Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 500 | 2025-06-04 |
Name
Aida Joseph Khenani
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Nkasi Kaskazini
Primary Question
MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -
Je, nini sababu ya Wilaya ya Nkasi kukosa miradi ya kimkakati?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) aliuliza: -
Mheshimiwa Spika, Serikali ilianzisha utaratibu wa kutekeleza miradi ya kimkakati katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuziwezesha halmashauri kuongeza mapato ya ndani na kuboresha huduma za kijamii na kiuchumi.
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya Nkasi iliibua na kuandaa maandiko ya miradi miwili ya kimkakati ya kuboresha minada mitatu ya kisasa na ujenzi wa hoteli ya kisasa katika Mji wa Namanyere. Maandiko hayo yaliwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI mwezi Julai, 2020 kwa ajili ya uchambuzi. Aidha, miradi hii ilikosa baadhi ya vigezo ikiwemo umiliki wa ardhi ya maeneo ya miradi na kutofanyika kwa upembuzi yakinifu wa miradi husika.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa halmashauri ipo katika hatua za mwisho za ukamilishaji wa vigezo vilivyokosekana wakati wa uchambuzi. Mara baada ya hatua hiyo kukamilika na miradi kukidhi vigezo, Serikali itatafuta fedha na kuanza utekelezaji wa miradi hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved