Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 246 | 2025-05-07 |
Name
Dr. Paulina Daniel Nahato
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha Taasisi na Mashirika yanatoa fursa kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu kufanya mazoezi kwa vitendo?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKINOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha wanafunzi wanapata fursa za kufanya mafunzo kwa vitendo, vyuo vikuu nchini vimekuwa na utaratibu wa kuanzisha ushirikiano na taasisi na mashirika ambayo yanatoa huduma zinazoshabihiana na fani zinazotolewa vyuoni. Hadi sasa taasisi 19 za elimu ya juu zimeanzisha Kamati za Ushauri wa Kitasnia (Industrial Advisory Commitee) kama mkakati wa kuongeza nafasi na kuimarisha mafunzo kwa vitendo ambapo jumla ya mikataba 158 imesainiwa kati ya vyuo na taasisi binafsi na viwanda. Ninakushukuru sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved