Primary Questions from Hon. Mary Francis Masanja (3 total)
MHE. NG'WASI D. KAMANI K.n.y MHE. MARY F. MASANJA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Nhungumalwa – Ngudu mpaka Magu kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Nhungumalwa – Ngudu yenye urefu wa kilometa 71 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, jumla ya mita 500 pamoja na roundabout zilijengwa katika eneo la Isandula. Aidha, mkataba wa ujenzi kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya kuanzia Magu hadi Ngudu yenye urefu wa kilomita 10 umesainiwa mwezi Mei, 2024 na kwa sasa mkandarasi yupo katika maandalizi ya kuanza ujenzi. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na kazi za ujenzi, ahsante.
MHE. NG'WASI D. KAMANI K.n.y MHE. MARY F. MASANJA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Nhungumalwa – Ngudu mpaka Magu kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Nhungumalwa – Ngudu yenye urefu wa kilometa 71 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, jumla ya mita 500 pamoja na roundabout zilijengwa katika eneo la Isandula. Aidha, mkataba wa ujenzi kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya kuanzia Magu hadi Ngudu yenye urefu wa kilomita 10 umesainiwa mwezi Mei, 2024 na kwa sasa mkandarasi yupo katika maandalizi ya kuanza ujenzi. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na kazi za ujenzi, ahsante.
MHE. MARY F. MASANJA aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka Gari la Wagonjwa na Watumishi Kituo cha Afya Budushi Wilayani Kwimba?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuajiri watumishi wa Kada ya Afya na kuwapeleka kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Katika mwaka wa fedha 2024/2025 jumla ya watumishi 9,384 waliajiriwa na kupangiwa kazi katika vituo vya kutolea huduma katika halmashauri, ambapo jumla ya watumishi 32 wa afya walipangwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba. Kituo cha Afya Budushi kina jumla ya watumishi 12.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 ilinunua magari 594, ambulances 382 na magari ya usimamizi wa huduma za afya 212, katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba imepokea magari matatu ya kubebea wagonjwa na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba, Kituo cha Afya Malya na Kituo cha Afya Kadashi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa dharura zinazotokea kwenye Kituo cha Afya Budushi zinahudumiwa na gari la kubebea wagonjwa lililopo Hospitali ya Sumve (VAH), ambayo ipo umbali wa kilomita moja. Serikali itaendelea kutenga bajeti, kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa na kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya nchini.