Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 42 Information, Culture, Arts and Sports Maswali kwa Waziri Mkuu 4 2024-06-06

Name

Shabani Hamisi Taletale

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante na mimi kupata nafasi ya kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, michezo ya kubashiri imekuwa ikichangia Pato la Taifa, lakini mapato ya michezo hii yamekuwa hayanufaishi moja kwa moja sekta ya michezo kutokana na michezo hii kusimamiwa na Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, je, Serikali haioni haja ya kuihamisha michezo hii kutoka kwenye Wizara ya Fedha kuipeleka kwenye Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taletale, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upo ukweli kwamba tunayo michezo ya kubahatisha na kubashiri michezo ambayo inaratibiwa na Bodi ya Bahati Nasibu na makampuni haya yanayoendesha ubashiri wa michezo wanalipa kodi na kwa mujibu wa sheria zetu nchini kodi zote huwa zinapewa mamlaka inayokusanya kodi ambayo huwa ni TRA.

Mheshimiwa Spika, sasa Mheshimiwa Mbunge anataka kusema kwa nini kibali hiki kisipewe Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuweza kuendeleza michezo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli hii Bodi ya Michezo ya Kubahatisha iko Wizara ya Fedha na anayekusanya mapato ni TRA kama ambavyo kodi zingine zinavyokusanywa na TRA, lakini baada ya kukusanya fedha hii Baraza la Michezo lililoko ndani ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo linapata mgao wa 5% ya makusanyo ya fedha kutoka kwenye michezo hii ya kubahatisha na kwa hiyo suala la uendelezaji wa michezo linabaki pale pale, kwa sababu hiyo 5% ndiyo inayotakiwa kukusanywa na hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo lengo la kuipa TRA kukusanya mapato ni katika kudhibiti mianya ya fedha katika kuweka uelewa wa taasisi husika ya ukusanyaji kodi ambao pia ni TRA na mamlaka ambayo imepewa na kwa hiyo sasa tuna uhakika kila ikikusanya tukishapata takwimu 5% tunapeleka kwenye mfuko wa kuendeleza michezo ulioko chini ya Baraza la Michezo kwa ajili ya shughuli za michezo na ndiyo utaratibu ambao kwa sasa unaendelea.

Mheshimiwa Spika, pia kama wadau wa michezo wataona kuna haja ya kuishauri Serikali, sisi tunapokea ushauri na kupitia vikao vyetu tutabadilisha kanuni na sheria zetu ili tuelekeze huko kama umuhimu upo kwa ajili ya kuendeleza michezo kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameeleza, nakushukuru sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister