Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 242 | 2025-05-07 |
Name
Stephen Lujwahuka Byabato
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukoba Mjini
Primary Question
MHE. STEPHEN L. BYABATO aliuliza:-
Je, kwa nini watumishi wanaojitolea wanapoajiriwa wasipangiwe katika Vituo walivyokuwa wakijitolea kama kipaumbele cha kwanza?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu ya Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma, Toleo Na.2 la Mwaka 2008, ikisomwa pamoja na Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura 298, Ajira katika Utumishi wa Umma hupatikana kwa ushindani na uwazi. Kujitolea katika Utumishi wa Umma huwezesha vijana kujipatia ujuzi wa ziada pamoja na kuwapa uzoefu na uwezo wa kushindana pindi ajira zinapotangazwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pale ambapo wanaojitolea wanafaulu usaili, majina yao hupelekwa kwa waajiri ambao huwapangia vituo vya kazi kulingana na mahitaji ya ikama iliyoidhinishwa katika vituo husika. Ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved