Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 195 2024-04-29

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani kuimarisha shughuli za TCU Zanzibar ili kupunguza usumbufu kwa wadau wa elimu Zanzibar?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inatekeleza majukumu yake yote katika pande zote mbili za Muungano. Majukumu hayo yanahusisha utoaji wa mafunzo kwa Viongozi na Wahadhiri wa Vyuo Vikuu vilivyopo Tanzania Bara na Zanzibar kuhusu masuala ya elimu ya chuo kikuu, ikiwemo Uongozi na Usimamizi wa Vyuo Vikuu, Uandaaji wa Mitaala inayokidhi mahitaji ya soko, Mbinu Bora za Ufundishaji na Uthibiti Ubora wa Elimu ya Juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano, katika kipindi cha Juni, 2023 hadi Machi, 2024 viongozi na wahadhiri 48 kutoka vyuo vikuu vitatu vilivyopo Zanzibar wamepata mafunzo yaliyojumuisha viongozi na wahadhiri kutoka vyuo vikuu na vyuo vikuu vishiriki 49 vilivyosajiliwa chini ya TCU.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TCU kila mwaka hufanya tathmini ya utekelezaji wa majukumu yake. Kutokana na tathmini hiyo, mikakati ya uboreshaji huwekwa kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya TCU katika pande zote za Tanzania Bara na Zanzibar.