Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 43 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 561 2024-06-07

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je, Serikali ipo tayari kuleta wataalamu Liwale kufanya utafiti kujua chanzo cha ugonjwa wa majani ya mikorosho kunyauka? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari imeanza kufanya utafiti wa kina ili kutambua chanzo cha ugonjwa majani kunyauka unaoikumba mikorosho katika Wilaya ya Liwale. Utafiti huo ulianza kufanyika mwaka 2023 na wataalamu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania kupitia Kituo cha TARI Naliendele kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, matokeo ya awali ya utafiti huo yamebaini kuwa chanzo cha mnyauko wa majani ya mikorosho katika Wilaya ya Liwale ni fangasi aina ya Fusarium oxysporum f. sp na ikajulikana kuwa ni kimelea kinachoishi kwenye udongo ambacho husababisha ugonjwa wa mnyauko fusari (fusarium wilt) na ugonjwa huu ni tishio kwa kuwa unasababisha kukauka kwa mikorosho. Serikali imeanza kutoa elimu kwa wakulima na wataalamu wa kilimo kuhusu mbinu za awali za kukabiliana na ugonjwa huo. (Makofi)