Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 508 | 2025-06-04 |
Name
Francis Isack Mtinga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Iramba Mashariki
Primary Question
MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi kwa kiwango cha lami kilometa 42 barabara inayoelekea Makao Makuu ya Wilaya Mkalama?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, barabara inayoelekea Makao Makuu ya Wilaya ya Mkalama inaitwa Barabara ya Iguguno Shamba hadi Nduguti yenye urefu wa kilometa 42.6. Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa Serikali imekamilisha ujenzi kwa kiwango cha lami wa kilometa 2.5 katika Mji wa Iguguno. Kwa sasa Serikali inaendelea na taratibu za manunuzi ili kumpata mkandarasi wa ujenzi wa kilometa 10 kwa kiwango cha lami. Kwa sehemu iliyobaki Serikali itaendelea kutafuta fedha ili kuendelea na ujenzi, ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved