Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 239 | 2025-05-07 |
Name
Felista Deogratius Njau
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga uzio katika Kituo cha Afya cha Uru Kusini - Moshi Vijijini?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imepeleka jumla ya shilingi milioni 750 katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha afya cha Uru Kusini ambapo majengo matano ujenzi umekamilika na kituo hicho kinatoa huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Moshi itatenga shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa uzio wa Kituo cha afya Uru Kusini. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved