu?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nampongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake kwamba asilimia zilizokuwa zikikopeshwa kwenye Halmashauri zipitie benki: -

Mheshimiwa Spika, sasa kwa kuwa wanawake na vijana watakuwa wanakopeshwa kupitia benki: Je, ni kwa nini sasa Serikali isiamue vikundi ambavyo ni vya wanawake na vijana vilivyounda SACCOS navyo viunganishwe katika kukopeshwa kupitia benki? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga barabra ya kutoka Simbo kwenda Kalia?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Barabara ya kutoka Uvinza mpaka Kasulu itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, ni lini Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Kazegunga – Mahembe – Kitanga – Kinazi mpaka Buhigwe? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika shule zote za msingi, sekondari na taasisi za dini katika wilaya zote Mkoa wa Kigoma?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Je, ni lini Barabara ya Uvinza – Maragarasi yenye kilometa 51 itamalizika kujengwa kwa kiwango cha lami?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa barabara hiyo inategemewa kiuchumi kutoa mazao sokoni, kupitisha watalii kwenda Mahale, na kwa kuwa mara nyingi Serikali imekuwa ikijibu upembuzi yakinifu, usanifu kwa muda mrefu, zaidi ya miaka mitano.

Je, Waziri anaweza akanihakikishia kabisa ni lini sasa barabara hiyo itaanza? (Makofi)

Swali langu la pili, kwa kuwa Kivuko cha Ilagala huanza kazi saa 12 na kuishia saa 12 na kinategemewa na Kata ya Sunuka, Sigunga, Helembe na Kalya, saa 12 mawasiliano yanakuwa yamekatika.

Je, kwa nini Serikali isiongeze muda kivuko kikafanya kazi mpaka Saa Sita usiku? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza: Kwa kuwa kituo hicho cha Kizazi kilianza kujengwa kwa nguvu za wananchi tangu 2019, mpaka sasa ni miaka mitano; na ninaishukuru Serikali kwa kutenga fedha hizo, lakini mpaka sasa hazijaanza kwenda; nataka Serikali inihakikishie: Je, ni lini kituo hicho kitakamilika ili wananchi waanze kupata huduma katika kituo hicho? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Katika Halmashauri ya Kasulu DC, ipo zahanati katika Kata ya Kagerankanda, zahanati ya Uvinza ina watumishi wawili tu, tena wanaume: Je, ni lini Serikali itamwagiza Mganga Mkuu pamoja na Mkurugenzi kupeleka watumishi wa kile katika zahanati hiyo? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante; je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kuanzia Kalela – Munzeze mpaka Buhingwe kwa kiwango cha lami? (Makofi)

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Katika Mji wa Kasulu eneo la Mwilamvya kuna tatizo la upatikanaji wa maji. Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji katika Mji wa Kasulu?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Tarafa ya Heru Juu iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu haina Mahakama, inafanyia kazi katika Ofisi ya Mtendaji. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Tarafa ya Heru Juu? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, je, ni lini kipande cha barabara cha kuanzia Malagarasi – Mpeta mpaka Uvinza kitakamilishwa kujengwa kwa kiwango cha lami?

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Sswali la kwanza, kama ni hivyo ni kwa nini sasa mbolea hizo kwa vifungashio ulivyovitaja hazipo madukani? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa mvua za kwanza ni za kupandia. Je, katika Mkoa wa Kigoma kwa mwaka huu mbolea zitafika Mkoa wa Kigoma mwezi gani? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Halmashauri ya Kasulu Vijijini ipo barabara ya kutoka Mgombe kwenda Kagerankanda, barabara hiyo hutumika kwa wakulima kupitisha mazao kupeleka majumbani kwao.

Je, ni lini Serikali itatoa pesa kwa TARURA ili barabara hiyo iweze kutengenezwa?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika Halmashauri ya Kasulu Vijijini ipo miradi ya umwagiliaji katika Kata ya Titye na Rungwe Mpya. Miradi hiyo haijakamilika kutokana na ukosefu wa fedha.

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha miradi hiyo? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, Je, ni lini Serikali itajenga skimu za umwagilaiji kwa kutumia maji ya Mto Rwiche katika manispaa ya Kigoma Ujiji?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Uvinza?

