Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Biharamulo Magharibi
Contributions
nil
Answers
nil
Commettees
0
Ministries
nil
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa bahati mbaya hatukuweza kuona performance report ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha tulionao. Endapo ningepata fursa ya kuona ripoti hiyo, kungekuwa na fursa ya kusema yafuatayo kwa takwimu zaidi. Kuna dalili nzuri kwenye viashiria vya uchumi mkubwa (macro economic indicators), lakini kuna kila dalili kuwa tunaporomoka kwenye micro economic indicators.
Mheshimiwa Naibu Spika, maoni yangu ni kwamba mpango wa 2017/2018 pia hauonekani kuzingatia upungufu huu. Mfano, tungeweka nguvu kubwa kwenye viwanda vya kiwango (size) ya kati badala ya vikubwa ingekuwa rahisi kuweka kichocheo kwa sekta ya kilimo kwenye mikoa tofauti tofauti kwa kuzingatia zao la kilimo linalopatikana eneo husika. Tuwe na mtiririko (sequence) sahihi wa nini cha kufanya. Kilimo kifunganishwe na upatikanaji wa umeme na maji, soko la ndani ya Tanzania na soko la Afrika Mashariki litatosha kwa awamu hiyo ya kwanza. Hii pia itaongeza wigo wa walipa kodi, miundombinu (ndege, meli, reli) ili kutanua soko nje ya Tanzania na Afrika Mashariki.