Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 45 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 588 2024-06-11

Name

Tamima Haji Abass

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza:-

Je, lini Serikali itatunga sheria mahsusi kwa makosa ya ukatili wa kijinsia?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuombe radhi, swali namba 589 ndilo nipo nalo hapa, bahati mbaya niruhusu nilipate jibu la swali hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sheria ya Ndoa, Sheria ya Mtoto, Sheria ya Makosa ya Mtandao na Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu zina vifungu vinavyozuia makosa ya ukatili wa kijinsia na vifungu vinavyohusika na makosa ya ukatili wa kijinsia. Hata hivyo, Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Wizara nyingine na asasi za kiraia inafanya tathmini ili kubaini iwapo ipo haja ya kuwa na sheria mahususi ya ukatili wa kijinsia au tuboreshe sheria zilizopo. Tathmini hiyo ikikamilika, itasaidia Serikali kufanya uamuzi sahihi kuhusu suala la kutunga sheria mahususi kwa makosa ya ukatili wa kijinsia au kuboresha sheria zilizopo, ahsante.