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu DC Barabara ya Mgombe – Kagerankanda mpaka Mvinza ni barabara ya kiuchumi na hupitisha malori makubwa kwenda kuchukua chokaa kupeleka nchi jirani ya Burundi; je, ni lini Serikali itajenga barabara hiyo? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, Ahsante. Nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Pamoja na majibu yake nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Katika Wilaya ya Buhigwe Kata ya Mkatanga, wananchi wa Kijiji cha Kitambuka waliomba kujengewa kituo cha afya na ombi hilo walilitoa mbele ya Makamau wa Rais Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango, na tayari wanayo matofali.

Je, Serikali iko tayari kutoa pesa ili wananchi waweze kujengewa kituo hicho? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu DC, Kata ya Kagera Nkanda iko umbali mrefu sana kutoka yaliko Makao Mkauu ya Halmasahuri ya Kasulu DC, ambapo ni kilometa 77 kutoka Makao Makuu.

Je, Serikali iko tayari kujenga kituo cha afya katika Kata ya Kagera Nkanda?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika Halmashauri hakuna sheria inayoruhusu vikundi vya SACCOS kukopeshwa. Je, ni lini Serikali italeta sheria Bungeni ili kufanya marekebisho SACCOS ziweze kukopeshwa?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika Mji wa Kasulu lipo tatizo la umeme kukatikakatika wakati wa mchana na kurudishwa usiku. Je, ni lini tatizo hilo litakwisha? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Kituo cha Muhange kipo mahali ambapo lipo soko la Ujirani Mwema na mara nyingi hutokea uhalifu na kutokana na ukosefu wa gari, Maaskari wa eneo hilo hulazimika kuazima pikipiki kwa Diwani wa eneo hilo. Ni lini sasa Serikali itapeleka japo pikipiki kwenye Kituo hicho? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kituo cha Kitanga katika Wilaya ya Kasulu kiko mpakani, eneo hilo linatenganishwa na Mto Malagalasi, ukitoka Kitanga kwenda Malagalasi unavuka Mto Malagalasi. Kwa hiyo naangalia ni jinsi gani kuna umuhimu wa kupeleka gari katika eneo hilo, na eneo hilo, kutoka Kitanga kwenda Kasulu Mjini ni kilomita 150, katika eneo hilo hutokea ujambazi mara nyingi.

Ni lini sasa kwa umuhimu wa eneo hilo Serikali itapeleka gari ili kunusuru maisha ya wananchi? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Serikali iliahidi kujenga jengo la Mahakama katika Tarafa ya Heru, tarafa maalum ambayo alikuwa akiishi Mwami Theresa Ntare. Je, ni lini sasa Serikali itajenga jengo kumuenzi Mwami Theresa Ntare? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma tulichelewa kupata umeme wa awamu ya kwanza na ya pili: Je, katika awamu wa tatu mzunguko wa pili, Serikali ipo tayari kumsimamia mkandarasi ili umeme uweze kufika vijijini na katika vitongoji vyote? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante; je, ni lini Serikali itajenga daraja linalounganisha Kalya na Ilagala katika Mto Malagarasi?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Kata ya Kitanga iko kilometa 77 kutoka yalipo makao makuu ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya katika kata hiyo?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Serikali iliahidi kujenga jengo la Mahakama katika Tarafa ya Heru, tarafa maalum ambayo alikuwa akiishi Mwami Theresa Ntare. Je, ni lini sasa Serikali itajenga jengo kumuenzi Mwami Theresa Ntare? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali iliahidi kufunga umeme katika shule zote za sekondari na taasisi za dini, lakini zipo shule ambazo hazijaweza kufungiwa umeme; je, ni lini Serikali itafunga umeme katika Shule ya Sekondari Kimenyi, katika Halmashauri ya Kasulu DC? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza; kwanza nishukuru Serikali kwa kuweka Mji wa Kasulu kati ya miji 28 itakayonufaika na mpango wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kwa wakati huu ambapo kuna mlipuko wa kipindupindu je, Serikali ina mpango upi wa dharura wa kuweza kuwasaidia wananchi wa Kasulu ili kuondokana na tatizo la maji machafu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili katika Halmashauri ya Kasulu DC zipo kata ambazo tayari zimeshachimba visima lakini maji hayajasambazwa kutokana na ukosefu wa miundombinu ya mabomba. Kata hizo ni Kata ya Kasangezi, Lusesa, Hurugongo na Shunguliba. Ni lini Serikali itamaliza matatizo hayo katika kata hizo nilizozitaja? (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya kutoka Kalela – Munzeze – Buhigwe kwa kiwango cha lami?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's