Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 499 2025-06-04

Name

Amb. Liberata Rutageruka Mulamula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. BALOZI LIBERATA R. MULAMULA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuanza ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya kimkakati ya Kyazi Kayanga – Missenyi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kujenga Barabara ya Kyazi Kayanga – Missenyi kwa kiwango cha lami ili kuboresha usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Kata za Bwanjai, Kitobo, Bugandika na maeneo jirani. Hivyo, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuifanyia usanifu na kupata gharama za kuijenga kwa kiwango cha lami. Pindi gharama za ujenzi kwa kiwango cha lami zikijulikana, Serikali itaanza ujenzi huo kwa bajeti zinazofuata.

Mheshimiwa Spika, katika kuiwezesha barabara hiyo kupitika na kurahisisha usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa kata hizo, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali imetenga shilingi milioni 59 kwa ajili ya kuifanyia matengenezo.