Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 499 | 2025-06-04 |
Name
Amb. Liberata Rutageruka Mulamula
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Nominated
Primary Question
MHE. BALOZI LIBERATA R. MULAMULA aliuliza: -
Je, kuna mpango gani wa kuanza ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya kimkakati ya Kyazi Kayanga – Missenyi?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kujenga Barabara ya Kyazi Kayanga – Missenyi kwa kiwango cha lami ili kuboresha usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Kata za Bwanjai, Kitobo, Bugandika na maeneo jirani. Hivyo, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuifanyia usanifu na kupata gharama za kuijenga kwa kiwango cha lami. Pindi gharama za ujenzi kwa kiwango cha lami zikijulikana, Serikali itaanza ujenzi huo kwa bajeti zinazofuata.
Mheshimiwa Spika, katika kuiwezesha barabara hiyo kupitika na kurahisisha usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa kata hizo, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali imetenga shilingi milioni 59 kwa ajili ya kuifanyia matengenezo.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved