Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 507 | 2025-06-04 |
Name
Mwita Mwikwabe Waitara
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tarime Vijijini
Primary Question
MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: -
Je, lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Vijiji vya Sirari, Nyamwaga na Nyamongo vilivyopo Tarime Vijijini?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Vijiji vya Sirari, Nyamwaga na Nyamongo vinapata huduma ya majisafi na salama kupitia vyanzo vya chemchem na visima virefu vilivyochimbwa kwenye maeneo hayo. Aidha, katika kuboresha zaidi huduma ya maji katika maeneo hayo, Serikali inatekeleza Mradi wa Miji 28 kutoka Ziwa Victoria kwenda katika Wilaya za Rorya na Tarime ambapo kukamilika kwake utanufaisha pia Kijiji cha Sirari. Mradi huo unatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2025/2026.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali itafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa miradi ya maji kwa ajili ya kufikisha huduma kwenye vijiji ambavyo havijafikiwa na Mradi wa Ziwa Victoria ikiwemo Vijiji vya Nyamwaga na Nyamongo, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved