Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 80 2024-02-05

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: -

Je, lini Serikali itatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kumalizia Mradi wa Maji wa Mageri utakaohudumia vijiji nane Wilayani Ngorongoro?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Lekishon Shangai, Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitenga fedha za utekelezaji wa Mradi wa Maji Mageri utakaohudumia vijiji nane vya Tinaga, Oloirien, Ng’arwa, Yasi, Mdito, Mageri, Mugongo na Magaiduru, ambapo hadi sasa jumla ya shilingi 2,264,520,000 zimetolewa. Fedha hizo zimesaidia kukamilisha utekelezaji wa Banio la Chanzo cha Maji Orkanjor, ulazaji wa bomba kuu kutoka kwenye chanzo hadi kwenye tenki umbali wa kilometa tatu na ununuzi wa pampu mbili zenye uwezo wa kusukuma maji lita milioni 2.05 kwa Siku. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zinazoendelea kwa sasa ni pamoja na ujenzi wa matenki tisa yenye jumla ya ujazo wa lita 2,000,000 na uchimbaji wa mitaro na ulazaji wa mabomba ya usambazaji umbali wa kilometa 80. Aidha, utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa asilimia 40 na unatarajiwa kukamilika mwezi Disemba, 2024. (Makofi)