Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 188 | 2025-04-30 |
Name
Robert Chacha Maboto
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bunda Mjini
Primary Question
MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Makao Makuu ya TANAPA katika Halmashauri ya Mji wa Bunda?
Name
Dunstan Luka Kitandula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkinga
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imetenga eneo lenye ukubwa wa ekari 41.13 katika eneo la Kunzugu, Kata ya Balili, Mjini Bunda kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za TANAPA Kanda ya Magharibi. Kwa sasa, Serikali imekamilisha zoezi la upembuzi yakinifu na uandaaji wa michoro kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hiyo. Kazi ya ujenzi inatarajiwa kuanza kwenye Mwaka wa Fedhaa 2025/2026.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved