Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 510 | 2025-06-04 |
Name
Hawa Mchafu Chakoma
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA Aliuliza: -
Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Kilindoni – Rasimkumbi - Mafia kilometa 52.16?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI Alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Kilindoni – Rasimkumbi - Mafia (kilometa 52.16) kwa awamu. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 na 2023/2024 Serikali imekamilisha kujenga jumla ya kilometa 2.15. Kwa sehemu iliyobaki (kilometa 50.13) iko katika hatua za manunuzi ya kumpata mkandarasi wa ujenzi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved