Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 509 | 2025-06-04 |
Name
Benaya Liuka Kapinga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbinga Vijijini
Primary Question
MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza upembuzi yakinifu na kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Nyoni – Maguu?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na ujenzi wa Barabara ya Nyoni – Maguu yenye urefu wa kilometa 30.55 kwa kiwango cha lami inafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa kipande cha barabara hiyo chenye jumla ya urefu wa kilometa 5.6 kinachopitia kwenye maeneo korofi yenye miteremko mikali tayari kimejengwa kwa kiwango cha lami na zege, ambapo kwa kilometa 4.6 kimejengwa kwa kiwango cha lami na kipande cheye urefu wa kilometa 1.0 kimejengwa kwa kiwango cha zege. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya kazi ya upembezi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved