Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 241 | 2025-05-07 |
Name
Aysharose Ndogholi Mattembe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FLATEI G. MASSAY K.n.y. MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka Gari la Wagonjwa kwenye Kituo cha Afya cha Mgori Jimbo la Singida Kaskazini?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022, ilinunua magari 594 ya kubebea wagonjwa na usimamizi wa huduma za afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Halmashauri ya Wilaya ya Singida imepokea magari mawili ya kubebea wagonjwa na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Singida na Kituo cha Afya cha Mgori.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu kwa ajili ya ununuzi wa magari ya kubebea wagonjwa na kuyapeleka katika halmashauri kote nchini kwa ajili ya kutoa huduma kwenye hospitali na vituo vya afya. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved