MHE. MARY F. MASANJA: Mheshimiwa Spika, Je, ni lini Serikali itaharakisha kuligawa Jimbo la Magu kuwa Majimbo mawili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ugawaji wa Majimbo unafanywa na Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, pamoja na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuwa ni sehemu ya wadau.
Mheshimiwa Spika, naomba nipokee hoja ya Mheshimiwa Mbunge Mary Masanja na tutaiwasilisha Serikalini ili vigezo hivyo viweze kuzingatiwa na hatua stahiki ziweze kuchukuliwa, ahsante.
MHE. MARY F. MASANJA: Mheshimiwa Spika, ni lini Barabara ya kutoka Nhungumalwa - Ngudu hadi Magu itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, barabara aliyoitaja, ambayo tutaanza kujenga kilometa 10, tayari ilishatangazwa na sasa hivi tuko kwenye hatua za manunuzi. Ahsante.