Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Contributions
nil
Answers
nil
Commettees
1
Ministries
nil
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naomba kuongezea mchango wangu wa kuzungumza nikianza na TBA; nawapongeza kwa kazi kubwa wanazofanya, lakini naomba Mradi wa Temeke Mwisho utengewe fedha na ukamilike.
Mheshimiwa Spika, Temeke ni Wilaya ambayo hakuna nyumba nyingi za watumishi, hivyo tunatamani kuona nyumba zile zimekamilika. Rai yangu pamoja na juhudi za Serikali za kutafuta sekta binafsi kuungana na TBA, lakini wasitupandishie gharama za nyumba kwa kuwa mara nyingi sekta binafsi wanaangalia faida zaidi bila kujali hali za wananchi wetu/watumishi wetu.
Mheshimiwa Spika, ndani ya mradi wa ujenzi wa nyumba za TBA kuna Shule ya Msingi Mji Mpya ambayo ina mazingira magumu sana, haiwezi kuendelezwa, je, Serikali hawaoni umuhimu wa kusaidia kuendeleza shule hiyo kama sehemu ya mradi huo? Kwa sababu watakaokuja kuishi pale nao watakuwa na familia zao.
Mheshimiwa Spika, ninaunga mkono hoja.