Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 247 | 2025-05-07 |
Name
Mustafa Mwinyikondo Rajab
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dimani
Primary Question
MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB aliuliza:-
Je, Idara ya Uhamiaji ina mpango gani wa kujenga hospitali Zanzibar kama ilivyo kwa Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo kwa vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama, Idara ya Uhamiaji ina mpango wa kuwa na zahanati kwa lengo la kutoa huduma za afya kwa watumishi na jamii inayoizunguka. Serikali kupitia Idara ya Uhamiaji imefanya mawasiliano ya awali na Wizara ya Afya ya Zanzibar ili kupata mwongozo kuhusu namna bora ya uanzishwaji wa zahanati itakayokidhi mahitaji kwa jamii itakayohudumiwa. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved