Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 9 | Sitting 1 | Works, Transport and Communication | Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi | 6 | 2022-11-01 |
Name
Edward Olelekaita Kisau
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kiteto
Primary Question
MHE. EDWARD K. OLELEKAITA aliuliza: -
Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Arusha – Simanjiro – Kiteto hadi Kongwa kilometa 430 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Uchaguzi (CCM) 2020 – 2025?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Edward Kisau Olelekaita, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mnamo tarehe 27 Juni, 2022 ilitangaza zabuni kwa ajili ya kuonesha nia (Expression of Interest) kwa Makampuni ya Ujenzi kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Arusha – Simanjiro – Kiteto – Njiapanda ya Kongwa yenye urefu wa kilometa 453.42 kwa utaratibu wa EPC + Jumla ya Makampuni kumi na moja (11) yalikidhi vigezo na tarehe 22 Novemba, Zabuni hizi zitafunguliwa.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved