Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 505 | 2025-06-04 |
Name
Joseph Zacharius Kamonga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ludewa
Primary Question
MHE. NEEMA W. MGAYA K.n.y. MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -
Je, jitihada zipi zinafanywa na Serikali kuhakikisha Wilaya ya Ludewa inajengewa miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ahsante, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umwagiliaji katika Wilaya ya Ludewa ikiwemo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Skimu za Umwagiliaji za Mbwila hekta 4,000, Iselela hekta 1,800 na Bonde la Mto Ruhuhu lenye ukubwa wa hekta 4,500. Upembuzi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2025 na kuanza taratibu za kumpata mkandarasi kwa ajili ya ujenzi. Aidha, Tume inaendelea na uchimbaji wa kisima cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mangalanyene chenye uwezo wa kumwagilia ekari 123. Kisima hicho kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kunufaisha wakulima 80 wa zao la chai.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved