Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwibara
Contributions
nil
Answers
nil
Commettees
1
Ministries
nil
MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, mara kadhaa nimeiomba Serikali kupitia upya madai ya wananchi waliopisha ujenzi wa Barabara ya Bunda kwenda Kisorya, kwani baadhi ya wananchi wanadai kuwa bado hawajalipwa fidia zao. Naiomba Serikali kupitia bajeti ya mwaka huu wa 2025 iwalipe wananchi hao stahili zao.
Mheshimiwa Spika, mawasiliano ya usafiri kati ya Visiwa vya Nafuba, Sozia, Nyamuguma, Machwela na Buyanza ni changamoto kubwa sana kwa wananchi. Naiomba Serikali ivipatie kivuko visiwa hivi.