Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 45 Water and Irrigation Wizara ya Maji 583 2024-06-11

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kuanzisha Mamlaka ya Maji Mkoa wa Pwani ili kuondoa changamoto ya maji maeneo mengi ya mkoa huo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya huduma majisafi na salama katika Mkoa wa Pwani ni wastani wa 79.8% kwa vijijini na 90% kwa mijini ambapo huduma hiyo inatolewa kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kwa upande wa vijijini na kwa maeneo ya mijini huduma hiyo inatolewa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali inaridhishwa na taasisi zinazotoa huduma ya majisafi na salama katika Mkoa wa Pwani ambapo maeneo yote ya mijini yanapata huduma za maji safi kwa viwango mbalimbali. Hata hivyo, Serikali ipo tayari kufanya mabadiliko yoyote yanayolenga kuboresha eneo la utoaji huduma ya maji katika Mkoa wa Pwani pindi itakapoonekana inafaa. (Makofi)