Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 18 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 234 | 2025-05-06 |
Name
Angelina Adam Malembeka
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kurejesha kilimo cha pamba katika Mikoa ya Kusini mwa Tanzania?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mikoa ya Kusini mwa Tanzania ikiwemo Mkoa wa Mtwara, Lindi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Ruvuma hairuhusiwi kulima pamba kutokana na karantini iliyowekwa kufuatia uwepo wa funza mwekundu. Karantini hiyo iliwekwa tangu mwaka 1947 na kuhuishwa mwaka 2000 baada ya wakulima wa Halmashauri ya Chunya Mkoani Mbeya kuripoti uwepo wa funza huyo ambaye alisababisha uharibifu wa pamba kwa 100%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, utafiti uliofanyika mwaka 2022 katika mikoa yenye karantini ulithibisha kuwa funza mwekundu bado yupo katika maeneo hayo. Hivyo, mikoa hiyo bado haijaruhusiwa kurejesha kilimo cha pamba kwa lengo la kudhibiti kusambaa kwa funza huyo katika maeneo mengine ya uzalishaji wa pamba nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima katika maeneo yaliyowekewa karantini wanashauriwa kuendelea kulima mazao mengine ikiwemo korosho, ufuta, alizeti, chai, mihogo, mahindi na mbaazi kulingana na ekolojia ya maeneo waliyopo. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved