Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Mary Pius Chatanda

Supplementary Questions
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Napenda kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Walimu wamekuwa wakinyanyasika sana katika suala la upandishwaji wa madaraja na hata wanapokuwa wamepandishwa hayo madaraja, bado malipo yao kulingana na madaraja waliyopewa hawapewi kwa wakati, inawachukua muda mrefu kulipwa kulingana na madaraja waliyopewa. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya jambo hili?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Naomba niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa amesema kwamba umeme umeunganishwa katika Gridi ya Taifa kule Hale; na kwa kuwa Korogwe imekuwa umeme unakatika mara kwa mara. Je, ni lini umeme utakoma kukatika ili kusudi wananchi wa Korogwe Mjini waweze kufanya shughuli zao za biashara pamoja na shughuli nyingine bila kuwa na kukatika kwa umeme?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuulize Waziri, amesema kuna wawekezaji ambao wanakusudia kuwekeza pale Kwamsisi, natoa pongezi kwa sababu kiwanda kile kinakuja katika Mkoa wetu wa Tanga. Kwa kuwa ndiyo wanatarajia kuanza kulima hayo mazao ambayo yatalisha kiwanda hicho, je, haoni ni wakati muafaka kwa matunda yaliyopo sasa na hasa ikizingatiwa kwamba Serikali imeshasema itafufua kwanza viwanda vilivyokuwepo hasa kiwanda kilichokuwepo pale Korogwe, ni kiwanda kidogo lakini kinaweza kutengeneza juice kikafufuliwa hicho kwanza wakati tunasubiri kiwanda kikubwa?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Naomba niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Waziri, Korogwe ilikuwa na mradi wa World Bank ambapo ilikamilisha miradi yake Kwa Msisi, Ngombezi na Kwa Mndolwa na ikabakiza mradi wa Rwengela Relini, Rwengela Darajani na Msambiazi. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha miradi hiyo ambayo imebakia?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mji wa Korogwe unapitiwa na Mto Pangani katikati ya mji, je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kwa kuutumia mto ule kuwapatia watu wananchi wa Mji wa Korogwe maji hasa ikizingatiwa kwamba wana shida ya maji, wanaangalia mto lakini maji hawayapati?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Sambamba na suala la madawati, wananchi wameitikia wito wa uandikishaji wa watoto shule za awali pamoja na darasa la kwanza. Je, Serikali iko tayari sasa kupeleka Walimu wa madarasa haya ya awali kwa sababu madarasa hayo hayana Walimu?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa walimu wamejiunga na PSPF lakini walimu hawa wanapoomba mikopo watu wa PSPF wanachelewa sana kuwapa majibu na kuwakamilishia haki yao ya msingi ambapo wengine wanakuwa wamekaribia kustaafu wanataka wajiandae. Je, Serikali inawaelezaje walimu hawa ambao wanakaribia kustaafu na wanahitaji wapate huo mkopo wanawacheleweshea kuwapa mkopo huo?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Wilaya ya Korogwe ina Halmashauri mbili na Halmashauri ya Mji wa Korogwe haina hospitali, wananchi wake asilimia 60 wanatibiwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya na kusababisha msongamano mkubwa katika hospitali hiyo. Halmashauri ya Mji tuna zahanati ipo Kata ya Majengo ambayo vilevile inalaza akina mama wajawazito wanajifungulia pale.
Je, Serikali sasa kwa maana ya Wizara ya Afya hasa ikizingatiwa kwamba hatuna hospitali itakuwa tayari kutusaidia kujenga jengo la upasuaji ili kusudi wa kina mama wale wajawazito wasiende kule kwenye hospitali ya Magunga ambako kuna msongamano mkubwa?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa niulize swali la nyongeza. Wafanyakazi wamekuwa wakikatwa fedha zao na kupelekwa kwenye huu mfuko wa PSPF. Lakini wafanyakazi hawa wanapokuwa wamemaliza huo muda wanacheleweshewa kupewa mafao yao. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuona kwamba, wafanyakazi hawa wanapomaliza muda wao wawe wanaandaliwa cheque zao mapema ili kusudi ziweze kuwasaidia katika kufanya shughuli zao wanazokuwa wamejipangia kuliko hivi sasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, je, Mheshimiwa Waziri amejibu amesema wameshaanza kulipa; anaweza sasa akanisaidia mimi orodha ya Mkoa wa Tanga, hususan Korogwe, wale ambao wamekwishalipwa ili wasiendelee kunieleza kwamba wanadai? Nipate ile orodha ili iweze kunisaidia.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Chama cha Mapinduzi ndicho kilichoshinda katika uchaguzi mkuu uliokwisha hivi karibuni mwaka 2015; na kwa kuwa Serikali iliyoko madarakani sasa inatakiwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi iliyojinadi kwa wananchi wake; na kwa kuwa ziko nchi ambazo uchaguzi ukishamalizika vyama vya siasa vingine havipaswi kwenda kufanya mikutano ya hadhara, je, hatuoni sasa ni wakati muafaka wa kufanya marekebisho ya sheria ili chama kilichoko madarakani kiweze kuachiwa nafasi ya kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa usalama barabarani ni pamoja na kusimamia kuhakikisha kwamba ajali hazitokei mara kwa mara.
Je, Korogwe kutoka Chalinze hadi Same ni kilometa kama 370 na kitu, je, Serikali kwa maana ya Wizara ya Mambo ya Ndani, askari wa Korogwe Mjini wao ni mara nyingi ndiyo ambao huwa wanashughulikia ajali kutoka kwenye maeneo hayo niliyoyasema hizo kilometa zote hizo. Watakuwa tayari kuwapatia gari askari wa barabarani ili waweze kufanya patrol ili waweze kupunguza ajali zinazotokea barabarani?

MHE. MARY P. CHATANDA: Korongwe Mjini.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwenye taarifa ya Waziri wa Fedha aliyoiwasilisha hii ya bajeti, imezungumzia tu suala la milioni 50, kwamba zitakwenda kwenye vijiji, haikuzungumzia Mitaa, kama ambavyo Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan walizungumza walipokuwa wakipita kwenye kampeni kwamba watahakikisha Mitaa na Vijiji vinapata mikopo ya milioni 50. Je, Serikali inatuambia nini juu ya wananchi wanaoishi mijini, ambao wana mitaa badala ya vijiji?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Wakuu wa Wilaya ndiyo Watendaji Wakuu ambao wanakutana na wananchi kwa karibu zaidi. Je, Waziri anaweza sasa kufanya mabadiliko badala ya kupeleka OC kwa RAS wakapeleka moja kwa moja kwa DAS ili kusudi waweze kufanya kazi zao vizuri zaidi?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa, Bunge lililopita kuna fedha zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya ile miradi 10 ya World Bank katika Vijiji Mji vya Mji wa Korogwe ikiwemo Lwengela Relini, Lwengela Darajani na Msambiazi. Je, Serikali ina mpango gani kwa sababu kwenye bajeti hii sijaona hiyo fedha? Safari iliyopita hawakupewa zile fedha, safari hii wana mkakati gani kuhakikisha kwamba vijiji hivi vinachimbiwa vile vile visima virefu kama ambavyo ilikuwa imepangwa?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa suala la mashamba ya mkonge kwa upande wa Korogwe Vijijini inafanana na Korogwe Mjini, na kwa kuwa Korogwe Mjini tayari ilishaingia kwenye mpango kabambe wa masterplan, na kwa kuwa mji huu una mashamba ya mkonge nayo ambayo hayaendelezwi na tayari tulishaleta mapendekezo ya kuomba mashamba hayo yafutwe.
Je, Serikali inatuambiaje na hasa ikizingatia kwamba tupo kwenye ule mpango kabambe wa masterplan kuhakikisha kwamba mashamba hayo yanafutwa ili maeneo hayo yaweze kutumika katika huu mpango kabambe ambao umeandaliwa?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwanza, naishukuru Wizara ya Elimu iliweza kutoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa Chuo cha Ualimu pale Korogwe ambapo kilileta wanachuo karibu 800 na kitu kwa ajili ya mafunzo pale. Hata hivyo, naiomba Serikali, kwa kuwa chuo kile kina maktaba ndogo na sisi wananchi tumeweza kujenga maktaba kubwa ambayo ingeweza kuwasaidia wanachuo ambao ni wengi sasa pale chuoni, pamoja na wananchi wa Korogwe kwa ujumla: Je, Serikali itakuwa tayari kutupa fedha ili tuweze kukamilisha lile jengo la maktaba?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kama ambavyo Naibu Waziri amesema kwamba chuo kile kina uwezo wa kudahili wanachuo 1,200 na ameeleza mwenyewe kwamba 2015/2016 kilidahili wanachuo 234. Kutokana na miundombinu na rasilimali iliyopo pale, kuwa na wanafunzi 234 kati ya 1,200 hatuoni kwamba hatukitendei haki chuo hiki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kuna utaratibu ule wa kuwadahili kupitia mtandao na huko vijijini hakuna mitandao kwa nini isirejee utaratibu wa kuandika barua pamoja na kutumia hizo internet kwa wenzetu walioko mijini ili watoto wa wanavijiji na wenyewe waweze kupata hizi nafasi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, zamani utaratibu ulikuwepo wanafunzi ambao wako shuleni walikuwa wakiomba nafasi za ualimu wakiwa shuleni. Je, kwa nini wasirudishe utaratibu huo mtu aweze kuomba akiwa shuleni ili tuweze kupata wanachuo wa kutosha kuliko kuwa na chuo ambacho kinataka wanafunzi 1,200 halafu wanadahili wanachuo 234?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri, alipotembelea Wilaya ya Korogwe aliweza kuona hali halisi ya tatizo la maji lililopo katika mji wetu wa Korogwe. Hata hivyo aliahidi kutuletea shilingi bilioni mbili ili angalau tatizo la maji lile liweze kuondoka pale, swali; kwa kuwa
wameshatuletea milioni 500 kwa ajili ya kutoa maji kutoka kwenye Mto Ruvu, je, sasa Serikali zile fedha wameshaziingiza kwenye bajeti ili kusudi ziweze kutusaidia katika kutengeneza miundombinu ile ambayo ni mibovu maana yake
tutakapokuwa tumejenga matenki au tumejenga ule mkondo wa maji bila ya kuwa na matenki ya maji makubwa bado tatizo la maji litakuwa lipo pale Korogwe. Je hizi fedha shilingi bilioni mbili alizosema zimetengwa katika bajeti hii? Nashukuru.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Wizara ya Utumishi ina watumishi wanaofanya kazi vizuri, hawajatumbuliwa, Serikali kwa maana ya Chuo cha Ualimu, kutokana na swali langu namba 81 ambalo nilijibiwa kwamba suala la upandishaji madaraja na likizo za Watumishi wamelipwa kwa kiasi kile ambacho walikuwa wamekitaja.
Je, watakuwa tayari sasa kutoa orodha ile ya wale waliokwishalipwa kwa Chuo kile cha Korogwe cha
Ualimu ili kusudi Walimu waweze kujitambua kwa sababu huwa kama wanawalipa, wanaingiza moja kwa moja kwenye mishahara, watakuwa tayari kuitoa hiyo orodha ili iende kwa Mkuu wa Chuo kila mtu aweze kutambua kile alichoweza kulipwa?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza nampongeza Waziri wa Elimu na Naibu wake na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa basi, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kufuatana nami ili aweze kuangalia lile jengo ili kusudi waweze kutoa kitu ambacho kinalingana na kazi ambayo inakusudiwa kumaliziwa?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sikubaliani na majibu ambayo yametolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri, hayaridhishi kabisa. Ukiangalia kwa mtiririko ulioko kwenye majibu haya imesema wazi mwaka 2006/2007 walifanya upembuzi na kugundua kwamba shilingi bilioni kumi na tatu ilihitajika kwa ajili ya mradi huu lakini wakafanya upembuzi tena mwaka 2014/2015 ikaonekana shilingi bilioni 1.54 zilitakiwa kwa ajili ya ujenzi wa bwawa hili lakini bado wakafanya mwaka 2015/2016 wakatenga milioni 800.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najenga hoja naomba utulie. (Kicheko) [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]
Mheshimiwa Mwenyekiti, walitenga fedha hizi shilingi milioni 800 hazikutoka, halafu mwaka 2016/2017 hawakutenga fedha…
… 2017/2018 hawakutenga fedha, sasa ni kwa nini wanazungumza uongo? Kwa nini hawakutenga fedha katika miaka miwili hii ambayo imo mpaka bajeti ya safari hii wanazungumza…
Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna mtu ambaye amekamilika, ulimi inawezekana umeteleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali haioni sasa kwamba kutokutekeleza mradi hii hawawatendei haki wananchi wa Wilaya ya Korogwe hususan Manga Mkocheni?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa niulize swali la nyongeza. Katika jibu la msingi la Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba Teaching Allowance ipo kwenye mshahara. Sasa tunapata tabu sana tukikutana na Walimu wanapotuambia juu ya kurudisha Teaching Allowance. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutamka ndani ya Bunge hili ili waweze kutambua kwamba Teaching Allowance yao iko kwenye mshahara?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwanza, niipongeze Wizara hii kwa maana ya MSD kwa kuwa sasa wanatoa dawa za kutosha katika hospitali zetu. Hata hivyo, kwa kuwa hospitali hizi zinapokuwa zinakosa hivi vifaa tiba, kama ambavyo amezungumza kwenye jibu lake la msingi, kwamba wanaruhusu kwenda kununua kwa wazabuni, haoni kwamba kitendo cha kwenda kununua kwa wazabuni bei ni kubwa mara mbili zaidi ya vile vifaa ambavyo wanakwenda kuvinunua kama vile dawa za amoxicillin pamoja na vile vifaa vya theater. Hawaoni kwamba sasa inakuwa ni gharama kubwa zaidi kuwahudumia hao wagonjwa ambao wanaokwenda kwenye hizi hospitali? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pili, kwa kuwa anasema kwamba mteja apewe ndani ya siku moja ili kwenda kununua kwenye haya maduka ya watu binafsi. Kwa nini isiwe ndani angalau ya wiki moja kuliko ile siku moja ili mtu apate nafasi nzuri ya kuweza kwenda kununua hizo dawa?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kunipa nafasi ili na mimi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti tatizo la Karatu linafanana
na tatizo la Korogwe Mjini. Korogwe Mjini haina hospitali, kwa maana ya Halmashauri ya Mji, na Wilaya yetu tumeamua kwa makusudi kabisa kujenga kwanza kituo cha afya ambacho tutakifanya kiwe hospitali.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kutusaidia kutupiga jeki kwa sababu tunajenga kituo cha afya chenye ghorofa tatu?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwanza napongeza TARURA kwamba wameanza kazi vizuri hususani katika Mji wangu wa Korogwe, lakini napenda kujua je, Wizara ina mpango gani sasa wa kuwawezesha hawa TARURA hususani kwenye hizi Halmashauri za Miji pamoja na kwamba wanawapa fedha za kujenga barabara zile kwa kiwango cha changarawe, sasa wapewe fedha za kutengeneza ile mifereji kwa kiwango cha kutumia mawe ili kusudi wasiweze kurudia mara kwa mara kutengeneza zile barabara? Wana mpango gani wa kuwatengea fedha ili Miji hii iweze kuwa na barabara zilizo imara kwa kupitia kuweka mawe misingi yao? (Makofi)
MHE. MARY P.CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pia nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri kwa kutukumbuka Korogwe, Kilindi na Mkinga kwamba mwaka huu wa fedha watatupatia fedha kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama. Swali la nyongeza, kwa kuwa vile vile Mahakama hizi zimekuwa na upungufu mkubwa wa wafanyakazi hususan Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutupelekea Mahakimu Mahakama za Mwanzo Korogwe Mjini na Vijijini? Ahsante sana.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sikubaliani na majibu ambayo yametolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri, hayaridhishi kabisa. Ukiangalia kwa mtiririko ulioko kwenye majibu haya imesema wazi mwaka 2006/2007 walifanya upembuzi na kugundua kwamba shilingi bilioni kumi na tatu ilihitajika kwa ajili ya mradi huu lakini wakafanya upembuzi tena mwaka 2014/2015 ikaonekana shilingi bilioni 1.54 zilitakiwa kwa ajili ya ujenzi wa bwawa hili lakini bado wakafanya mwaka 2015/2016 wakatenga milioni 800.
Mheshimiwa Mwenyekiti, walitenga fedha hizi shilingi milioni 800 hazikutoka, halafu mwaka 2016/2017 hawakutenga fedha…

… 2017/2018 hawakutenga fedha, sasa ni kwa nini wanazungumza uongo? Kwa nini hawakutenga fedha katika miaka miwili hii ambayo imo mpaka bajeti ya safari hii wanazungumza…

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali haioni sasa kwamba kutokutekeleza mradi hii hawawatendei haki wananchi wa Wilaya ya Korogwe hususan Manga Mkocheni?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa niulize swali la nyongeza. Katika jibu la msingi la Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba Teaching Allowance ipo kwenye mshahara. Sasa tunapata tabu sana tukikutana na Walimu wanapotuambia juu ya kurudisha Teaching Allowance. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutamka ndani ya Bunge hili ili waweze kutambua kwamba Teaching Allowance yao iko kwenye mshahara?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nimpongeze vilevile yeye mwenyewe kama Naibu Waziri na Waziri wake kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha kwamba wanawapatia wananchi umeme. Nina maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mradi huu unaonekana utakwenda hadi Arusha, na kwa kuwa tayari wananchi wa Kibaha wao wameshafanyiwa tathmini ya kuhakikisha kwamba wanapata hizi fedha ambazo zimetengwa. Je, hawa wananchi wengine ambao watapitiwa na umeme hadi Arusha ni lini sasa watafanyiwa tathmini hiyo ili nao waweze kulipwa fidia zao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Korogwe Mjini tunapata umeme ambao unawaka na kuzimika au unachezacheza, nini tatizo la umeme huo Korogwe Mjini? Naomba nipatiwe majibu. (Makofi)
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Korogwe hususan Korogwe Mjini tuna Hospitali ya Magunga, lakini tuna kata mbili ambazo zipo mbali nje ya mji kabisa, Kata ya Kwamsisi na Kata ya Mgombezi ambazo zina vijiji kama sita sita. Je, Serikali itakuwa tayari kutusaidia kupata fedha kwa ajili ya kuwajengea vituo vya afya? (Makofi)
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru na nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Serikali ilikuwa bado haijaupa kipaumbele mradi huu na sasa wanasema walishaliweka katika vipaumbele vya kutekeleza mradi huu kama mradi kabambe wa umwagiliaji. Je, sasa Waziri atakuwa tayari kufuatana na Mbunge wa Jimbo ndugu yangu Stephen Ngonyani baada ya Bunge hili ili kwenda kuwaeleza wananchi wa Mkomazi kutokana na mradi huu kuwa unasuasua kwa muda mrefu?
La pili, kwa kuwa atakapokuwa anapita kwenda Mkomazi, kwa kuwa kauli mbiu ya Rais wetu mpendwa ni Hapa Kazi tu, je, atakuwa tayari kupita Korogwe Mjini kwenye mradi wa kwa Mgumi wa umwagiliaji ili aweze kwenda kuuona na hatimaye kuweza kuufanyia kazi kutokana na matatizo walionayo? (Makofi). Mheshimimiwa Spika, ahsante sana.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa elimu ya msingi ni kuanzia elimu ya awali kwa maana chekechea. Kutokana na kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya kupeleka fedha kwa kila kichwa cha mtoto kwenye elimu ya msingi, je, haioni sasa ni wakati muafaka wa kutoa fedha hata kwenye hii elimu kwa hawa watoto wa shule za awali ili kusudi ziweze kusaidia katika uendeshaji wa madarasa haya ya awali?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kwa kunipa nafasi. Naipongeza Serikali kwa kutupatia fedha Korogwe Girls za ukarabati wa shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati mbaya sana katika ukarabati ule bweni moja la Thabita limeshindikana kabisa kukarabatiwa kutokana na ubovu wa bweni lile.

Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutupatia fedha ili tuweze kujenga jengo hilo kutokana na watoto 120 kwenda kutawanywa kwenye mabweni mengine?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ili nami niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Korogwe Mji tulikuwa na kiwanda cha matunda na kama tunavyofahamu Mkoa wa Tanga una kilimo sana cha matunda. Kiwanda kile baada ya kubinafsishwa, yule mwekezaji ni miaka karibu 20 sasa kiwanda kile alishang’oa mashine zote na mabati yote yameshatolewa. Je, mtakuwa tayari sasa kutukabidhi eneo lile ili kusudi tuweze kuwawekea vijana shughuli za kufanya katika eneo lile?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Korogwe Mji tumekabidhiwa Hospitali ya Wilaya Magunga kutoka Korogwe Vijijini. Kwa bahati mbaya sana ina wodi moja tu ambayo wanalala wajawazito pamoja na wale waliojifungua. Je, Serikali itakuwa tayari kusaidia tupate fedha angalau tuweze kujenga wodi ya wajawazito na watoto?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kijiji cha Kitifu kipo Kata ya Mgombezi kimejenga zahanati na kimekamilisha, isipokuwa tu tunaomba mtusaidie majengo ya daktari pamoja na majengo mengine ambayo hayajakamilika. Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana, je, mtakuwa tayari kutusaidia angalau tuweze kupata fedha kwa ajili ya jengo la mganga?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru, naomba kuuliza swali la nyongeza, Korogwe Mji tuna kijiji kinaitwa Mahenge, kiko nje kabisa ya Mji wa Korogwe na katika mpango wa miji 28, sina hakika kama kinaweza kikafikiwa na ule mradi wa maji.

Je, mtakuwa tayari kukipatia maji kijiji hicho kwa kuwapa kisima cha maji kirefu?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Mgombezi ina zahanati na Kata ya Mtonga ina zahanati ambayo ina wakazi wengi, hasa ikizingatiwa kwamba, kuna mashamba ya mkonge. Je, watakuwa tayari sasa kutusaidia kupandisha hadhi Zahanati ya Mtonga pamoja na Zahanati ya Mgombezi ili viwe vituo vya afya, hasa ikizingatiwa kwamba, kuna watu wengi sana ambao wana shughuli za mkonge kule? Nashukuru sana.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza Mji wa Korogwe upo bondeni, mvua zote ambazo zinanyesha kuanzia vuli hadi sasa masika zimeendelea kuathiri sana miundombinu iliyopo kwenye mji ule. Na mara nyingi nikiiomba Serikali kwamba kama inawezekana ni vizuri tukatengewa fedha za kutosha ili tuweze kujenga mifereji ambayo itasaidia kupunguza kasi ya uharibifu wa barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, sasa mtakuwa tayari angalau kuweza kuwa mnatutengea fedha ziweze kujenga mifereji wakati tukiendelea kusubiri barabara za lami ambazo Serikali imeendelea kutupa angalau kwa kidogo kidogo ili kupunguza hata hiyo gharama ambayo kila mwaka mnatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara za changarawe, nashukuru sana. (Makofi)
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa majengo yanayotumika sasa hivi yana uchakavu mkubwa na ya muda mrefu, je, watakuwa tayari sasa angalau kuwapa fedha waweze kukarabati yale majengo ambayo yanatumika sasa hivi ikiwa ni pamoja na uzio?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, chuo kile kina uhaba wa watumishi wa kada ya ualimu watano pamoja na karani, mpiga chapa na mtu wa IT. Wizara itakuwa tayari kutusaidia angalau kuweza kupatikana hao walimu watano pamoja na hao watumishi wengine niliowataja?
MHE. MARY P. CHATANDA Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafas niulize swali la nyongeza. Nichukue nafasi hii kuishukuru Wizara ya Nishati kupitia Waziri, Naibu Waziri pamoja na watendaji wa TANESCO Mkoa na Wilaya ya Korogwe kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya sasa ya kuhakikisha kwamba vijiji vinapata umeme wa REA katika maeneo yale ambayo yalikuwa yamekosa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la nyongeza ni kwamba; kwa kuwa adha hii imekuwa ni ya muda mrefu na majibu aliyoyatoa Naibu Waziri ni mazuri, yanaridhisha:

Je, ni lini sasa ukarabati huu utakamilika? Maana unaweza ukasema unaendelea kukarabati, halafu inaweza ikawa mwaka mzima unafanyika ukarabati. Ni lini sasa watakamilisha ukarabati huu ili kusudi wananchi waondokane na adha hii ambayo wanaipata sasa? (Makofi)
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wakulima wanapata adha hii kubwa ya kununua mbolea kwa bei kubwa, kwa nini Serikali sasa isianzishe maduka haya ya pembejeo huko vijijini kupitia Mawakala ili kuwaletea unafuu wakulima kwa ajili ya ununuzi wa mbolea?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa napenda kuishukuru Serikali kwa namna ambavyo imekuwa ikitukimbilia pale shule yetu imekuwa na majanga ya moto zaidi ya mara mbili. Tunaishukuru sana Serikali.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili nishukuru kwa majibu mazuri niliyopewa na Waziri.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, katika huu mpango wa pili ambapo watakuwa wametafuta fedha, je, Shule ya Korongwe Girls itapewa kipaumbele cha kwanza hasa ikizingatiwa kwamba pia ina watoto wenye ulemavu ili walimu wale wawe na moyo wa kuendelea kufanya kazi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa tunazo shule za kata katika Halmashauri zetu kwa nchi nzima ambapo tulikuwa tumeweka mipango kwa ajili ya ujenzi wa maabara lakini kwa bahati mbaya sana Halmashauri nyingine zimeshindwa kukamilisha mahabara hizo. Je, mtakuwa tayari sasa kuweka mpango wa kukamilisha zile maabara zilizoko kwenye Halmshauri zetu ili watoto waweze kupata elimu iliyo bora kuliko bora elimu?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona, pamoja na majibu mazuri ya kwenye swali la msingi la Naibu Waziri, Wilaya ya Korogwe ina Halmashauri mbili ambapo Polisi wanakaa kwenye jengo la mkoloni ambalo Mkuu wa Wilaya yumo, Mahakama imo na hiyo Polisi ipo hapo.

Je, katika mipango ambayo wanakusudia sasa kuanza baadaye atakuwa tayari kuipa kipaumbele Korogwe ili wawe na jengo la ofisi kwa sababu kiwanja wanacho?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Gereza la Kwa Mngumi lililopo Korogwe linafanya shughuli za kilimo pamoja na mabwawa ya samaki na kwa bahati nzuri Naibu Waziri umeshafika pale tukushukuru kwa kuwasaidia mashine zile za kufyatulia tofali. Je, sasa mtakuwa na mpango wa kuweza kuwasaidia kuwawezesha ili waweze kupanua yale mabwawa pamoja na kilimo kama ambavyo mnaelekeza kwamba magerea waweze kujitegemea katika uzalishaji?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze Serikali kwa kufanya ukarabati wa reli Tanga - Korogwe - Mombo na Mazinde na kuendelea. Nilikuwa nataka kujua kwenye maeneo yale ya reli kuna nyumba za Serikali ambazo zilikuwa zimejengwa kwa ajili ya watumishi ambao walikuwa wanaishi katika maeneo yale. Sasa katika ukarabati huu wa reli, je, mko tayari sasa kuzikarabati nyumba zile ili kusudi wale wafanyakazi waendelee kukaa kwenye zile nyumba kwa kusaidia kulinda mataruma yale yasiendelee kuibiwa?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza niwapongeze wenzetu wa TARURA kwa kazi nzuri wanazofanya pale Korogwe ajili ya ujenzi wa zile barabara kwa kiwango cha lami na kiwango cha changarawe. Nina swali la nyongeza.

Kwa kuwa mnawapa fedha kwa ajili ya ujenzi wa zile barabara za changarawe na Mji wa Korogwe umekaa bondeni, mvua zikinyesha kama hivi sasa barabara zile zote zinasombwa na maji.

Je, Serikali itakuwa tayari sasa mnapotupa fedha hizo kutuwekea na fedha za kujenga mifereji ili kusudi ziweze kuhimili hizo barabara kwa muda mrefu?
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Wizara ya Ujenzi kupitia TANROAD wamekuwa wakifanya kazi ya kuweka alama za X kwenye maeneo ambayo wanakusudia kufanya upanuzi wa barabara, lakini kazi hiyo ambayo wamekuwa wakiifanya hawawahusishi wananchi wa maeneo husika kwa kuwaarifu kwamba wanakusudia kufanya hivyo, watu wanawaona tu wanaweka alama za X. Je, kwa nini wanafanya kazi hiyo bila kuwahusisha wananchi ili waweze kuwafahamu na kuondoa taharuki ambazo zinajitokeza katika kuwekewa alama za X? (Makofi)

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's