Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 245 | 2025-05-07 |
Name
Dr. Thea Medard Ntara
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:-
Je, upi mkakati wa kuzirudishia Hospitali za Mafunzo Vyuo Vikuu vyenye Programu ya Afya kama UDOM na MUHAS ili kukidhi miongozo ya Kimataifa?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliipa Wizara ya Afya jukumu la kusimamia Hospitali ya Mloganzila na Benjamin Mkapa ambazo zilikuwa Hospitali za Vyuo Vikuu vya MUHAS na UDOM, kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi sambamba na kuboresha ubora wa huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Vyuo Vikuu vya Dodoma na Muhimbili vinaendelea kutumia Hospitali hizi kufundishia wanafunzi wao. Ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved