Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 506 | 2025-06-04 |
Name
Grace Victor Tendega
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:
Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha uvunaji wa maji ya mvua unapunguza changamoto ya maji?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Serikali inaendelea kutekeleza mkakati wa uvunaji wa maji ya mvua wa miaka mitano kuanzia mwaka 2022 hadi 2026 kwa kujenga mabwawa kwa lengo la kukabiliana na changamoto za mafuriko na ukame. Pia utekelezaji unaendelea wa mkakati wa uvunaji wa maji ya mvua kandokando ya barabara kwa miaka mitano kuanzia mwaka 2020 hadi 2025 kwa kujenga malambo ambao uliandaliwa mahususi kwa ajili ya kulinda miundombinu ya barabara na reli. Kupitia mikakati hiyo, jumla ya mabwawa 45 yamejengwa katika kipindi cha mwaka 2022 hadi 2025, mabwawa 19 yanaendelea na ujenzi kwenye maeneo mbalimbali nchini.
Mheshimiwa Spika, vilevile katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 5.5 kwa ajili ya kukarabati mabwawa 15 ya ukubwa mdogo na wa kati sanjari kuhamasisiha uvunaji wa maji ya mvua kupitia mapaa ya nyumba hususani kwenye taasisi za umma kama mashule, zahanati, vituo vya afya, hospitali na ofisi mbalimbali.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved