Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 201 2024-04-29

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza:-

Je, lini Serikali itamaliza mgogoro wa ardhi wa Rwanyabara baina ya mwekezaji na wananchi wa Kijiji cha Bushasha Bukoba Vijijini?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2008, uongozi wa Kijiji cha Bushasha kilichopo katika Wilaya ya Bukoba uligawa ardhi yenye ukubwa wa ekari 242 kwa wawekezaji ambao ni Ndugu Deusdelt Rwehabura na Kampuni ya Kagera Tea Company Limited.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia hatua hiyo, familia ya Ndugu Sosthenes Ntagalinda Kajwahula ilifungua Shauri Na. 104/2008 katika Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya Bukoba dhidi ya Halmashauri ya Kijiji cha Bushasha ikidai ardhi iliyogawiwa kwa wawekezaji hao ni yao. Tarehe 20 Desemba, 2015, shauri hilo liliamuliwa ambapo familia ya Ndugu Ntagalinda ilipata tuzo ya kuwa wamiliki halali wa ardhi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia uamuzi huo wa Baraza, wananchi waliokuwemo ndani ya eneo hilo wameendelea kulalamika kwenye ngazi mbalimbali za Serikali, hivyo uongozi wa ngazi ya Mkoa na Wilaya umeanza taratibu za kuzikutanisha pande husika kwa ajili ya suluhisho la ardhi hiyo nje ya mfumo wa Mahakama. Natoa rai kwa wananchi waliopo katika eneo hilo kuwa na subira wakati Serikali ikitafuta njia nyingine ya kumaliza mgogoro uliopo.