Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 503 | 2025-06-04 |
Name
Innocent Sebba Bilakwate
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kyerwa
Primary Question
MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka gari la polisi na gari la zimamoto katika Wilaya ya Kyerwa inayopakana na nchi mbili ili kukabiliana na majanga ya moto?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ahsante, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imepeleka gari jipya moja aina ya Toyota Land Cruiser Pickup kwa Polisi Wilaya ya Kyerwa. Aidha, kwa upande wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Serikali itapeleka gari moja katika wilaya hiyo ikiwa ni mpango wa Serikali wa kusambaza magari ya zimamoto na uokoaji kwa wilaya zote nchini kwa ajili ya kukabiliana na majanga ya moto, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved