Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 138 2024-02-09

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Mahaya – Singida?

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Immanuel Elibariki Kingu, Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ambayo Jimbo la Singida Magharibi lipo imetengewa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule za msingi. Aidha, Shilingi milioni 595.6 zimetumika kujenga shule mpya moja na vyumba vya madarasa vinne katika shule mbili za msingi katika Jimbo la Singida Magharibi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Msingi Mayaha imetengewa bajeti kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mawili kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Serikali itaendelea kuongeza madarasa katika shule hii kulingana na upatikanaji wa fedha.