Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 244 | 2025-05-07 |
Name
Jesca Jonathani Msambatavangu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Iringa Mjini
Primary Question
MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza:-
Je, lini NHIF itajumuisha huduma za afya ya akili kwenye vifurushi vya bima ya afya?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, huduma za matibabu ya afya ya akili, ushauri nasaha na huduma nyingine za kibingwa ikiwemo huduma za utengamao ni baadhi ya huduma zilizoorodheshwa kama huduma muhimu za afya kwenye mwongozo wa matibabu (Standard Treatment Guideline) ambapo hutumika kama kigezo kikuu cha huduma za msingi zinazolipiwa na Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika utoaji wa huduma za matibabu kwa wagonjwa wa akili, Mfuko wa Bima (NHIF) hugharamia dawa zote kwa kuzingatia aina ya dawa na ngazi ya huduma kwa mujibu wa Mwongozo wa Matibabu (STG).
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved