Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Je, lini Serikali italipa fidia eneo la Makaburi Idefu – Makambako ili kupisha ujenzi wa One Stop Centre?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kabla ya swali Mheshimiwa Deo Sanga anashukuru sana kwamba malipo ya fidia ile yamefanyika na swali lake namba moja ni kwa sababu malipo yameshafanyika na lile eneo la makaburi siyo kubwa, Serikali haioni umuhimu wa kulipa haraka ili ipate uhuru wa kuendelea na ujenzi wa One Stop Centre pale Makambako?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; pale Kilolo ambapo Makao Makuu ya Wilaya yamejengwa, kuna madai ya fidia ya muda mrefu na yalikwishawasilishwa Hazina mara kadhaa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuyaharakisha malipo yale ili wale wananchi pia waweze kupata haki yao? Nakushukuru.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nyamoga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kuhusu ulipaji wa fidia kule Idefu, Makambako, kwa kuwa tumeshalipa fedha nyingi sana shilingi bilioni 4.6 kilichobakia ni kidogo tu ni shilingi milioni 100. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ndani ya mwaka huu wa fedha tunaenda kulipa fidia iliyobakia. Upande wa Kilolo Serikali ipo tayari kufanya haraka, tunasubiri tu Mthamini Mkuu aweke idhini, akishatoa idhini yake tunaenda kulipa hiyo. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Je, lini Serikali italipa fidia eneo la Makaburi Idefu – Makambako ili kupisha ujenzi wa One Stop Centre?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi wa Gona, Sehemu ya Njia Panda pale Himo na Mabungo pale Uchira ambao nao wamepisha Serikali kujenga one stop center ya customs? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali ya nyongeza la Mheshimiwa Kimei, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Kimei suala hilo linatambulika Serikalini na tunalifanyia kazi. Awe na subira, fidia hiyo katika eneo alilolitaja italipwa kwa wakati mahususi. Ahsante. (Makofi)