Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 196 2024-04-29

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: -

Je, Chuo cha Utalii Dar es Salaam na Vyuo vingine vya utalii vimetoa wafanyakazi wangapi ngazi ya Menejimenti katika Hoteli za Serengeti na Ngorongoro?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro zipo hoteli zinazotoa huduma za malazi za kudumu 13. Kati ya hizo, 12 zimeajiri Mameneja wazawa na moja imeajiri Meneja ambaye ni raia wa kigeni. Kwa upande wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, kati ya hoteli 31 zinazotoa huduma za malazi za kudumu 22 zimeajiri Mameneja wazawa na tisa zimeajiri baadhi ya Mameneja ambao ni raia wa kigeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) kinatoa mafunzo katika ngazi ya Cheti na Diploma ambayo yanawezesha wahitimu wengi kuajiriwa katika kada ya utendaji na baadhi katika kada za usimamizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kwa kuwa Chuo cha Taifa cha Utalii kwa sasa hakitoi mafunzo kwa ngazi ya shahada na kimekuwa na changamoto ya kutoa wafanyakazi katika ngazi ya menejimenti kwenye hoteli, kwa hali hiyo, hoteli nyingi zinazotoa huduma za malazi zimeajiri Watanzania katika ngazi ya menejimenti waliomaliza kozi za utalii katika vyuo vingine nchini ikiwemo Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine na Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino.