Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishat | 243 | 2025-05-07 |
Name
Zuberi Mohamedi Kuchauka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Liwale
Primary Question
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-
Je, lini majiko yanayotumia gesi yataanza kutumika katika Shule za Sekondari kote Nchini?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia mwezi Machi, 2025, Serikali kupitia wadau mbalimbali imewezesha jumla ya shule za sekondari 216 kuhamia katika matumizi ya nishatisafi ya kupikia ambapo kati ya hizo, shule za sekondari 146 zinatumia Gesi ya LPG. Aidha, Serikali kupitia REA inaendelea kutoa ruzuku ya ujenzi wa miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 20 Aprili, 2025, REA kupitia Wizara ya Nishati imepokea kibali kutoka TAMISEMI cha kufunga miundombinu ya huduma ya nishati safi ya kupikia katika shule 115 zikiwemo: shule za mikoa za sayansi za wasichana 16; shule za kitaifa za wavulana 7; shule za bweni za kawaida 66; na shule kongwe za sekondari 26. Serikali kupitia REA na wadau mbalimbali itaendelea kufunga miundombinu ya nishati ya kupikia katika shule za sekondari kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved