Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kutujaalia afya na leo tuko hapa mbele yake tukisikiliza mambo mbalimbali. Nianze kwa kuipongeza Kamati kwa maazimio mbalimbali ambayo yamewasilishwa kwetu. Sisi kama Serikali maazimio haya tunayachukua kwa ajili ya kwenda kuyafanyia kazi na kuyachakata kwa namna yoyote ile ili kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo machache ambayo yamezungumzwa na Waheshimiwa Wabunge na kwa kweli kwa upande wa Wizara yetu Wabunge wengi wamechangia na sehemu kubwa sana walijikita kwenye hii migogoro ya adhi, fidia lakini pia mpango wa maboresho ya matumizi bora ya ardhi kwenye vijiji. Mambo yote haya na ushauri wote walioutoa sisi kama Serikali tunayapokea na tunakwenda kuyachakata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kama Wizara kwenye suala la mabaraza ya ardhi, sasa hivi tunaendelea na mchakato ambao, ili kukamilisha ile idadi ya wilaya tulizonazo ya kuajiri wale wenye viti wa mabaraza. Muda mfupi ujao tunaweza kabisa wilaya zote zikawa zimepata watendaji ambao watakwenda kutusaidia kupunguza hasa umbali kutoka wilaya moja mpaka wilaya nyingine, kwa mfano mtu wa Dodoma hapa tumempa mpaka Kiteto kule unakuta wakati mwingine tunakuwa na limbikizo la kesi ambazo zingetakiwa zitatuliwe kwa muda mfupi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ni imani yangu kwamba wakati ujao tutakapokuwa tunatoa taarifa ya utekelezaji tutakuwa tunawafikisha kwenye kuondoa kiu hii hasa kwenye upande wa mabaraza. Ninaomba mtupe nafasi ili tuweze kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kubuni na kutekeleza mipango mbalimbali ya kupunguza migogoro ya ardhi naomba niwape comfort Waheshimiwa Wabunge, kwamba Wizara imejipanga na kama Wabunge walivyosema asubuhi, tuna timu mbalimbali zinazotafiti kwa nini kuna migogoro mingi hapa nchini na nini asili yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi tu unaweza ukaona migogoro hii ina sura kama mpaka tatu hivi. Iko sura ile ambayo ni wananchi wenyewe kugombania maeneo yao kwa mipaka ile isiyotambuliwa. Tunayo mashamba makubwa makubwa ambayo wananchi wanaoonekana wamekaa katika maeneo yale uasili wao ni kwamba wana historia ambazo haziwezi zikabadili uwepo wao pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano mashamba makubwa watu walichukuliwa kutoka sehemu mbalimbali kwenda kuongeza nguvu za uzalishaji kwenye yale mashamba. Hili nalo tumelipokea na tunalifanyia kazi kwa haraka ili kuangalia. Case study moja ni Mkoa wa Manyara ambao wananchi wake wengi ambao wanagombana na wale wawekezaji sehemu kubwa sana wana asili ya uwepo wao pale kwa sababu wazazi wao ambao walichukuliwa kutoka maeneo mbalimbali waliletwa na hao wenye mashamba na sasa hivi inaonekana ni tatizo na ni kadhia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunafanya nao kazi na nimekutana na wawekezaji wa mashamba makubwa takriban Mkoa mzima wa Manyara. Tumekubaliana na wengi wameanza kukubaliana kwamba okay tatizo the way lilivyo iko haja sasa ya kuangalia upya namna ya kuachia maeneo mengine ambayo hawa Watanzania wanaweza wakaendelea kuyatumia kwa namna yoyote ile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hili suala la mipango ya kutatua migogoro tunaendelea nalo. Tunatengeneza mifumo ambayo baada ya muda kama mlivyosikia kwenye taarifa ya Kamati, tuko zaidi ya asilimia 80 katika kuanza kufanya majaribio ya kutumia TEHAMA katika process nzima ya mtu anapotafuta kiwanja. Kwa sasa hivi bado tunabeba mafaili mkononi, na hiyo imesababisha matatizo mengi sana. Matatizo mengi ya katikati ya miji ambayo tayari imeshapimwa siyo kwamba inahitaji kupimwa upya. Kule ku-move kwa njia ya mkono bila kutumia mitandao hii mara nyingi imesababisha vitu vingi kuwa na mambo ya double allocation bila sababu za msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa dawa inachemka; niwaombe tu Waheshimiwa nadhani mpaka kufikia Bunge linalokuja tutakuwa tunatoa taarifa ya utekelezaji. Wengine mtakuwa mnaona kwenye mitandao yenu kupitia simu zenu jinsi mnavyopewa ripoti ya maeneo ambayo mnayamiliki kihalali. Kwa hiyo, niwaombe tuwe na muda wa kutosha ambao tutakwenda kuleta matokeo zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nizungumzie kwa ufupi sana kuhusu susala la maboresho ya mipango ya matumizi bora ya ardhi ya vijiji. Waheshimiwa Wabunge niwaambie, mpaka kufikia 2024 hapo tutakuwa tayari tumeshapima vijiji 5,000 na vijiji 5,000 ni karibu nusu ya safari ya vijiji vyote vya Tanzania. Kwa hiyo, naomba tu kwa sababu fedha zile ambazo zimeombwa kutoka kwenye mifuko mbalimbli, tunazo fedha zinazotegemewa kutoka kwenye halmashauri kama mtakumbuka Bunge lililopita na tuna fedha ambazo tunazitenga kwenye bajeti yetu ya kila siku. Kwenye huu mfuko ambao unatokana na mfuko wa World Bank tayari kwa sababu bajeti ya kwanza ilikuwa inasema tutenge bajeti ya shilingi bilioni saba; lakini nataka niwakikishie mpaka sasa tumeshatenga shilingi bilioni 21 katika zoezi hili na tunakwenda kupima vijiji zaidi ya 1,600.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotokea hapa katika tofauti ya utekelezaji; Tume hii iko chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Utendaji kazi wake ni wa pamoja wala siyo kwa kutenganisha. Mradi kama huu wa World Bank una masharti magumu sana katika kutoa fedha yake kuihamisha kuipeleka Tume. Kwa hiyo, hizi shilingi bilioni 21 zinasimamiwa na Wizara yetu chini ya fungu la Wizara lakini watendaji ni wale wanaotoka kwenye tume kwenda kutekeleza yale majukumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Waheshimiwa Wabunge ni kweli mnaweza msizione fedha kwenye account za tume lakini tume tunai-facilitate kwa asilimia 100; na mpaka sasa hivi maafisa wengi kutoka kwenye ile tume wako uwandani na wanaendelea na kazi, hatujakwama mahali popote. Kwa hiyo, niwaombe tu kwamba ni mambo ambayo yanatekelezeka kwa utaratibu wa kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ongezeko la fedha. Mkopo huu ulikuwa na mambo mengi, na moja ya eneo lake ilikuwa ni kufanya mamboresho kwenye maeneo ya utawala wa Wizara. Niwakikishie Waheshimiwa Wabunge, mikoa yote inaenda kupata majengo kwa ajili ya maafisa wetu. Najua mnajua wanavyohangaika kwenye halmashauri kule, wanavyojibana kwenye vyumba vidogo vidogo. Tunakwenda kujenga ofisi za mikoa yote. Mikataba tayari imeshasainiwa ya kubaini wale wakandarasi. Tunakwenda vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na eneo hili vile vile tunakwenda kuanzisha ofisi za ardhi za wilaya ambazo kwa miaka yote hazijawahi kutokea. Kwa hiyo, kumekuwa na miss communication. Kumekuwa na mtengano wa kimawasiliano kati ya maafisa wetu ambao tumewa-attach kwenye halmashauri ambao wako chini ya Wizara yetu na kamishna wa mkoa; unakuta load ya kamishna wa mkoa ni kubwa. Tunakwenda kuwa na makamishna wasaidizi wa wilaya ili waweze kusimamia zile halmashauri zilizoko chini ya Wizara zao. Hii itatusaidia sana kutusogeza karibu na huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wengi wamezungumzia masuala ya mabadiliko ya sheria na sera. Wizara iko kwenye mchakato na sera ilishakwenda mpaka kwenye Baraza la Mawaziri. Sasa Waheshimiwa Wabunge tukae mkao wa kuipokea huku Bungeni kwa ajili ya kuipitia, lakini iko mwishoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuliabaini kwamba sera ile ni ya muda mrefu na ina mapungufu. Kwa hiyo, yale mapungufu yote mliyoyaona ninyi na kushauri, ushauri wenu wote tumeuweka kwenye haya mapendekezo ya sera mpya ambayo inakuja. Niwaombe tu kwa ujumla wake. Kwanza napokea shukrani nzote napongezi zote mlizozipeleka kwa Mheshimiwa Waziri na Wizara yake, na mimi nitamfikishia; lakini pongezi zote zilizotolewa kwa Serikali nzima kwa maana ya Mheshimiwa Rais pamoja na watendaji wake wote tuliopo. Tunashukuru sana kwa hizo shukrani ambazo kweli mnatambua mchango ambao unatolewa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Niwaombe tujipe muda kuhusiana na mambo haya. The way tunavyokwenda tunakwenda katika michakato tofautitofauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo moja ambalo ningependa niwambiwa Watanzania wote ardhi ya Tanzania kwa ukubwa wake haina nyongeza nyingine yoyote tulikuwa nayo Mwaka 1953, tukawa nayo Mwaka 1960, tunayo Mwaka 1970 na tunayo 2024, haitaongezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kupitia hilo sisi Watanzania Mwaka 1950 tulikuwa chini milioni tisa, leo tunapozungumza tuko milioni 61. Hekima ituongoze katika kupitia haya mambo ambayo yanaihusu ardhi. Ongezeko letu ni sababu nyingine ya msingi kabisa ya ongezeko la kusukumana sukumana katika maeneo yetu. Nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge na nawashukuru kwa jinsi ambavyo mnatupa mawazo jinsi ya kukabili ongezeko la watu bila ongezeko la ardhi, ahsante sana Mungu awabariki sana.