Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

Hon. Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, mara kadhaa nimeiomba Serikali kupitia upya madai ya wananchi waliopisha ujenzi wa Barabara ya Bunda kwenda Kisorya, kwani baadhi ya wananchi wanadai kuwa bado hawajalipwa fidia zao. Naiomba Serikali kupitia bajeti ya mwaka huu wa 2025 iwalipe wananchi hao stahili zao.

Mheshimiwa Spika, mawasiliano ya usafiri kati ya Visiwa vya Nafuba, Sozia, Nyamuguma, Machwela na Buyanza ni changamoto kubwa sana kwa wananchi. Naiomba Serikali ivipatie kivuko visiwa hivi.