Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 18 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 233 | 2025-05-06 |
Name
Vita Rashid Kawawa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Primary Question
MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: -
Je, kwa nini ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma umesimama?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma unatekelezwa kwa awamu ambapo hadi sasa Serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 na tayari jengo la huduma za mionzi limekamilika sambamba na kusimikwa mashine ya CT-Scan na Digital X-Ray na tayari huduma zinatolewa. Aidha, ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) unaendelea na jengo la kusafisha figo (Dialysis).
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma, na mradi huu unatarajiwa kukamilika katika awamu tatu.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved